Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
TAARIFA: Huduma Yetu ya Ufalme itaratibu Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa miezi ya mkusanyiko. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho yahitajiwayo ili kuruhusu watu wahudhurie Mkusanyiko wa Wilaya wa “Walimu wa Neno la Mungu.” Tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalotangulia mkusanyiko ili kurudia shauri linalowafaa lililoonyeshwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2001. Katika mwezi wa Oktoba, Mkutano wa Utumishi utapangwa ili kupitia mambo makuu ya mkusanyiko. Tukiwa mkusanyikoni twaweza kuandika mambo yatakayotusaidia katika mazungumzo hayo kutia ndani orodha ya mambo makuu tunayotaka kutumia kibinafsi maishani mwetu na katika huduma ya shambani. Kisha twaweza kujitayarisha kueleza jinsi ambavyo tumetumia madokezo hayo tangu tulipohudhuria mkusanyiko. Tutajengana kwa kueleza jinsi ambavyo tumenufaika na mafundisho mazuri tuliyopokea.
Juma Linaloanza Julai 9
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Zungumzieni taarifa iliyo juu kuhusu marekebisho ya Mkutano wa Utumishi na yale ambayo yatafanywa kwenye Mkutano wa Utumishi wa Oktoba, wakati mambo makuu ya mkusanyiko wa wilaya yatakapozungumziwa.
Dak. 17: Ripoti ya Utumishi ya Machi. Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi kama hotuba na mahoji. Kazia ripoti ya utumishi wa shambani ya Machi ya nchi na ripoti ya utumishi wa shambani ya Aprili ya kutaniko lenu. Hoji wahubiri mbalimbali ambao walijitahidi zaidi katika huduma mwezi wa Aprili. Waombe wasimulie shangwe waliyopata kutokana na kushiriki kikamili na kile wanachofanya ili kuendelea na bidii hiyo katika huduma.—Ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2001, fungu la 28-30.
Dak. 20: “Je, Waweza Kutumikia Mahali Palipo na Uhitaji Mkubwa Zaidi?”a Tia ndani mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo ambayo wahubiri wa kwenu wamepata katika eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida.—Ona kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 112-113.
Wimbo 42 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Vijana—Hesabuni Kimbele Gharama ya Kazi-Maisha Yenu. Baba na mwana au binti yake tineja wamwendea mzee aliye na ujuzi katika kazi ya kimwili. Baada ya kufikiria sehemu ya Mkutano wa Utumishi majuma mawili yaliyopita kuhusu kuchagua kazi-maisha, kijana huyo anafikiria kwa uzito kufanya utumishi wa painia wa kawaida lakini hana uhakika kuhusu jinsi atakavyojiruzuku. Mzee huyo akazia uhitaji wa kuwa na usawaziko. (Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1999, ukurasa wa 11, fungu la 13) Ni jambo la hekima kujifunza kazi fulani ili uwe tayari kujiruzuku. Wengi wamefaulu kwa kujifunza kazi zisizohitaji wakati mwingi na fedha nyingi. (Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1996, ukurasa wa 14; Vijana Huuliza, ukurasa wa 178) Wanazungumzia pamoja Amkeni!, Machi 8, 1996, ukurasa wa 9-11, na baadhi ya madokezo ya kupata au kutafuta kazi ya kimwili inayofaa.
Dak. 20: Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? Mazungumzo na wasikilizaji kukiwa na onyesho. Chunguzeni broshua hii na mzungumzie jinsi inavyoweza kutumiwa kujulisha wengine kutuhusu na kuhusu kazi yetu. Inaeleza sisi ni nani (ukurasa wa 3-5), yakazia baadhi ya historia na utendaji wetu wa kisasa (ukurasa wa 6-11), hutaja imani zinazotutofautisha na dini nyingine (ukurasa wa 12-14), hueleza kuhusu habari njema tunazohubiri na jinsi tunavyozihubiri (ukurasa wa 15-21), huonyesha jinsi ambavyo kazi yetu hunufaisha jamii (ukurasa wa 22-24), hueleza jinsi ambavyo tengenezo letu limeenea ulimwenguni (ukurasa wa 25-26), na hujibu maswali ambayo kwa kawaida yanaulizwa kutuhusu (ukurasa wa 27-31). Toa onyesho la mhubiri akitumia broshua hii kujibu mwenye nyumba anayeuliza mojawapo ya maswali yaliyo kwenye ukurasa wa 29, kisha mhubiri atoe mwaliko ulio kwenye ukurasa wa nyuma. Tia moyo wote watumie broshua hii kuwajulisha watu wa ukoo wasio Mashahidi kutuhusu, kuamsha kupendezwa katika ziara za kurudia, na kuelekeza mafunzo ya Biblia kwenye tengenezo.
Wimbo 50 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Pia taja jinsi ya kutumia kijitabu Habari Njema kwa Mataifa Yote inapowezekana.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Jitayarishe Kujifunza Unabii wa Isaya!”b Taja kifupi jinsi tutakavyonufaika kwa kujifunza kitabu cha Isaya. (Ona sura ya 1, fungu la 10-12, katika Unabii wa Isaya I.) Tia moyo wote wahudhurie Funzo la Kitabu la Kutaniko kwa ukawaida.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Julai.
Dak. 20: Vijana—Iweni na Ufahamu Mnapopangia Elimu Yenu. Mzee aongea na wazazi kadhaa na vijana wao kuhusu elimu ya ziada. Mzee aongoza mazungumzo hayo kulingana na Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1999, ukurasa wa 16-17, fungu la 11-13, akikazia kwa nini huduma ya wakati wote yapaswa kutangulizwa. (Mnara wa Mlinzi, Desemba 1, 1996, ukurasa wa 18-19, fungu la 13-15) Kisha kikundi hicho chazungumzia shauri linalopatikana katika Amkeni!, Machi 8, 1998, ukurasa wa 20-21, linalokazia uhitaji wa kutumia busara katika kuchanganua faida na hasara za elimu ya ziada na kuchagua ile itakayowasaidia kujitegemeza huku wakiendelea kuhubiri kwa bidii. Wote wakubali kwamba wanapaswa kuongozwa na shauri la Yesu la kuweka faida za Ufalme kwanza.—Mt. 6:33.
Dak. 15: “Enyi Wazazi Msipuuze Uvutano wa Televisheni kwa Watoto Wenu.”c
Wimbo 57 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 6
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Alika wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa wakati wa mahubiri ya vivi hivi walipokuwa wakisafiri, wakiwa likizoni, au kutembelea watu wa ukoo wasio Mashahidi.
Dak. 10: “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Hotuba. Tangaza tarehe ya kusanyiko linalofuata ikiwa yajulikana. Wote wapaswa kujitahidi kualika wanafunzi wa Biblia. Tia moyo wahubiri wasiobatizwa wafikirie kwa uzito kuonyesha wakfu wao kwa Yehova kwenye kusanyiko linalofuata ikiwa hawatabatizwa kwenye mkusanyiko wa wilaya unaokuja. Sihi wote wahudhurie vipindi vyote kila siku.
Dak. 20: “Usisite-Site!”d Wakati ukiruhusu, simulia mambo yaliyoonwa kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Desemba 15, 1999, ukurasa wa 25.
Wimbo 63 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
d Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.