Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Oktoba 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tia moyo kila mtu achunguze sura ya 1 ya kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli au kwa walio na video watazame United by Divine Teaching wakijitayarisha kwa mazungumzo ya Mkutano wa Utumishi wa juma la Oktoba 22. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, toa maonyesho mawili mafupi ya jinsi ya kutoa magazeti, ukitumia Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15 na onyesho jingine ukitumia Amkeni!, Oktoba 22. Ikiwa matoleo hayo hayako katika kutaniko lenu wakati huu, tumia matoleo mawili mapya yaliyopo.
Dak. 35: “Je, Unatumia Yale Uliyojifunza Katika Mkusanyiko wa Wilaya wa ‘Walimu wa Neno la Mungu’?” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya programu ya mkusanyiko, yakishughulikiwa na kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi. Baada ya utangulizi wa dakika moja, tumia dakika 10-12 kuzungumzia programu ya kila siku. Eleza kifupi mambo makuu ya kila kichwa kidogo, kisha uombe wasikilizaji watoe maelezo juu ya (1) jinsi ambavyo wamejitahidi kutumia mafundisho hayo, (2) jinsi ambavyo wamenufaika kwa kuyatumia, na (3) mambo wanayohitaji kufanya. Fanya mazungumzo yawe machangamfu kwa kutumia maswali yenye kuamsha fikira. Saidia wote wathamini uhitaji wa kutumia kile ambacho wamejifunza.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Je, Una ‘Moyo Mtiifu’? (1 Fal. 3:9) Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1998, ukurasa wa 29-31. Zungumzia njia ambazo tunaweza kuonyesha utii tunaposhirikiana na kutaniko.
Dak. 20: Tumia Magazeti Yetu Vizuri. Mwangalizi wa utumishi na mtumishi wa magazeti wanazungumzia wasiwasi wao kuhusu ugawanyaji wa magazeti. Wanataja idadi ya magazeti ambayo kutaniko hupokea kila mwezi ikilinganishwa na idadi iliyoachiwa watu. Inaonekana kwamba, magazeti mengi yanawekwa tu au yanatupwa. Wahubiri wanaweza kutumiaje magazeti yetu vizuri zaidi? Akina ndugu hao wanazungumzia mambo yaliyo katika sehemu ya Mkutano wa Utumishi yenye kichwa “Kazia Uangalifu Magazeti!” juma la Oktoba 4, 1999. Wanazungumzia jambo lililoonwa katika Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1998, ukurasa wa 28-29, na kuchunguza jinsi madokezo yaliyopo yanavyoweza kutumiwa. Kila mtu anatiwa moyo kujaribu utoaji unaoonyeshwa kila mwezi katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Wimbo 156 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, toa maonyesho mawili mafupi ya utoaji wa magazeti, moja ukitumia gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na jingine ukitumia gazeti la Amkeni! la Novemba 8 au matoleo mapya yaliyo katika kutaniko.
Dak. 10: Utajibuje? Elezea kifupi ukurasa wa 184-185 wa kitabu Kutoa Sababu, ambapo jibu lililo wazi lapatikana kuhusu swali, ‘Mashahidi wa Yehova hutumia njia gani kueleza Biblia?’ Toa onyesho lililotayarishwa vizuri la jinsi ya kujibu swali hilo katika ziara ya kurudia, halafu mwalike mtu huyo kwa uchangamfu ahudhurie mikutano ya kutaniko.
Dak. 25: Mazungumzo ya sura ya 1 ya kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli. Kazia umuhimu wa kuendeleza umoja wetu kwa kuepuka mambo yanayosababisha migawanyiko. Mahali ambapo watu wana video tumieni sehemu yenye kichwa “Kutazama Muungano Halisi wa Kidugu Kwenye Video United by Divine Teaching.” Mazungumzo na wasikilizaji. Tumia fungu la kwanza unapotoa utangulizi wa sehemu hiyo na fungu la mwisho unapomalizia sehemu hiyo. Ili kufanya mazungumzo ya video hiyo yawe machangamfu, uliza kila swali lililo katika sehemu hiyo. Ikiwa kuna wowote katika kutaniko ambao wamewahi kuhudhuria mikusanyiko katika nchi nyingine, waombe wasimulie jinsi walivyohisi walipojionea wenyewe ukubwa na umoja wa tengenezo letu. La sivyo, waombe wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kuchangamsha kutoka katika Kitabu-Mwaka cha 1994, ukurasa wa 7-9, na 1995 Yearbook, ukurasa wa 8-11. Mahali ambapo watu wana video, tutachunguza video To the Ends of the Earth mwezi wa Desemba.
Wimbo 47 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 29
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Oktoba. Toleo la vichapo la Novemba ni broshua Anataka au kitabu Ujuzi. Toa onyesho hili fupi: “Katika nyakati hizi ngumu kiuchumi, watu wengi wana shida ya kupata riziki. Je, wafikiri serikali za kibinadamu zitatatua tatizo hili kwa njia itakayofaidi watu wote? [Ngoja jibu.] Nimeona ahadi hii ya Biblia kuwa yenye kutia moyo sana.” Soma Zaburi 72:12-14. Kisha toa broshua Anataka au kitabu Ujuzi, ukitoa maelezo mafupi kutoka kwenye kichapo hicho.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 18: “Mazoea Yako ya Kujilisha Kiroho Ni Yenye Kuridhisha Kadiri Gani?”a Alika watu watoe maelezo ya ziada kuhusu Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1997, ukurasa wa 28-31, wakieleza ni kwa nini ni lazima tujitahidi kudumisha mazoea mazuri ya kujilisha kiroho na jinsi tunavyoweza kufanya hivyo.
Wimbo 181 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 18: Familia Yajitayarisha kwa Ajili ya Mikutano. Baba azungumza na familia yake jinsi wote wanavyoweza kujitayarisha ili kushiriki ifaavyo kwenye mikutano. Wakitumia miongozo iliyo katika Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1999, ukurasa wa 19-20, fungu la 9, wanatayarisha maelezo watakayotoa kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi la juma hili. (1) Kila mshiriki wa familia achagua swali moja au mawili atakayojibu. (2) Baada ya kuchunguza mafungu hayo, wanaeleza majibu yao kwa maneno yao wenyewe. (3) Wanateua maandiko yasiyonukuliwa yenye mambo makuu, wanazungumzia jinsi kila andiko linavyohusiana na habari hiyo, na kupanga yale watakayosema ili kuyahusisha katika habari hiyo. Wote wana hamu ya kushiriki katika mkutano huo.
Dak. 17: “Lengo Letu Ni Nini?”b Kazia umuhimu wa kusaidia wanafunzi waone faida ya kuhudhuria mikutano ya kutaniko. Tia ndani onyesho lililotayarishwa vizuri la jinsi ya kufanya hivyo, ukitumia kitabu Ujuzi sura ya 17, fungu la 6-8.
Wimbo 186 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.