Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/01 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 12
  • Juma Linaloanza Novemba 19
  • Juma Linaloanza Novemba 26
  • Juma Linaloanza Desemba 3
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 11/01 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Novemba 12

Wimbo 170

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.

Dak. 15: “Mtegemee Yehova Akupe Nguvu.”a Tia ndani maelezo mafupi kutoka kwenye Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1999, ukurasa wa 18-19, fungu la 6-8.

Dak. 22: “Jihadhari na Misemo ya Kawaida ya Ushirikina.” Mazungumzo na wasikilizaji yakifanywa na mwangalizi wa utumishi.

Wimbo 191 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 19

Wimbo 172

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 22: “Sitawisha Nguvu Zako za Ufahamu.”b Mzee azungumzia kwa uchangamfu programu ya siku ya kusanyiko la pekee iliyofanywa katika mwaka wa utumishi uliopita.

Wimbo 195 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 26

Wimbo 177

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Novemba. Tayarisha vizuri maonyesho mawili ya kutoa magazeti kwa kutumia madokezo yaliyo katika safu yenye kichwa “Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti.” Tumia gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 katika onyesho la kwanza na katika lile jingine tumia gazeti la Amkeni! la Desemba 8 au matoleo ya karibuni yanayopatikana kutanikoni. Kisha eleza jinsi ya kupata madokezo ya kutumia wakati wa kutoa broshua yoyote yenye kurasa 32 inayopatikana kutanikoni kwa ajili ya toleo la Desemba. Ikiwa Watch Tower Publications Index yapatikana, angalia chini ya kichwa “Presentations” na kichwa kidogo kilicho katikati kinachosema “List by Publication.” Toa mfano mmoja au miwili. Wakumbushe wote watumie sana trakti zinazopatikana katika kutaniko lenu.

Dak. 15: “Nitapata Wapi Wakati?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani mambo makuu kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2000, ukurasa wa 20-21, fungu la 9-10, chini ya kichwa kidogo “Jinsi Ambavyo Wengine Hupata Wakati wa Kujifunza.” Alika wasikilizaji wasimulie jinsi ambavyo wamefanikiwa kukomboa wakati ili kufanya mambo ya maana zaidi kwa kuepuka mambo yasiyo ya lazima. Kazia uhitaji wa kupanga ratiba ya funzo la kibinafsi na la familia, mikutano ya kutaniko, huduma ya shambani, na usomaji wa Biblia kila siku.

Dak. 15: Vijana Wanamsifu Yehova. Mazungumzo na wasikilizaji. Katika makutaniko mengi kuna vijana ambao hushiriki katika kazi ya kuhubiri. Jambo hilo linafaa hata ingawa wanawahubiria hasa watu wazima. (Zab. 148:12, 13; Mt. 21:15, 16) Vijana hufurahia sana utumishi wa shambani wakati wazazi na wahubiri wengine wanapopendezwa nao na wanapowazoeza na kuwatia moyo. Alika wasikilizaji wadokeze jinsi wanavyoweza kuhusisha vijana katika kazi ya kwenda mlango hadi mlango na kufanya ziara za kurudia. Waulize wazazi wasimulie mambo ambayo wamefanya ili kuwasaidia watoto wao wajifunze jinsi ya kutoa magazeti, kutumia Biblia wanapohubiri, na kuongea bila wasiwasi milangoni. Kazia faida za kuwapongeza watoto. Hoji kijana mmoja au wawili ambao ni wahubiri, na uwaombe waeleze mambo wanayofurahia kuhusu kazi ya kuhubiri na kwa nini wanayafurahia.

Wimbo 198 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 3

Wimbo 179

Dak. 8: Matangazo ya kwenu.

Dak. 17: Yaliyomo Katika Kitabu Kutoa Sababu. Mazungumzo na wasikilizaji. Zungumzieni mifano inayofuata inayoonyesha jinsi sehemu mbalimbali katika kitabu hicho ni muhimu katika kueleza mafundisho ya Biblia: Fasili, kama vile ya “Ufalme” (ukurasa wa 325) au ya “roho” (ukurasa wa 261); tafsiri mbalimbali zinazoonyesha mahali na jinsi jina la Mungu linavyotumiwa katika Biblia (ukurasa wa 420-422) au ukweli kuhusu motoni (hell) (ukurasa wa 205-207); orodha, zinazoeleza imani ambayo hututofautisha na dini nyingine (ukurasa wa 179-180) au jinsi mtu anavyoweza kujua dini ya kweli (ukurasa wa 73-75); historia, inayoonyesha asili ya Krismasi (ukurasa wa 290-292) au kutokuwemo kwa Wakristo wa mapema (ukurasa 142-144); uthibitisho wa sayansi, unaounga mkono uumbaji (ukurasa wa 397-399) au unaoonyesha madhara ya kutumia bangi na tumbaku (ukurasa wa 58-61). Tia moyo wahubiri watumie msaada huu mzuri wa kufundisha fursa zinapotokea katika huduma ya shambani.

Dak. 20: “Baraka Tunazopata kwa Kuthamini Upendo wa Yehova—Sehemu ya 1.”c Mnapozungumzia fungu la 3-6, waombe wahubiri kutanikoni wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo ambayo wamepata kwa kuhubiri nyumba hadi nyumba, kutoa ushahidi wa barabarani, na katika ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia.

Wimbo 200 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki