‘Weka Kando Kitu Fulani’
Katika kutaniko la awali la Kikristo, kulikuwa na mahitaji ya kimwili yaliyopaswa kushughulikiwa. Kila mtu alipoendelea kufanikiwa, alisihiwa “aweke kando kitu fulani” kiwe mchango wa kushughulikia mahitaji hayo. (1 Kor. 16:1-3) Kwa sababu ya ukarimu wao, wote walipata shangwe ya kutoa “maonyesho mengi ya shukrani kwa Mungu.”—2 Kor. 9:11, 12.
Leo kazi ya ulimwenguni pote ya watu wa Yehova yaendelea kupanuka, hivyo twahitaji twendelee kuitegemeza kifedha. Ingefaa sisi pia ‘tuweke kando kitu fulani’ kwa ukawaida ili kusaidia katika uhitaji huu. (2 Kor. 8:3, 4) Twaweza kutoa vitu vya kimwili kwa njia nyingi. (Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2001, ukurasa wa 28-29.) Sisi huiona hiyo kuwa fursa ya pekee inayoleta furaha ya kweli.—Mdo. 20:35.