Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/02 uku. 8
  • Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Tangu Utotoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Tangu Utotoni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Wazazi, Pendezweni na Watoto Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je! Mtoto Wako Mdogo ‘Anakua Kuelekea Wokovu’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Wazoeze Watoto Wako Kuwa Wahudumu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kujenga Familia Yenye Nguvu Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 1/02 uku. 8

Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Tangu Utotoni

1 “Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.” (Mit. 22:6) Wazazi, ikiwa hamtaki watoto wenu ‘waiache’ njia ya kweli, mafundisho hayo yapasa kuanza lini? Tangu utotoni!

2 Paulo aliposema kwamba Timotheo alianza kufunzwa ‘tangu utotoni,’ ni wazi alimaanisha tangu alipokuwa mvulana mdogo. (2 Tim. 3:14, 15) Hivyo, Timotheo alikuja kuwa mtu wa kiroho sana. (Flp. 2:19-22) Wazazi, nyinyi pia lazima mwanze kuwafundisha watoto wenu ‘tangu utotoni’ ili ‘wakue mbele za Yehova.’—1 Sam. 2:21.

3 Wapeni Maji Wanayohitaji Ili Wakue: Kama vile mimea inavyohitaji maji kwa ukawaida ili ikue hadi kufikia miti mikubwa, watoto wa umri wote wanahitaji kupewa maji ya kweli ya Biblia ili wakue kufikia kuwa watumishi wa Mungu wakomavu. Njia ya msingi ya kuwafundisha watoto kweli na kuwasaidia wawe rafiki za Yehova ni kupitia funzo la Biblia la familia, la kawaida. Lakini wazazi, fikirieni muda ambao watoto wenu wanaweza kuwa makini. Kuwafundisha watoto wachanga mara nyingi lakini kwa vipindi vifupi kutakuwa na matokeo zaidi kuliko kuwafundisha mara chache kwa vipindi virefu.—Kum. 11:18, 19.

4 Msidhani kwamba watoto wenu hawawezi kujifunza. Waambieni hadithi za watu wa nyakati za Biblia. Waambieni wachore picha zinazoonyesha matukio ya Biblia au waigize matukio hayo. Tumieni video na kaseti zetu, kutia ndani drama za Biblia. Fanyeni funzo la familia lifaane na umri na uwezo wa kujifunza wa watoto wenu. Watoto wachanga watafundishwa mambo ya msingi kwa muda mfupi; lakini mtoto anapokuwa mkubwa, anapaswa kufundishwa mambo mengi hatua kwa hatua. Fanyeni mafundisho ya Biblia yawe machangamfu na yenye mambo mbalimbali. Mkitaka watoto wenu ‘wafanyize hamu’ ya lile Neno, fanyeni funzo liwe lenye kupendeza kwelikweli kadiri mwezavyo.—1 Pet. 2:2.

5 Wahusisheni Katika Kutaniko: Wekeeni watoto wenu miradi ya hatua kwa hatua ili wahusike kabisa katika kutaniko. Mradi wao wa kwanza unaweza kuwa upi? Wazazi wa watoto wawili wadogo walisema: “Tulianza kuwafundisha watoto wote wawili waketi kimya kwenye Jumba la Ufalme.” Baadaye, wasaidieni watoto watoe maelezo mikutanoni kwa maneno yao wenyewe, na waweke mradi wa kujiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Miradi mizuri inayoweza kuwekwa kuhusiana na utumishi wa shambani ni kama vile kuachia mtu trakti, kusoma andiko, kutoa gazeti, na kuwa na mazungumzo yenye kujenga pamoja na wenye nyumba.

6 Wekeni Kielelezo kwa Matendo: Je, watoto wenu huwasikia mkiongea juu ya Yehova kila siku na kusali? Je, wanawaona mkisoma Neno lake, mkihudhuria mikutano, mkishiriki katika utumishi wa shambani, na kufurahia kufanya mapenzi ya Mungu? (Zab. 40:8) Ni muhimu watoto waone mkifanya mambo hayo na mkiyafanya pamoja nao. Msichana mmoja alisema hivi kuhusu mama yake ambaye alikuwa amelea watoto sita waliokuja kuwa Mashahidi waaminifu: “Jambo lililotuvutia zaidi lilikuwa kielelezo cha Mama kwa kuwa kielelezo chake kilikuwa bora.” Mzazi mmoja mwenye watoto wanne alisema: “Usemi ‘Yehova ndiye wa kutangulizwa’ haukuwa msemo wa kawaida tu lakini tuliishi kulingana nao.”

7 Wazazi, anzeni mapema kuwafundisha watoto wenu kweli ya Neno la Mungu, mkiwawekea miradi ya hatua kwa hatua, na kuwawekea kielelezo bora. Mtafurahi kwamba mlifanya hivyo!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki