Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 uku. 1
  • Shangwe ya Kuungana Pamoja na Yehova na Mwana Wake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shangwe ya Kuungana Pamoja na Yehova na Mwana Wake
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Tunahudhuria Ukumbusho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Kukumbuka Fidia kwa Uthamini
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Yehova Hubariki Jitihada Zetu za Kuadhimisha Ukumbusho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • “Endeleeni Kufanya Hivi kwa Kunikumbuka Mimi” Ukumbusho wa Kifo cha Yesu Utakuwa Aprili 2
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 uku. 1

Shangwe ya Kuungana Pamoja na Yehova na Mwana Wake

Tukio Muhimu Zaidi Mwaka Huu Litaadhimishwa Machi 28

1 Kwa kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana baada ya jua kutua Machi 28, 2002, tutaonyesha kwamba tuna shangwe ya kuungana pamoja na Yehova Mungu na Yesu Kristo. Katika pindi hiyo ya pekee sana, mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta watafurahia “ushirika” wa pekee walio nao pamoja na warithi wengine wa Ufalme, pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake. (1 Yoh. 1:3; Efe. 1:11, 12) Mamilioni ya “kondoo wengine” watatafakari kuhusu fursa yao ya pekee ya kuungana pamoja na Yehova na Mwana wake, wakiwa na kusudi moja la kutimiza kazi ya Mungu!—Yn. 10:16.

2 Kufanya Kazi Pamoja Tukiwa na Uhusiano wa Karibu Sana: Sikuzote Yehova na Yesu wamefurahia kuungana. Walifurahia ushirika wa karibu kwa muda mrefu sana kabla ya mwanadamu kuumbwa. (Mika 5:2) Kwa hiyo walikuwa na uhusiano wa karibu sana na wenye upendo. Akiwa hekima inayofananishwa na mtu, Mwana huyo wa kwanza alisema hivi kabla ya kuwa binadamu: “Nikawa furaha yake [Yehova] kila siku; nikifurahi daima mbele zake.” (Mit. 8:30) Kuishi pamoja na Chanzo cha upendo kwa miaka mingi sana na kushirikiana naye kwa ukaribu sana kulikuwa na matokeo makubwa sana kwa Mwana wa Mungu!—1 Yoh. 4:8.

3 Akifikiria uhitaji wa wanadamu kukombolewa, Yehova alimchagua Mwana wake mzaliwa-pekee, ambaye alipenda wanadamu sana, ili kutoa dhabihu ya fidia ambayo inatupatia tumaini letu la pekee. (Mit. 8:31) Kama vile Yehova na Mwana wake wameungana katika kutimiza kusudi moja, twadumu tukiwa tumeungana nao huku tukiwa na umoja sisi kwa sisi katika upendo wenye nguvu, tukifanya mapenzi ya Mungu kwa shangwe.

4 Kuonyesha Shukrani Zetu za Moyoni: Kwa kuhudhuria Ukumbusho na kusikiliza kwa uangalifu na kwa heshima, twaonyesha shukrani zetu za kutoka moyoni kwa upendo wa Yehova na dhabihu ya Mwana wake kwa ajili yetu. Kielelezo cha Yesu cha upendo, uaminifu wake hadi kifo ili kuandaa fidia, na utawala wake akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu uliosimamishwa, na vilevile baraka ambazo Ufalme huo utaletea wanadamu, vitakaziwa. Pia tutakumbushwa uhitaji wa kuonyesha imani yetu daima, huku tukifanya kazi kwa bidii kupatana na mapenzi ya Yehova tukiwa “wafanyakazi wenzi katika kweli.”—3 Yoh. 8; Yak. 2:17.

5 Kusaidia Wengine Washiriki Nasi: Mabaraza ya wazee yapaswa kujitahidi zaidi kutia moyo Mashahidi wote wasiotenda katika eneo lao wahudhurie Ukumbusho wa Kifo cha Kristo. (Mt. 18:12, 13) Andika orodha ya wale watakaotembelewa ili yeyote asisahaulike.

6 Je, unajua wengine ambao wangeweza kuhudhuria Ukumbusho? Wasaidie wathamini pindi hiyo. Waalike kwa uchangamfu, na uwafanye wahisi kuwa wamekaribishwa. Na tufanye yote tuwezayo kualika wanafunzi wetu wote wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa, na pia washiriki wa familia na watu tunaowafahamu, kwenye tukio hilo muhimu zaidi mwaka huu. Faida za fidia zingali zapatikana kwa wote wanaojifunza “thamani iliyo bora zaidi ya ujuzi wa Kristo Yesu.” (Flp. 3:8) Wale wanaodhihirisha imani katika dhabihu ya Kristo wanaweza kupata tumaini hakika la uhai udumuo milele.—Yn. 3:16.

7 Usipuuze kamwe matokeo ambayo Ukumbusho unaweza kuwa nayo kwa watu wenye mioyo minyofu. Miaka miwili iliyopita kwenye nchi ya kisiwa cha Papua New Guinea, watu 11 wenye kupendezwa walisafiri katika mashua ndogo kwa muda wa saa 17 katika bahari iliyochafuka ili kuhudhuria Ukumbusho. Kwa nini walifanya hivyo? Walisema hivi: “Tulitaka kuadhimisha Ukumbusho wa Kristo na waabudu wenzetu wa Yehova; kwa hiyo tukafunga safari hiyo.” Fikiria bidii iliyoonyeshwa na watu hao wenye kupendezwa na jinsi walivyothamini shangwe ya kuungana pamoja na Yehova, Mwana wake, na udugu wa Kikristo!

8 Wape wote wenye kupendezwa fursa ya kuwa na funzo la Biblia. Watie moyo wahudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na kuwaambia wengine kweli wanazojifunza. Wasaidie ‘kutembea katika nuru’ na ‘kuzoea kweli’ kwa kutumia kanuni za Biblia maishani mwao. (1 Yoh. 1:6, 7) Wasaidie kusitawisha uhusiano wa karibu sana pamoja na Yehova na kuzidi kuthamini fursa ya pekee waliyo nayo ya kufanya mapenzi yake kwa umoja.

9 Ni pendeleo bora kama nini kuwa na shangwe ya kuungana ‘katika roho moja, kwa nafsi moja tukipigana sambamba kwa ajili ya imani ya habari njema.’! (Flp. 1:27, 28) Na tutazamie kushirikiana pamoja kwa upendo kwenye Ukumbusho mnamo Machi 28, tukimshukuru Yehova na Mwana wake sikuzote!—Luka 22:19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki