Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Machi 11
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili tofauti ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 15 na Amkeni! la Februari 22. Katika kila kisa, onyesha njia tofauti ya kushughulikia usemi huu wa kuzuia mazungumzo, “Mimi sipendezwi.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 16.
Dak. 12: Boresha Ufundishaji Wako Shambani. Zungumzia madokezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1996 kuhusu jinsi ya kuongoza mafunzo ya Biblia. Kazia umuhimu wa kujitayarisha kikamili kwa ajili ya funzo, ukifikiria mahitaji ya mwanafunzi. Toa onyesho fupi ukitumia sehemu fulani ya kitabu Ujuzi ili kuonyesha jinsi mhubiri anavyoweza kutenga mambo makuu na maandiko machache ya msingi ili ayatumie anapoenda kwa mwanafunzi.
Dak. 20: “Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora.”a Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Tia moyo wote washiriki kikamili katika huduma wakijitayarisha kwa ajili ya mwadhimisho wa Ukumbusho mnamo Machi 28. Zungumzia jinsi ambavyo vikaratasi vya mwaliko vyaweza kutumiwa ifaavyo. Waombe wahubiri wasimulie jinsi walivyofaulu kuwaalika watu wa ukoo, majirani, wanafunzi wa Biblia, na watu wengine wenye kupendezwa wahudhurie Ukumbusho mwaka uliopita na shangwe waliyopata. Tia moyo wote wanaoweza wafanye upainia-msaidizi mwezi wa Aprili na wachukue fomu ya ombi baada ya mkutano.
Wimbo 82 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Zungumzia “Vikumbusho vya Ukumbusho.” Tia moyo wote wafuate ratiba ya usomaji wa Biblia inayoanza Machi 23-28 kwa ajili ya Ukumbusho, kama inavyoonyeshwa katika kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2002.
Dak. 15: “Shangwe ya Kuungana Pamoja na Yehova na Mwana Wake.” Mzee atoe hotuba ya Kimaandiko inayochochea. Tia moyo kila mtu ajitahidi sana kati ya sasa na Machi 28 kualika watu wengi iwezekanavyo wahudhurie Ukumbusho pamoja nasi.
Dak. 20: “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza.” Ishughulikiwe na mwangalizi-msimamizi. Soma maandiko na kueleza matumizi yake wakati ukiruhusu.
Wimbo 45 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 25
Dak. 14: Matangazo ya kwenu. Eleza kwamba si kuchelewa mno kuleta ombi la kufanya upainia-msaidizi mwezi wa Aprili. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga mzee aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1 na kijana aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Amkeni! la Machi 8. Baada ya kila onyesho, kazia mambo mazuri ya utoaji huo. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 16: Tumia Kitabu Kutoa Sababu Kutia Moyo. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kila mtu anahitaji kitia-moyo chenye upendo mara kwa mara. Kwa hiyo, sote twapaswa kuona uhitaji wa ‘kusema kwa kuliwaza’ wengine, kutia ndani walioshuka moyo tunaokutana nao katika huduma. (1 The. 5:14) Ukitumia kitabu Kutoa Sababu, omba wasikilizaji wataje jinsi wanavyoweza kutumia Maandiko kumtia moyo mtu fulani anayekabili mojawapo ya majaribu yanayotajwa kwenye ukurasa wa 106-110. Dokeza kila mtu ajaribu kumtia moyo mtu fulani wakati wowote kukiwa na uhitaji wa kufanya hivyo.—Gal. 6:10.
Wimbo 131 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 1
Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Machi.
Dak. 18: “‘Zawadi Zikiwa Wanadamu’ Huchunga Kundi la Mungu kwa Hamu.” Hotuba itolewe na mzee. Zungumzia maandiko yaliyotajwa. Onyesha jinsi mambo yenye kutia moyo yanavyoweza kutokezwa na jinsi yanavyotokezwa na ziara za uchungaji kwa wasiotenda na kwa kuwasaidia wagonjwa wafanye yale wawezayo. Wachungaji wenye upendo wanathamini jitihada za moyo wote za kundi za kuendelea kuwa watendaji katika utumishi wa Yehova.
Dak. 20: “Ongeza Shangwe Yako ya Kuhubiri.”b Unapozungumzia fungu la 5, omba madokezo yanayofaa juu ya jinsi ya kupata matokeo mazuri zaidi katika eneo lenu. Onyesha mfano mmoja au miwili ya jinsi tunavyoweza kumwendea mtu na kumhubiria kifupi. Tia moyo kila mtu atafute fursa za kuhubiri juma hili.
Wimbo 15 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.