Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Iwapo mtu anapendezwa unapomrudia, panga kumpelekea magazeti kwa ukawaida. Watu wakipendezwa, toa broshua Anataka au Rafiki ya Mungu na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini? au kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa wenye nyumba wana vichapo hivyo, toa broshua inayofaa ambayo kutaniko inayo akibani. Julai: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa inapofaa.
◼ Mahubiri yetu ya kila mwaka ya eneo la mbali yatafanywa Julai na Agosti. Makutaniko yaliyo na maombi hususa ya kuhubiri eneo la mbali yanaweza kuandikia ofisi ya tawi kabla ya Mei 15, 2002. Kutaniko lolote ambalo halijapewa eneo la mbali laweza kupanga kuhubiri eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida.
◼ Beji za kusanyiko la wilaya la mwaka wa 2002 katika Kifaransa, Kiganda, Kiingereza, Kirundi, na Kiswahili zitatiwa ndani ya upakizi wa vichapo. Si lazima ziombwe. Beji zitapakiwa kwa mafungu ya kadi 25 ikitegemea ukubwa wa kila kutaniko. Ikiwa beji za ziada zahitajiwa na makutaniko, zapasa kuombwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Vifuko vya beji vya plastiki vyapaswa kuombwa kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevihitaji.
◼ Ni muhimu kwa Sosaiti kuwa na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29-SW) na kuituma kwa Sosaiti haraka iwezekanavyo. Hiyo yatia ndani mabadiliko yoyote katika anwani ya eneo lao.
◼ Waandishi wa kutaniko wanapaswa kuweka fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205-SW) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b-SW). Zaweza kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Wekeni angalau akiba ya mwaka mmoja. Chunguzeni fomu zote za ombi la painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa kikamili. Ikiwa wenye kutoa maombi hawakumbuki vizuri tarehe ya ubatizo wao, wanapaswa kukadiria tarehe na kuiandika mahali.
◼ Iwapo wakati wowote utapanga kusafiri kwenda nchi nyingine, na utake kufahamishwa tarehe, nyakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kusanyiko la mzunguko au la wilaya, uliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Utapata orodha ya anwani za ofisi za tawi katika ukurasa wa mwisho wa Yearbook ya karibuni.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Watch Tower Publications Index 2001—Kiingereza
Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu —Kijaluo
◼ Video Mpya Zinazopatikana:
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi—Sehemu ya 7—Lugha ya Ishara ya Marekani
Respect Jehovah’s Authority—On Videocassette—Lugha Ishara ya Marekani
Warning Examples for Our Day—On Videocassette—Kiingereza