Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 7
  • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Tumia Magazeti Vizuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 7

Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

Kwa kuwa sasa maandikisho ya posta ya magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanakomeshwa, jitihada zitatakikana ili kuhakikisha kwamba sisi na wale tunaohubiria hatukosi hata toleo moja la magazeti hayo.

Magazeti ya Kibinafsi: Andikisho lako linapoisha, ongeza agizo lako la sasa kwenye idara ya magazeti. Wazazi wanapaswa kuagiza magazeti ya kutosha ili kila mmoja katika familia awe na gazeti lake mwenyewe. Kuandika jina lako kwenye gazeti lako kutahakikisha kwamba huliachii mtu bila kukusudia katika utumishi wa shambani. Mara tu magazeti yanapofika, akina ndugu wanaoyashughulikia watahakikisha kwamba kila toleo la magazeti hayo lapatikana kwenye Jumba la Ufalme.

Watu Wanaopelekewa Magazeti kwa Ukawaida: Wahubiri wanapaswa kujitahidi kuwa na watu wanaowapelekea magazeti kwa ukawaida, wanaopenda kupokea kila toleo. Kuwapelekea watu hao magazeti kibinafsi kutatokeza fursa za kusitawisha kupendezwa walikoonyesha na kuanzisha mafunzo ya Biblia.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1998, ukurasa wa 12.

Walio na Mahitaji ya Pekee: Hali ya pekee ambayo itaruhusiwa kutuma andikisho kwa posta ni kama kuna mtu anayependezwa kikweli lakini anaishi katika eneo lisilogawiwa kutaniko lolote. Ikiwa mtu anayeishi katika eneo la kutaniko hawezi kufikiwa ili kupelekewa magazeti kwa ukawaida lakini angependa kupata magazeti, zungumza na Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Wakikubali, anaweza kufanyiwa andikisho. Fomu za kawaida za andikisho (M-1-SW na M-101-SW) zaweza kutumiwa kwa kusudi hilo.

Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kubariki jitihada zetu zote za kutangaza Ufalme kupitia magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki