Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Mei 13
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga maonyesho tofauti-tofauti ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15 na la Amkeni! la Aprili 22. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti za kujibu kizuia-mazungumzo “Nina shughuli.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 19-20.
Dak. 15: “Badilishano la Kitia-Moyo la Pekee.” Hotuba. Tia wote moyo watazamie kwa hamu kuhudhuria kusanyiko la wilaya. Wasihi wote wahudhurie vipindi vyote, kuanzia Ijumaa asubuhi hadi Jumapili alasiri.
Dak. 15: “Sikuzote Fuatieni Lililo Jema.”a Kazia umuhimu wa kutii mipango ya mahali pa kulala ambayo imewekwa kwa faida yetu. Kazia vikumbusho vilivyo katika fungu la 2. Eleza kwa nini kila mtu anapaswa kuwa na mwenendo mzuri.
Wimbo 115 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 20
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Sanduku la Swali.
Dak. 12: “Tosheleza Mahitaji Yako ya Kiroho.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Zungumzia kwa nini sote twapaswa kukazia fikira programu ya kusanyiko. Kazia uhitaji wa kutumia yale tunayojifunza badala ya kusikia tu. Tia moyo wote waandike mambo makuu. Omba wasikilizaji watoe maelezo machache kuhusu faida walizopata kutokana na programu ya mwaka jana.
Dak. 18: “Kuvaa na Kujipamba kwa Kiasi.”b Ishughulikiwe na mzee ambaye atasoma kila fungu baada ya kulizungumzia. Saidia wote wathamini umuhimu wa kuwa waangalifu kuhusu jinsi tunavyoonekana hadharani.
Wimbo 169 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 27
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Mei. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga mhubiri mwenye umri mkubwa aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na mhubiri mchanga aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Amkeni! la Mei 8. Baada ya kila onyesho, eleza jinsi andiko linavyoweza kutiwa ndani ya utoaji huo kwa urahisi.
Dak. 15: “Je, Kutaniko Lenu Lina Eneo Kubwa Mno?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. (Makutaniko yaliyo na maeneo machache yanaweza kuzungumzia makala “Tumia Wakati Wako kwa Matokeo,” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1999.) Eleza kutaniko lina eneo kubwa kadiri gani na lilihubiriwa hadi wapi mwaka uliopita. Eleza jinsi madokezo yaliyotolewa yanavyotumika kwenu. Zungumzia mipango inayofanywa ili kuhubiri eneo lisilohubiriwa mara nyingi hivi karibuni.
Dak. 18: “Je, Unatumia Broshua Anataka Kuanzisha Mafunzo?” (Watu wote wawe na nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 kwa ajili ya mazungumzo haya.) Anza kwa onyesho lililotayarishwa vizuri linaloonyesha jinsi ya kuanzisha funzo ukitumia kielelezo kilicho katika fungu la 3. Baada ya hapo, taja mambo makuu ya broshua, na ueleze jinsi ilivyotayarishwa vizuri kwa ajili ya kuanzisha mafunzo. Onyesha umuhimu wa kupitia madokezo ya utoaji mbalimbali yanayopatikana katika nyongeza ya Januari 2002. Uliza wasikilizaji wamefanikiwa kwa kutumia madokezo yapi. Malizia kwa kurudia onyesho lililotajwa juu.
Wimbo 93 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 3
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Panga wahubiri wasimulie shangwe walizopata kwa sababu ya kushiriki katika upania msaidizi au upainia wa kawaida mwezi wa Machi, Aprili, au Mei. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Jinsi Ambavyo Kitabu Kutoa Sababu Hutumia Tafsiri Nyingine za Biblia. Hotuba fupi ikifuatiwa na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Soma fungu la 2 kwenye ukurasa wa 8 wa kitabu Kutoa Sababu, na ueleze kwa nini na jinsi Biblia inavyopaswa kutumiwa zaidi katika huduma yetu. Taja orodha ya mafupisho ya tafsiri za Biblia kwenye ukurasa wa 6, na ueleze kwa nini tunatumia manukuu kutoka katika tafsiri nyingine. Zungumzia maonyo yanayotolewa kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1997, ukurasa wa 16, fungu la 2 na ukurasa wa 20, fungu la 15. Ukitumia vichwa “Mwandamano wa Kimitume,” “Mifano ya Kuabudu,” na “Utatu” katika kitabu Kutoa Sababu, waombe wasikilizaji waonyeshe jinsi ambavyo kulinganisha tafsiri mbalimbali kunavyoweza kusaidia kufundisha kweli.
Dak. 15: “Imani Yetu Hutuchochea Kufanya Kazi Njema.”c Mnapozungumzia fungu la 2, hoji kifupi Shahidi mwenye bidii. Omba mhubiri huyo aeleze jinsi ambavyo kuwahubiria wengine hudhihirisha na kuimarisha imani yake.
Wimbo 56 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.