Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/02 uku. 1
  • Je, “Wataka” Kusaidia Wengine?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, “Wataka” Kusaidia Wengine?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unaweza Kusaidia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Mwige Yesu kwa Kuwatumikia Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Familia, Sifuni Mungu Mkiwa Sehemu ya Kutaniko Lake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 6/02 uku. 1

Je, “Wataka” Kusaidia Wengine?

1 Yesu aliwajali watu sana. Wakati mkoma mmoja alipoomba msaada wake, Yesu alinyoosha mkono wake, akamshika na kusema: “Mimi nataka. Fanywa safi.” (Mr. 1:40-42) Twaweza kuigaje mtazamo wa Yesu wa kusaidia wengine?

2 Watu Wenye Kupendezwa: Kila mshiriki wa kutaniko ana sehemu katika kusaidia wapya wawe waabudu wa Yehova. Wapya wanapokuja kwenye mikutano, wasalimie na upate kufahamiana nao. Tafuta njia unazoweza kutumia kuwatia moyo. Wapongeze kwa maelezo wanayotoa. Wapongeze kwa jitihada zao za kutumia kanuni za Biblia maishani mwao. Wasaidie waone kwamba wanaweza kupata marafiki wa kweli kutanikoni.

3 Waamini Wenzetu: “Wale ambao katika imani ni jamaa zetu” ndio hasa wanaohitaji msaada wetu katika njia mbalimbali. (Gal. 6:10) Wengi hupambana na matatizo ya afya. Wanaweza kufaidika unapowatembelea ili uwatie moyo, na labda pia unapowasaidia kwa njia yenye kutumika. Huenda wengine wakawa wanakabiliana na magumu mengine katika maisha yao. Waonyeshe unawajali kwa kutumia wakati kuwasikiliza na kuwajenga. (1 The. 5:14) Pia wazee wanahitaji ushirikiano wetu wanapotimiza madaraka yao. (Ebr. 13:17) Kwa kuonyesha roho ya utayari na ya kusaidia, twaweza ‘kuwa msaada wenye kuwatia nguvu’ waamini wenzetu.—Kol. 4:11.

4 Washiriki wa Familia: Pia twapaswa kujitahidi kuiga hali ya Yesu ya kujali watu katika familia yetu wenyewe. Wazazi wanaoonyesha kujali sana ‘huendelea kuwalea watoto wao katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.’ (Efe. 6:4) Watoto wanaweza kufanya sehemu yao kwa kuwa tayari bila kuchelewa kwa ajili ya funzo la familia, mikutano ya kutaniko, au utumishi wa shambani. Watoto wenye umri mkubwa wanaweza kuonyesha huruma kama ya Yesu kwa kuwasaidia wazazi wao wakabiliane na magumu yanayosababishwa na uzee. Katika njia hizi na nyinginezo, sisi sote twaweza “kuzoea ujitoaji-kimungu kwa watu wa nyumbani [kwetu] wenyewe.”—1 Tim. 5:4.

5 Tukimwiga Yesu katika kusaidia wengine, huenda tukaweza kupunguza matatizo yao na kuwa na uhusiano mzuri pamoja na familia yetu na kutaniko letu. Jambo la maana zaidi, tutamletea Yehova heshima, “Baba ya rehema nyororo.”—2 Kor. 1:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki