Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/02 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 10
  • Juma Linaloanza Juni 17
  • Juma Linaloanza Juni 24
  • Juma Linaloanza Julai 1
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 6/02 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Juni 10

Wimbo 58

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Katika makutaniko ambayo watu wana video, tia moyo kila mmoja atazame video Our Whole Association of Brothers akijitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Juni 24. Katika makutaniko ambayo akina ndugu hawana video hiyo, katika juma hilo mtazungumzia habari iliyo katika kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli, sura ya 17, “Mwe na Upendo Mwingi kwa Mmoja na Mwenzake,” fungu la 1-5 na 14-17. Ukitumia madokezo katika ukurasa wa 6, toa maonyesho mawili, moja la jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Mei 15 na la pili la Amkeni! la Mei 22. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Sipendezwi na dini.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 16-17.

Dak. 10: Sanduku la Swali. Soma makala yote na maandiko yaliyotajwa hapo. Kisha toa maelezo ya ziada, ukizungumzia mambo mengine yaliyo katika Sanduku la Swali kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998.

Dak. 20: “Kupanda kwa Wingi Huleta Baraka Tele.”a Tia ndani maelezo yanayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 1992, ukurasa wa 15-16, fungu la 14-17.

Wimbo 220 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 17

Wimbo 136

Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 20: “Tuna Kifaa Kipya cha Kuanzisha Mafunzo!” Mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Panga wakaribishaji wagawanye trakti hiyo mpya Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? ikiwa yapatikana. Tia ndani maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri ya utoaji, ukitumia madokezo yaliyo katika sanduku “Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti.” Mhubiri mmoja anatoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 15, na mwingine gazeti la Amkeni! la Mei 22. Katika kila onyesho mhubiri amalizia kwa kumpa mwenye nyumba trakti ya Kujua Biblia—yule asiyekubali magazeti na pia yule anayeyakubali. Tia moyo kila mtu awape trakti hiyo mpya wote anaokutana nao katika huduma.

Dak. 18: “Ridhika na Yale Uliyo Nayo.”b Kazia shauri la Kimaandiko, ukisoma na kuzungumzia maandiko mengi yaliyotajwa hapo wakati ukiruhusu.

Wimbo 197 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 24

Wimbo 52

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Wenzi wa ndoa watoa onyesho wakihubiri pamoja katika utumishi wakionyesha jinsi ya kutumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 kutoa magazeti ya Juni 1 na Juni 8. Mke anatoa Mnara wa Mlinzi, na mume anatoa Amkeni!

Dak. 12: Simulia au uigize mambo yaliyoonwa kutoka kwa wahubiri wa kwenu (1) kuhubiria wafanyakazi au wanashule wenzako (2) kuhubiri katika vikao vingine tofauti na nyumba kwa nyumba au barabarani. Katika matayarisho kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo, tia moyo kila mtu atayarishe utoaji kwa kutumia broshua zitakazotolewa Julai na Agosti.—Ona Sanduku “Vichapo Vingine,” katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002.

Dak. 25: Katika makutaniko ambayo akina ndugu hawana video, zungumzieni habari inayopatikana katika kitabu Wenye Umoja Katika Ibada, sura ya 17, “Mwe na Upendo Mwingi kwa Mmoja na Mwenzake,” fungu la 1-5 na 14-17. Ulimwengu unapoendelea kugawanyika, kazia kwamba Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa upendo wao na kwamba hawaruhusu mambo yoyote yenye kugawanya kama vile ukabila, utaifa, na jamii au lugha ziwagawanye. Mahali ambapo akina ndugu wana video, fanyeni “Kwa Nini Twapenda Ushirika Mzima wa Ndugu Zetu.”Anzeni moja kwa moja mazungumzo ya video Whole Association, mkitumia maswali yaliyopo.

Wimbo 95 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 1

Wimbo 83

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Juni. Waulize wahubiri waseme ni broshua gani ambazo wanapanga kutumia ili kuzitoa mwezi wa Julai na ni utoaji gani watakaotumia.

Dak. 15: Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Eleza sehemu za broshua hii ambazo zaifanya iwe kifaa chenye nguvu cha kufundishia watoto na wengine wasiojua kusoma vizuri wajifunze kuhusu Yehova. Zungumzia mifano ya maelezo yake rahisi na yenye kueleweka. (Ona somo la 2, 8, na 12.) Onyesha jinsi picha zinavyoweza kutumiwa ili kufikia moyo wa mwanafunzi. Dokeza njia ambazo broshua hii yaweza kutumiwa kwa matokeo mazuri. Wazazi wanapaswa kujifunza broshua hiyo na watoto wao wachanga. Tia moyo kila mtu aitoe katika huduma anapoweza.

Dak. 15: “Je, ‘Wataka’ Kusaidia Wengine?”c Tia moyo kila mmoja katika kutaniko awe na roho ya kusaidia.

Wimbo 156 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki