Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
TAARIFA: Huduma Yetu ya Ufalme itakuwa na Mkutano wa Utumishi wa kila juma la miezi ya kusanyiko. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho yanayohitajiwa ili kuwaruhusu watu wahudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii.” Inapofaa tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalotangulia kusanyiko ili kurudia shauri linalofaa kwenu lililoonyeshwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi huu. Katika mwezi wa Oktoba, sehemu yote ya Mkutano wa Utumishi itatumiwa ili kupitia mambo makuu ya kusanyiko. Tukiwa kusanyikoni twaweza kuandika mambo yatakayotusaidia katika mazungumzo hayo kutia ndani orodha ya mambo hususa tunayotaka kutumia maishani mwetu na katika huduma ya shambani. Kisha twaweza kueleza jinsi ambavyo tumetumia madokezo hayo tangu tulipohudhuria kusanyiko. Tutajengana kwa kueleza jinsi ambavyo tumenufaika na mafundisho mazuri tuliyopokea.
Juma Linaloanza Julai 8
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho mawili ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15 na gazeti la Amkeni! la Juni 22. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kujibu kizuia-mazungumzo “Tayari sisi ni Wakristo huku.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 19.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee anayeonyesha jinsi habari hiyo inavyofaa hali ya kwenu.
Dak. 20: Kujitayarisha Kuhubiri Isivyo Rasmi. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu ukurasa wa 93-94 katika kitabu Huduma Yetu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa kwanza wa nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002, onyesha kifupi njia mbili au tatu za kumhubiria isivyo rasmi mgeni, jirani, mtu wa ukoo, au mtu unayemfahamu.
Wimbo 139 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Sababu Nzuri za Kutumia Biblia Katika Huduma Yetu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Yesu alijua Maandiko na kuyarejezea mara nyingi alipofundisha. (Luka 24:27, 44-47) Aliyofundisha hayakuwa yake mwenyewe. (Yn. 7:16-18) Ni muhimu sisi pia tutumie Neno la Mungu. Lina nguvu inayozidi chochote ambacho huenda tukasema. (Yn. 12:49, 50; Ebr. 4:12) Watu wanyofu huvutiwa na faraja na tumaini kutoka kwa Maandiko. Uwe na mradi wa kusoma angalau andiko moja unapohubiri. Eleza kwamba maandiko yametiwa ndani ya utoaji wa magazeti uliopendekezwa kwa mwezi huu. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi ambavyo kutumia Biblia katika huduma kumewasaidia na pia kusaidia wale waliohubiria.
Wimbo 215 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Mzazi na mtoto wanaohubiri pamoja waonyesha jinsi ya kutumia madokezo ya kutoa magazeti ya Julai 1 na Julai 8 yaliyo kwenye ukurasa wa 4. Mmoja anatoa Mnara wa Mlinzi, na mwingine Amkeni! Tia moyo wazazi wazoeze watoto wao hatua kwa hatua katika huduma.
Dak. 17: Utamwambia Nini Mtu Anayekuuliza Juu ya Uislamu? Hotuba na maonyesho. Ukitumia kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura ya 12, eleza kifupi ulinganifu uliopo kati ya Biblia na Kurani. (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 285.) Onyesha tofauti iliyopo kati ya fundisho la Kiislamu kuhusu nafsi (ukurasa wa 297-300) na maelezo ya Biblia. (Ona kielezi-chini kwenye ukurasa wa 299.) Ukitumia kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 232-236, onyesha jinsi ya kumweleza mtu anayependezwa yale ambayo Biblia husema kuhusu nafsi.
Dak. 18: Naweza Kuepukaje Hatari Kwenye Internet? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea gazeti la Amkeni! la Januari 22, 2000, ukurasa wa 19-21. Eleza mitego ya matumizi yasiyo na mpaka ya Internet, na ueleze jinsi ya kuepuka kunaswa. Omba wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamenufaika kwa kutumia shauri hili. Mahali ambapo watu hawatumii Internet, zungumzieni “Je, Wafuatia Wema wa Adili?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1997, ukurasa wa 14-19, ukikazia zaidi kichwa kidogo “Wema wa Adili na Ushirika.”
Wimbo 61 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Julai.
Dak. 10: “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Hotuba. Tangaza tarehe ya kusanyiko la mzunguko litakalofuata. Wasihi wote wahudhurie na kusikiliza kwa makini programu hiyo. Watie moyo wahubiri wasiobatizwa wazingatie kufanya maendeleo ili wastahili kubatizwa. Jitahidi sana kuwaalika wanafunzi wa Biblia.
Dak. 25: “Unganishweni Pamoja kwa Upatano.”a Mnapozungumzia fungu la 3, tia ndani maelezo kutoka kwenye gazeti la Amkeni! la Aprili 22, 2000, ukurasa wa 9-10. Mkifikia fungu la 4, tia ndani maelezo kutoka kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1995, ukurasa wa 16-17, fungu la 4-6.
Wimbo 81 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: “Jinsi Michango Yetu Inavyotumiwa.”b Kazia kwamba watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu ndio wanaopaswa kuwa wa kwanza kugharimia kazi ya ulimwenguni pote. Taja kiasi ambacho kutaniko limechanga kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote kwa miezi mitatu iliyopita na kama kuna uhitaji wa kufanyia maendeleo jambo hilo. Shukuru kutaniko kwa michango yao kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote.
Dak. 15: Mambo yaliyoonwa ya kwenu. Alika wasikilizaji wasimulie mambo kadhaa yaliyoonwa yenye kujenga yanayohusiana na kuhudhuria kusanyiko la wilaya, kufanya upainia-msaidizi, au kushiriki katika utendaji mwingine wa kiroho.
Wimbo 184 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.