Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jul. 15
“Je, unafikiri waovu wanaadhibiwa motoni? [Ngojea jibu.] Biblia yaonyesha wazi adhabu ya kifo. [Soma Waroma 6:23a.] Basi, je, kuna mahali penye moto wa mateso? Je, hukumu itakayotekelezwa dhidi ya waovu ni kutengwa na Mungu? Gazeti hili lina majibu ya Kimaandiko ya maswali haya.”
Amkeni! Jul. 22
“Watu wengi huona kucheza kamari kuwa tafrija isiyo na ubaya wowote. Wengine huhisi kwamba inadhuru familia na jamii kwa ujumla.Toleo hili la Amkeni! lachunguza mchezo wa kamari kulingana na uchunguzi uliofanywa hivi majuzi. Labda wewe pia utapendezwa kusoma jinsi ambavyo kanuni za Biblia zinavyohusiana na habari hii.” Kwa mfano, ebu soma 1 Timotheo 6:10.
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Watu wengi hufikiri kwamba matendo na desturi za kishirikina hazidhuru. [Mwonyeshe jambo moja au mawili kutoka kwenye sanduku lililo katika ukurasa wa 5.] Je, umepata kufikiria mawazo hayo yametoka wapi? [Baada ya jibu lake, soma 2 Wakorintho 11:14.] Gazeti hili laeleza maoni ya Biblia kuhusu ushirikina.”
Amkeni! Ago. 8
“Watu wengi wanahangaika sana juu ya jeuri na ugaidi unaoongezeka. Labda utakubaliana na maneno ya Mhubiri 8:9. [Soma na ungoje jibu.] Toleo hili la Amkeni! lazungumzia yale tunayoweza kujifunza kutokana na yaliyopita na linaonyesha jinsi hali hiyo itakavyokwisha hivi karibuni.”