Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 15
“Kwa maelfu ya miaka, wanadamu wametunga mafundisho mengi mbalimbali. Je, unafikiri kwamba tunaweza kutofautisha mafundisho ya kweli na ya uwongo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha mahali ambapo unaweza kupata mafundisho ya kweli ambayo yanampendeza Mungu.” Soma 2 Timotheo 3:16.
Amkeni! Julai 22
“Inahuzunisha sana kuona mateso yanayosababishwa na misiba ya asili. [Taja msiba fulani unaojulikana kwenu.] Je, unafikiri kwamba misiba kama hiyo inaongezeka? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linajibu swali hilo. Pia linawafariji wale ambao wamefiwa na wapendwa wao katika misiba kama hiyo.” Soma Yohana 5:28, 29.
MNARA WA MLINZI Ago. 1
“Watu wengi leo wanahisi kwamba hawafai. Unafikiri wanaweza kusaidiwaje? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Biblia inavyoweza kuwasaidia watu hao wapate shangwe ya kweli.” Kazia maandiko yaliyoandikwa kwa herufi nzito za mlazo katika makala “Biblia Inaweza Kukusaidia Upate Shangwe.”
Amkeni! Ago. 8
“Watu wengi huishi kwa woga daima. Unafikiri ni nini kinachosababisha hali hiyo ya woga? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili lina mapendekezo mazuri ya kutusaidia kujilinda tusipatwe na hatari zinazowapata watu wengi. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia ya kuwapo kwa ulimwengu ambamo watu wataishi bila woga.” Soma Isaya 11:9.