Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jul. 15
“Wengi wameona kwamba watu wengi zaidi hupenda kujitenga na wengine. Unafikiri inafaa kufanya hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ona maneno haya yenye hekima kuhusu umuhimu wa kushirikiana na watu. [Soma Mhubiri 4:9, 10.] Gazeti hili linaonyesha ni kwa nini sisi sote tunawahitaji wengine na jinsi ambavyo tatizo la kujitenga na wengine linaweza kutatuliwa.”
Amkeni! Jul. 22
“Watu wengi wana wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa ponografia. Je, unafikiri tunapaswa kuhangaikia jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Shauri zuri linalopatikana katika Biblia linaweza kutulinda. [Soma Waefeso 5:3, 4.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kujilinda kutokana na hatari hiyo isiyoonekana.”
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Je, unajua kwamba kulingana na ripoti moja, zaidi ya nusu ya wakazi wa ulimwengu hujiruzuku kwa chini ya dola 2 kwa siku? Unafikiri kwamba kuna kitu kinachoweza kufanywa ili kutatua tatizo hilo? [Mruhusu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi laonyesha utatuzi wa kudumu wa umaskini unaotajwa katika Biblia.”—Soma Zab. 72:12, 13, 16.
Amkeni! Ago. 8
“Katika miaka ya karibuni, misiba inayosababishwa na hali ya hewa imeleta madhara makubwa ulimwenguni. Unafikiri ni nini kinachoweza kufanywa ili kuondoa kuteseka ambako husababishwa nayo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili lachunguza tatizo la hali ya hewa inayobadilika pamoja na utatuzi unaotajwa katika Biblia.”—Soma Isaya 35:1.