Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/02 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 9
  • Juma Linaloanza Desemba 16
  • Juma Linaloanza Desemba 23
  • Juma Linaloanza Desemba 30
  • Juma Linaloanza Januari 6
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 12/02 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 9

Wimbo 193

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 15 na Amkeni! la Novemba 22.

Dak. 15: “Tangaza Ujumbe wa Ufalme.”a Mnapozungumzia fungu la 3, tia ndani madokezo ya jinsi ya kusoma Biblia moja kwa moja unapohubiri habari njema.—km 12/01 uku. 1 fu. 3.

Dak. 18: Zaa Matunda Katika Kila Kazi Njema. Hotuba, wasikilizaji wakishiriki. Itolewe na mzee. Zungumzia historia na maendeleo ya kutaniko lenu, kutia ndani jitihada zilizofanya kutaniko likaanzishwa. Panga mapema ili wengine waliokuwapo wakati huo wasimulie mambo yaliyoonwa. Chunguzeni matarajio ya ongezeko zaidi, na utie moyo wote waunge mkono utendaji wa kutaniko kwa bidii.

Wimbo 119 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 16

Wimbo 29

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Eleza mipango hususa ya shambani ya Desemba 25 na Januari 1.

Dak. 15: Wale Wenye Ufahamu Wenye Kina Wataelewa. (Dan. 12:3, 10) Onyesho. Mtu mwenye kupendezwa auliza hivi: “Nawezaje kuwa na uhakika kwamba mnaelewa sawasawa yale ambayo Biblia hufundisha?” Mhubiri aeleza jinsi ya kutafuta habari fulani kulingana na somo linalohusika unapofanya utafiti wa Biblia. (w96 5/15 uku. 19-20) Akitumia mfano mmoja au miwili kutoka katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 78-83, aonyesha jinsi tulivyopata kuelewa kusudi la Mungu la kuumba dunia hii kwa kuchunguza kwa uangalifu Maandiko. Mhubiri anaeleza jinsi ambavyo njia hiyohiyo yaweza kutumiwa ili kusahihisha mafundisho mengine ya Biblia, kisha anajitolea kujifunza naye Biblia.

Dak. 20: “Wakumbuke Waaminifu Wenye Umri Mkubwa Zaidi.”b Tia ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1994, ukurasa wa 29. Taja mpango wa wahubiri walio dhaifu kimwili kuripoti saa za utumishi kuanzia dakika 15, 30, 45, n.k. Panga watu wachache wasimulie mambo yaliyoonwa kuonyesha jinsi ambavyo kushirikiana na watu hao huleta baraka kwa wote.

Wimbo 154 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 23

Wimbo 148

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, toa onyesho la jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na Amkeni! la Desemba 8. Watie moyo wale walio na video No Blood—Medicine Meets the Challenge waitazame wanapojitayarisha kwa mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Januari 6. Mahali ambapo watu hawana video hizo mtie moyo kila mtu asome habari iliyo kwenye ukurasa wa 5 na 13 wa broshua Damu Inaweza Kuokoaje Uhai Wako?

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Je, Wewe Hutoa Ripoti Sahihi?”c Mnapozungumzia fungu la 2, tia ndani maelezo kutoka katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 106-108.

Wimbo 165 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 30

Wimbo 152

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Desemba. Kama kutaniko lenu litabadili saa za mikutano mwaka ujao, wahimize wote kwa fadhili wahudhurie kwa ukawaida wakati wa hizo saa mpya. Taja toleo la vichapo la Januari, ukikazia vitabu ambavyo kutaniko linavyo akibani.

Dak. 15: Sanduku la Swali na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 20: “Makusanyiko ya 2003 ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova ya ‘Mtukuzeni Mungu.’”d Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko, akikazia fungu la 3-9. Mnapofikia fungu la 7, kazia daraka la mwandishi akiwa mratibu wa kusanyiko kwa niaba ya kutaniko. Pongeza wote kwa uchangamfu kwa kufanya mipango yao ya kusanyiko bila kukawia.

Wimbo 147 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 6

Wimbo 67

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 23: Msaada wa Kutii Sheria ya Mungu Kuhusu Damu. Hotuba itolewe na mzee mwenye sifa ya ustahili, ikitegemea muhtasari kutoka katika ofisi ya tawi. Mwandishi apaswa kuwa na idadi ya kutosha ya kadi zifuatazo: Kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na Kadi ya Utambulisho. Wahubiri waliobatizwa watapewa kadi hizo baada ya mkutano wa leo, lakini HAZIPASI kujazwa leo. Kutia sahihi, kushuhudia, na kuandika tarehe katika kadi zote kutafanywa baada ya Funzo la Kitabu la Kutaniko litakalofuata, na mwangalizi wa funzo la kitabu anaweza kusaidia ikiwa lazima. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi wanapaswa kumwona mwenye kadi akitia sahihi kadi hiyo. Wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe na wa watoto wao kwa kugeuza maneno yaliyo katika kadi hii yafae hali zao na masadikisho yao wenyewe.

Dak. 17: Mzee mwenye sifa za ustahili anazungumza pamoja na wasikilizaji habari iliyo kwenye ukurasa wa 5 na 13 wa broshua Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako. Kazia msimamo wetu wa kimaandiko kuhusu kutiwa damu mishipani na utaje kwamba kuna vitu vinavyoweza kutumiwa badala ya damu. Mahali ambapo watu wana video tumia sehemu yenye kichwa “Kwa Kweli Ingefaa Uitazame Video No Blood—Medicine Meets the Challenge.” Zungumzieni moja kwa moja video No Blood, mkitumia maswali yaliyo katika sanduku la ukurasa wa 7. Baadaye, soma fungu la mwisho katika sanduku hilo.

Wimbo 79 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki