Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Januari 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho mawili tofauti ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15 na Amkeni! la Desemba 22. Toa magazeti mawili-mawili katika kila onyesho, ijapokuwa ni gazeti moja tu litakalokaziwa.
Dak. 15: Wavutwa Bila Neno. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Mwenendo mzuri wa Kikristo ni ushahidi mkubwa. Umechochea wenzi wa ndoa wengine wasioamini kuwa waabudu wa Yehova. (1 Pet. 3:1, 2) Eleza mambo yaliyoonwa yanayopatikana katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1999, ukurasa wa 4; Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1995, ukurasa wa 10-11; na 1995 Yearbook, ukurasa wa 46. Panga mapema ili wahubiri wawili au watatu watoe maelezo kuhusu matokeo mazuri waliyopata kwa sababu ya kufuata shauri hilo la Biblia.
Dak. 20: “Kuishi Kupatana na Wakfu Wetu.”a Baada ya kuzungumzia fungu la 3, mhoji kifupi kijana ambaye amebatizwa. Amekabiliana na vishawishi gani tangu abatizwe? Ni nini kilichomsaidia ashinde magumu hayo? Amenufaikaje kwa kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova?
Wimbo 22 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 20
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Je, Unayachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Watie moyo wote watumie kwa faida yao kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2003. Zungumzia maelezo yaliyo kwenye dibaji, ukurasa wa 3-4. Ikiwa bado hamjapokea kijitabu hicho, tumia dibaji katika kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2002. Toa madokezo ya jinsi ambavyo familia zaweza kuzungumzia andiko pamoja. Ili uonyeshe manufaa za kuchunguza andiko kila siku, zungumzia andiko moja au mawili na maelezo ya mwezi ujao. Tia ndani onyesho fupi la mume na mke wakichunguza andiko na maelezo ya leo pamoja.
Dak. 22: “Wafundishe Wengine Lugha Safi.”b Baada ya kuzungumzia fungu la 6, panga mhubiri anayefaa zaidi sehemu hiyo atoe onyesho la jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia akiwa amesimama mlangoni pa mwenye nyumba anapofanya ziara ya kurudia, akitumia mojawapo ya madokezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002, ukurasa wa 4. Mhubiri na asome fungu moja katika broshua Anataka, kisha amalizie kwa kuuliza swali la fungu linalofuata na apange kulijibu katika ziara itakayofuata. Watie moyo wote waangalie kama mtu yeyote waliyemhubiria huenda akataka kujifunza Biblia kwa njia hiyo.
Wimbo 68 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho mawili tofauti ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari 8. Katika kila onyesho mhubiri amalizie kwa kumpa mwenye nyumba trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?—ampe mwenye nyumba anayekataa magazeti na yule anayeyakubali. Eleza kifupi jinsi ya kuwarudia watu tunaowaachia magazeti na trakti.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni, 2002, uku. 4, fu. 10.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Wasaidie Wengine Wamkaribie Yehova. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tutatoa kitabu kipya, Mkaribie Yehova mwezi wa Februari. Zungumzia taarifa kwa wasomaji iliyo kwenye ukurasa wa 3, na ukazie baadhi ya sehemu za kitabu hicho. Kila moja ya sehemu hizo nne yakazia mojawapo ya sifa kuu za Yehova. Kuna sura inayozungumzia jinsi Yesu alivyoonyesha sifa hiyo na sura inayozungumzia jinsi tunavyoweza kuonyesha sifa hiyo. Kuna picha 17 zinazoonyesha nyakati za Biblia. “Maswali ya Kutafakari” yanatusaidia kuchunguza sehemu nyingine muhimu za somo hilo. Zungumzieni sanduku “Madokezo ya Kutoa Kitabu Mkaribie Yehova,” na upange mhubiri anayefaa zaidi sehemu hiyo atoe onyesho moja.
Wimbo 124 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 3
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Zungumzia Sanduku la Swali. Watie moyo wahubiri watumie fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) wanapokuta watu ambao wanaongea lugha nyingine, kama ilivyoelezwa katika barua kwa makutaniko yote ya Oktoba 15, 1998. Kwa kawaida, fomu hiyo yapaswa kutumiwa kwa kusudi hilo hata kama mtu huyo hapendezwi na ujumbe wa Ufalme.
Dak. 12: Igeni Imani Yao. Mhoji mzee ambaye amemtumikia Yehova kwa unyenyekevu na uaminifu kwa miaka mingi. (Ebr. 13:7) Alijifunzaje kweli? Ni vizuizi gani alivyohitaji kuvishinda ili awe mwaminifu? Ni maandalizi au mambo gani ya kiroho yenye kutia moyo yaliyomsaidia afanye maendeleo? Alifanya nini ili afikie pendeleo hilo katika kutaniko? (1 Tim. 3:1) Ni nini ambacho kimemsaidia aweze kutimiza madaraka yake katika kutaniko, kazini, na katika familia? (1 Tim. 5:8) Analionaje pendeleo la kusaidia wengine kutanikoni?
Dak. 18: “Kazi Inayotaka Tuwe Wanyenyekevu.”c Mnapozungumzia fungu la 3, waombe wasikilizaji watoe madokezo ya jinsi ya kumjibu mtu anayejaribu kutudhihaki au mjeuri, mwenye mabishano au mwenye hasira. Mnapozungumzia fungu la 4, tia ndani maelezo kutoka katika kitabu Insight, Buku la 1, ukurasa wa 1160, fungu la 3, ikiwa buku hilo lapatikana kwenu.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.