Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/03 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Machi 10
  • Juma Linaloanza Machi 17
  • Juma Linaloanza Machi 24
  • Juma Linaloanza Machi 31
  • Juma Linaloanza Aprili 7
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 3/03 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Machi 10

Wimbo 5

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Februari 15 na Amkeni! la Februari 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatatolewa, ijapokuwa ni moja tu litakalozungumziwa.

Dak. 15: “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Taja mambo makuu ya ripoti ya ulimwenguni pote kutoka gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2003.

Dak. 20: “Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!”a (Mafungu 1-11) Baada ya kuzungumzia fungu la 6, mhubiri atoe onyesho fupi la jinsi ya kumwalika mtu wa ukoo, jirani, mwanashule, au mfanyakazi mwenzake kwenye Ukumbusho akitumia vikaratasi vya mwaliko. Ikiwa wahubiri hawajapokea vikaratasi vya kualika watu kwenye Ukumbusho, mipango inapaswa kufanywa ili wavipokee baada ya mkutano.

Wimbo 19 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 17

Wimbo 34

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Chagua Marafiki Wako kwa Hekima. Hotuba itolewe na mzee ikitegemea gazeti la Amkeni! la Februari 22, 1997 ukurasa wa 13, na habari iliyo chini ya kichwa “Mashirika Mabaya” kwenye ukurasa wa 120 katika kitabu Kutoa Sababu. Onyesha jinsi kanuni hizo zinavyowahusu vijana na watu wazima pia. Kazia faida za kuchagua marafiki wanaompenda Yehova na wanaojitahidi kufuata viwango vyake.

Dak. 20: “Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!”b (Mafungu 12-25) Ishughulikiwe na mwangalizi msimamizi. Anapozungumzia fungu la 13, kuwe na onyesho fupi la mzee akimtembelea ndugu mgonjwa ili kumtia moyo na kumweleza kwa fadhili jinsi anavyoweza kuongeza utendaji wake katika majira ya Ukumbusho.

Wimbo 53 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 24

Wimbo 72

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Machi 1, na Amkeni! la Machi 8.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Mashahidi wa Yehova Hunufaisha Jamii. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Nyakati nyingine sisi hupata fursa ya kueleza watu jinsi huduma yetu na mwenendo wetu hunufaisha jamii. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu mambo yafuatayo: (1) Sisi huwafundisha watu kufuata viwango vya Biblia kuhusu maadili. (2) Sisi huwafundisha watu kuwa wanyofu na kuwaheshimu wenye mamlaka. (3) Sisi huwafundisha watu wa rangi, mataifa, na matabaka mbalimbali jinsi ya kuishi kwa umoja. (4) Sisi huwasaidia wengine kuboresha maisha yao ya familia kwa kuwatia moyo wafuate kanuni za Biblia. (5) Tumewafundisha wengi kujua kusoma na kuandika. (6) Sisi hujitahidi kuwasaidia wengine nyakati za misiba. (7) Tumefanya mengi ili kupata uhuru wa kidini ambao umewafaidi watu wote.—Ona kitabu Wapiga-Mbiu, ukurasa wa 699.

Wimbo 121 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 31

Wimbo 130

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za mwezi wa Machi. Taja toleo la Aprili. Zungumzia mambo makuu katika sanduku, “Vikumbusho vya Ukumbusho.”

Dak. 13: Mambo Yaliyoonwa. Waombe wasikilizaji wasimulie mambo waliyoona wakati wa mwezi wenye utendaji mwingi wa Machi. Wapongeze wote kwa jitihada zao na uwatie moyo wote washiriki kadiri wawezavyo katika kazi ya kuhubiri mwezi wa Aprili.

Dak. 20: “Yehova Ndiye wa Kusifiwa Sana.”c Kazia umuhimu wa Ukumbusho. Eleza jinsi ambavyo wote wanaweza kuwasaidia wengine wahudhurie. Eleza mipango inayoweza kufanywa ili kuwatembelea wasiotenda na kuwasaidia wawe watendaji tena. Waombe wasikilizaji waeleze mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo kuhusiana na Ukumbusho wa mwaka jana.

Wimbo 173 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 7

Wimbo 191

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Jinsi ya Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tunawezaje kusitawisha ustadi wa kutoa sababu shambani kwa njia yenye matokeo? (1) Pata ujuzi kamili wa Maandiko kupitia funzo la kibinafsi la kawaida na kuhudhuria mikutano. (2) Tafakari yale ambayo umejifunza, na ufikirie jinsi unavyoweza kutumia kweli hizo katika hali mbalimbali. (3) Unapofikiria jinsi utakavyoeleza maandiko, tafuta sababu za Kimaandiko zinazounga mkono maelezo yako. (4) Fikiria jinsi unavyoweza kueleza maandiko kwa watu mbalimbali. (5) Fikiria mfano unaoweza kutumia kueleza hoja fulani.

Dak. 20: “Jinsi Kweli Inavyotuweka Huru.”d Tia ndani maelezo yaliyo katika sanduku kwenye ukurasa wa 6 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1998. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo kweli zilizo katika Neno la Mungu zimewaweka huru.

Wimbo 217 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki