Vikumbusho vya Ukumbusho
Mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu utafanywa Jumatano, Aprili 16. Wazee wanapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:
◼ Mnapopanga saa za mkutano, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa mpaka baada ya jua kushuka.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, apaswa kujulishwa saa kamili na mahali hususa pa sherehe.
◼ Matayarisho ya mkate na divai inayofaa yapaswa kufanywa mapema.—Ona Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 1985 ukurasa wa 17 au Februari 15, 1985, ukurasa wa 19 (Kiingereza).
◼ Sahani, bilauri, meza, na kitambaa cha meza kifaacho vyapasa kuletwa kwenye jumba na kuwekwa mahali pake mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkutano huo papasa kusafishwa kabisa mapema.
◼ Wakaribishaji na watakaopitisha mifano wapasa kuteuliwa na kuelezwa mapema kuhusu wajibu wao, utaratibu utakaofuatwa, na uhitaji wa kuvalia kwa njia ya heshima.
◼ Mipango yapasa kufanywa ili kuwatumikia watiwa-mafuta wowote ambao ni wagonjwa na hawawezi kufika.
◼ Makutaniko zaidi ya moja yanapopangiwa kutumia Jumba la Ufalme lilelile, kwapaswa kuwe na makubaliano mazuri miongoni mwa makutaniko hayo ili kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye jumba, milangoni, nje ya jumba, na kwenye maegesho ya magari. Ikiwezekana, ni vema kuwe na tofauti ya dakika 45 baina ya kila mwadhimisho.