Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Aprili 14
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6, panga kuwe na maonyesho mawili ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 15 na Amkeni! la Machi 22. Katika kila onyesho, magazeti mawili yatatolewa, ijapokuwa ni moja tu litakalozungumziwa.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.
Dak. 20: ‘Kung’aa Tukiwa Wamulikaji.’a Malizia kwa hotuba ya dakika tano inayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 1997, ukurasa wa 14-15, fungu la 8-13. Kazia ni kwa nini hatuufanyi ujumbe wa Ufalme kuwa siri.
Wimbo 134 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Zungumzieni kitabu Mwabudu Mungu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Eleza mpango wa kutumia kitabu hicho kipya kikiwa kitabu cha pili cha funzo. (km 6/00 uku. 4 fu. 5-6) Waombe wasikilizaji waeleze mambo wanayofurahia katika kitabu hicho. Kazia kwamba sehemu fulani za kitabu hicho zina maswali na maandiko yanayomsaidia mwanafunzi atafakari juu ya Neno la Mungu. Taja mfano ulio kwenye ukurasa wa 47-49, fungu la 13.
Dak. 20: “Ifanyie Nafasi.”b Mhoji mhubiri mmoja au wawili ambao wanatumia vizuri useja wao kuendeleza mambo ya Ufalme. Panga waeleze kinachowasaidia waridhike na utumishi wao.
Wimbo 35 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi za Aprili. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6, panga kuwe na maonyesho mawili ya kutoa Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, na Amkeni! la Aprili 8.
Dak. 15: “Tumia Kitabu Mwabudu Mungu Kuongoza Mafunzo ya Biblia.” Mwangalizi wa Utumishi azungumzia sehemu hiyo.
Dak. 20: “Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia.”c Ishughulikiwe na mzee akitumia maswali yaliyo kwenye makala hiyo. Waombe wasikilizaji wasimulie kwa ufupi mambo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani yanayothibitisha hoja hizo. Mnapozungumzia fungu la 5, igiza jambo moja lililoonwa katika eneo lenu kuonyesha funzo la Biblia lilivyoanzishwa.
Wimbo 89 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 5
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Zungumzia kwa ufupi madokezo yaliyo kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 2002, ukurasa wa 2, sehemu yenye kichwa “Kupanga Mapema Wakati wa Likizo.”
Dak. 15: “Wasaidie Wengine Wapate Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Kazia jinsi broshua hiyo inavyozungumzia imani zinazopendwa na watu wengi. Baada ya kuzungumzia fungu la nne, panga kuwe na onyesho lililotayarishwa vizuri kuhusu kujibu swali: “Je, Mungu Huzikubali Dini Zote?” (ol ukurasa wa 19-21) Watie moyo wote washiriki katika huduma mwisho wa juma hili.
Dak. 15: Ripoti Nzuri Huleta Shangwe. (Mit. 15:30) Mazungumzo na wasikilizaji yakionyesha mambo yaliyotimizwa na kutaniko kwa sababu ya jitihada ya pekee ya mwezi wa Machi na Aprili. Liombe kutaniko lisimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo kuhusiana na mambo yafuatayo: (1) kumsaidia mtu anayependezwa kuhudhuria Ukumbusho, (2) kufanya upainia msaidizi, (3) kumtia moyo mhubiri asiyetenda arudie utendaji wake kutanikoni, (4) kumsaidia mhubiri mpya aanze kuhubiri, na (5) kusitawisha upendezi wa wale waliohudhuria Ukumbusho. Panga maelezo hayo mapema. Wapongeze wote na uwatie moyo waendelee kujitahidi siku zijazo.
Wimbo 126 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.