Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/03 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 12
  • Juma Linaloanza Mei 19
  • Juma Linaloanza Mei 26
  • Juma Linaloanza Juni 2
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 5/03 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Mei 12

Wimbo 1

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15 na Amkeni! la Aprili 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja ndilo litakalozungumziwa. Usikose kutaja mpango wa kutoa mchango.

Dak. 20: Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Kufanya Maendeleo. Hotuba inayozungumzia mambo makuu kutoka kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 9-12 na 21-38. Tia moyo wazazi watumie habari hii katika funzo lao la familia, wakiwa na madhumuni ya kuzoeza watoto wao wafanye maendeleo katika huduma. Taja mambo hususa yanayoweza kutumiwa ili kusaidia vijana wasitawishe stadi zinazohitajiwa.

Dak. 15: “Tumekabidhiwa Habari Njema.”a Panga mapema ili mhubiri mmoja au wawili waeleze kifupi jinsi walivyoweza kufanya marekebisho ili waongeze utumishi wao.

Wimbo 46 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 19

Wimbo 62

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Zungumzia “Ujenzi wa Kimataifa wa Majumba ya Ufalme Katika Nchi Fulani za Ulaya.” Taja kwamba ujenzi wa Majumba ya Ufalme katika nchi zilizo na matatizo ya kiuchumi na katika eneo la ofisi ya tawi ya kwetu unategemezwa kwa michango ya Hazina ya Majumba ya Ufalme.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 15: “Msifu Yehova kwa Kutoa Ushahidi Kila Unapopata Nafasi.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Mnapozungumzia fungu la 3, uliza wasikilizaji wangesema nini ili kuanzisha mazungumzo ya Biblia katika hali zifuatazo: (1) wanaposimama kwenye foleni, (2) wanaposafiri kwa gari la umma, (3) kwa jirani anayefanya kazi uani mwake, (4) kwa mfanyakazi mwenzao kazini, (5) kwa mwanashule mwenzao. Panga mapema ili mhubiri aliyefanikiwa kutoa ushahidi nafasi ilipotokea asimulie jambo lililoonwa.

Wimbo 135 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 26

Wimbo 174

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Mei. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na Amkeni! la Mei 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja ndilo litakalozungumziwa. Mwishoni mwa onyesho moja, mwachie mwenye nyumba ambaye hakuchukua magazeti trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?

Dak. 10: “Kuthamini Vitabu Vyetu.” Hotuba.

Dak. 25: “Neno la Mungu Ni Kweli.”b Tumia maswali yaliyopo. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi walivyosaidiwa kujifunza kweli wahubiri walipotumia Biblia kujibu maswali yao. Mnapozungumzia fungu la 4, panga mhubiri atoe onyesho la jinsi ya kutumia Biblia kwenye ziara ya kwanza, akitumia baadhi ya madokezo yaliyo kwenye makala “Litumie Sawasawa Neno la Mungu.”—km 12/01 uku. 1 fu. 3-4.

Wimbo 188 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 2

Wimbo 210

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia dokezo moja au mawili kutoka katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 inayozungumzia jinsi ya kutoa broshua Anataka na kitabu Ujuzi.

Dak. 20: Ndoa Yenye Kuheshimika—Ni Takwa la Mungu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Katika nchi nyingi, ni jambo la kawaida kwa watu wawili kuishi pamoja bila kuoana kisheria. Wengine hudai kwamba jambo hilo lina manufaa kadhaa. Eleza maoni ya Biblia, ukikazia kwamba ndoa ilianzishwa na Mungu. (rs uku. 241-242) Kuishi pamoja bila kufunga ndoa kisheria ni kufanya uasherati. (fy uku. 17) Kinyume na yale ambayo wengi huamini, uchunguzi umeonyesha kwamba kuishi pamoja kabla ya kufunga ndoa hufanya ndoa nyingi zisifanikiwe. (g02 3/8 uku. 29; g92 9/8 uku. 28, Kiingereza; g91 5/8 uku. 28, Kiingereza) Wakristo humheshimu Yehova kwa kufuata sheria zake. Wao hujinufaisha pia wanapofanya hivyo.—Isa. 48:17, 18.

Dak. 15: Unafaidikaje? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa shule. Kuanzia Januari tulianza programu mpya ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Zungumzia kifupi mambo mapya ya shule. Taja faida ambazo watu wamepata kufikia sasa. Je, wengi zaidi wamejiandikisha kwenye shule? Je, watu wamekuwa na nia ya kushiriki zaidi? Wanafunzi wanafaidikaje na mpango mpya wa kupewa shauri? Waombe wasikilizaji wasimulie jinsi ambavyo wamefaidika kufikia sasa na jinsi wanavyofikiri programu hiyo itawasaidia siku zijazo.

Wimbo 225 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki