Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa na waliohudhuria Ukumbusho au mikutano mingine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani kwa ukawaida na kutaniko, jitahidi kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa ikiwa watu hao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Toa kitabu Ujuzi au broshua Anataka. Ikiwa wenye nyumba tayari wana vichapo hivyo, tumia broshua nyingine zinazofaa ambazo ziko kutanikoni. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai–Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Katika sehemu mbalimbali za ulimwengu, broshua zifuatazo zaweza kufaa: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Juni 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Wanafunzi wa darasa la 13 la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma nchini Kenya walihitimu Januari 19, 2003. Lilikuwa jambo lenye kutia moyo kusikia maelezo ya uthamini ya wanafunzi hao waliohudhuria darasa hilo kutoka Ethiopia, Kenya, Sudan, Tanzania, na Uganda. Ndugu waseja wenye umri wa kati ya miaka 23 hadi 50 ambao wangependa kuhudhuria shule hiyo wanaweza kupata habari zaidi kutoka katika mikutano inayofanywa na mwangalizi wa wilaya wakati wa kusanyiko la mzunguko. Lazima wawe wametumikia wakiwa watumishi wa huduma kwa angaa miaka miwili au wawe ni wazee wa kutaniko.