Kuthamini Vitabu Vyetu
1 “Hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi.” (Mhu. 12:12) Vitabu vingi havina faida yoyote. Hata hivyo, vitabu vinavyochapishwa na Mashahidi wa Yehova ni tofauti. Ni vyenye thamani sana kwa sababu vina chakula cha kiroho kinachookoa uhai. Huwasaidia watu wanaopendezwa kumjua Yehova, na huimarisha imani ya wale ambao tayari ni watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu.
2 Tunataka kuwapa wengine vitabu vyetu kwa sababu tunajua kwamba vinaweza kuwafaidi. Hata ingawa vitabu vyetu haviuzwi, pesa zinahitajiwa ili kuvichapisha na kuvisafirisha. Kwa hiyo, hatutaki kuwapa watu vitabu hivyo ovyoovyo. Ikiwa hatujui kama mwenye nyumba anapendezwa, kwa kawaida tunampa nakala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au labda trakti tu. Tunapaswa kumrudia kila mtu aliyechukua kichapo, na akipendezwa wakati huo, tunaweza kumpa kingine.
3 Wahubiri fulani huogopa kuwaambia wenye nyumba kwamba kazi yetu hugharimiwa kwa michango ya hiari, lakini mara nyingi inafaa tuwaambie jambo hilo. Hilo linawasaidia wenye nyumba waelewe wazi kwamba kazi yetu si ya kibiashara. Huonyesha wazi kwamba kusudi letu ni kuhubiri habari njema za Ufalme na kufanya wanafunzi. Hutusaidia kutambua watu wanaopendezwa kikweli. Mara nyingi watu huwa na pesa za kununua sigara na vitabu vya kilimwengu. Ikiwa wanapendezwa kikweli na habari ulizowajulisha, wataona inafaa kutoa michango ili kuendeleza Ukristo wa kweli. Tunapoeleza jinsi kazi yetu inavyogharimiwa, tunaonyesha kwamba tunathamini vitabu vyetu. Pia tunaonyesha kwamba tunatambua pesa zinahitajiwa ili kuvichapisha.
4 Mpango wa michango ukielezwa kwa njia inayofaa, watu wengi hufurahi kuchangia kazi yetu muhimu. Huenda nyakati nyingine ukahisi kwamba haifai kutaja michango, lakini kwa ujumla ni vyema kuitaja kwenye ziara ya kwanza tunapokutana na mwenye nyumba anayefurahia kusoma vitabu vyetu.