Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/03 uku. 6
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 6/03 uku. 6

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Juni 30, 2003. Mwangalizi wa shule atashughulikia pitio la dakika 30 linalotegemea habari iliyozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa juma la kuanzia Mei 5 hadi Juni 30, 2003. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejezo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

Sifa za Usemi

1. Kwa nini ubadilifu wa sauti ni muhimu unapotoa hotuba, na hilo linaweza kufanywaje? [be uku. 111 sanduku; uku. 112 sanduku]

2. Hata ingawa msemaji anaamini mambo anayosema na anampenda Yehova, kwa nini huenda akakosa shauku? [be uku. 115 fu. 3-4; uku. 116 fu. 1]

3. Ni nini kitakachomsaidia msemaji kutoa hotuba kwa hisia, na kwa nini hilo ni muhimu? [be uku. 119 fu. 1-4]

4. Shauku na hisia zinazofaa katika hotuba hutegemea nini? [be uku. 120 fu. 2-5]

5. Kweli au Si Kweli: Ishara za mwili na za uso ni muhimu maadamu tu wasikilizaji wanakuangalia. Eleza. [be uku. 121 fu. 3]

Hotuba Na. 1

6. Ni mambo gani yaliyomsaidia Yosia kuchagua mwenendo wa maisha unaofaa licha ya kuwa na maisha mabaya utotoni? (2 Nya. 34:1, 2) [w01 4/15 uku. 27 fu. 1-6; uku. 28 fu. 4]

7. Mithali 9:7, 8a inamaanisha nini, na inahusuje utumishi wa shambani? [w01 5/15 uku. 29 fu. 4-5]

8. Yehova alimaanisha nini alipowaambia Waisraeli, ‘Msisahau,’ na tunawezaje kuepuka kuwa wasahaulifu? (Kum. 4:9; 8:11) [be uku. 20 fu. 1-3]

9. Maneno ya kutoka moyoni aliyosema Daudi kwenye Zaburi 32:1, 5 na Zaburi 51:10, 15 yanaonyeshaje kwamba mtu hapaswi kujiona hafai baada ya kufanya dhambi nzito na kuonyesha toba ya kweli? [w01 6/1 uku. 30 fu. 1-3]

10. Maagizo ambayo Paulo alitoa kwenye 1 Timotheo 5:3-16 yanatufunza nini kuhusu kuwasaidia wenye uhitaji? [w01 6/15 uku. 10 fu. 3]

Usomaji wa Biblia wa Kila Juma

11. Yesu alimaanisha nini alipotumia usemi ‘kuzaliwa mara ya pili,’ kwenye Yohana 3:3? [w95 7/1 uku. 9-10 fu. 4-5]

12. Yesu alitumiaje elimu yake, na hilo latufunza somo gani muhimu? (Yoh. 7:15-18) [w96 2/1 uku. 9-10 fu. 4-7]

13. Kwa nini andiko la Yohana 7:53–8:11 halipatikani katika sehemu kuu ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya?

14. Yesu ‘alikujaje kwa namna ileile’ kama alivyoenda mbinguni? (Mdo. 1:11) [w90 6/1 uku. 11 fu. 5]

15. Kwa nini andiko la Matendo 5:13 linasema kwamba “hakuna hata mmoja kati ya wale wengine aliyekuwa na moyo wa kujiunga mwenyewe nao [wanafunzi]”?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki