Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
TAARIFA: Huduma Yetu ya Ufalme itakuwa na Mkutano wa Utumishi wa kila juma katika miezi ya kusanyiko la wilaya. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho yanayohitajiwa ili kuwaruhusu watu wahudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Mtukuzeni Mungu.” Inapofaa, tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalotangulia kusanyiko ili kurudia shauri linalofaa hali za kwenu lililoonyeshwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi huu. Katika mwezi wa Oktoba, Mkutano mmoja wa Utumishi utatumiwa kupitia mambo makuu ya kusanyiko. Tukiwa kusanyikoni tunaweza kuandika mambo yatakayotusaidia katika mazungumzo hayo kutia ndani orodha ya mambo hususa tunayotaka kutumia maishani mwetu na katika huduma ya shambani. Kisha twaweza kuwatia wengine moyo kwa kueleza jinsi ambavyo tumetumia madokezo hayo tangu tulipohudhuria kusanyiko.
Juma Linaloanza Juni 9
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 15 na Amkeni! la Mei 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Tumia andiko moja katika kila onyesho.
Dak. 15: “Kazi Yetu Kuu Ni Huduma ya Kikristo.”a Watie moyo vijana wafikirie baraka wanazoweza kufurahia kwa kufanya utumishi wa wakati wote. Tia ndani maelezo kuhusu habari yenye kichwa kidogo “Wakati Utamaduni na Dhamiri Zinapopingana,” katika Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2000, ukurasa wa 19-20.
Dak. 18: “Kukusanyika Ili Tumsifu Yehova.”b Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Wahimize wote wahudhurie kila kipindi, kuanzia Ijumaa asubuhi hadi Jumapili alasiri. Kazia uhitaji wa kutumia yale tunayojifunza badala ya kusikia tu. Eleza taarifa iliyo juu kuhusu mipango ya kupitia mambo makuu ya kusanyiko la wilaya kwenye Mkutano wa Utumishi mwezi wa Oktoba. Watie moyo wote waandike mambo makuu.
Wimbo 190 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 16
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 18: “Uwe Kielelezo Katika Kazi Zilizo Bora.”c Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Kazia uhitaji wa kufuata mipango ya mahali pa kulala ambayo imefanywa kwa faida yetu. Eleza kwa nini ni muhimu kila mtu awe na mwenendo mzuri.
Wimbo 131 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja, mhubiri atoa ushahidi barabarani.
Dak. 20: Tunaweza Kufanya Nini Tunapovunjika Moyo? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1999, ukurasa wa 28-29, pamoja na kichwa kidogo “Kudumisha Mtazamo Ufaao.” Pitia madokezo yanayofaa pamoja na shauri la Kimaandiko. Panga mapema mhubiri mmoja au wawili wenye matokeo waeleze kinachowasaidia kudumisha shangwe katika huduma yao.
Dak. 15: “Kuhubiri Katika Ulimwengu Unaozidi Kubadilika.”d Mnapozungumzia fungu la 2 na 3, waombe wasikilizaji waeleze matukio ya karibuni yanayoweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo katika eneo lenu. Mnapozungumzia fungu la 4, panga kuwe na onyesho fupi mkitumia mojawapo ya utoaji uliotajwa.
Wimbo 15 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Juni. Pitia toleo la vichapo la Julai na Agosti. Kazia broshua mbili mlizo nazo akibani. Panga maonyesho yaliyotayarishwa vizuri kuhusu kutoa broshua hizo katika huduma. Waweza kupata madokezo ya utoaji mbalimbali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1998, ukurasa 8. Utoaji zaidi waweza kupatikana katika Watch Tower Publications Index chini ya kichwa “Presentations” na kichwa kidogo “List by Publication.”
Dak. 15: “Kuwa Mwenye Matokeo Licha ya Ulemavu.”e Eleza pia jinsi wengine wanavyoweza kusaidia, kulingana na gazeti Amkeni! la Machi 8, 1991, ukurasa wa 23-24, au Amkeni! la Agosti 22, 1990, ukurasa wa 22-23 la Kiingereza, chini ya kichwa kidogo “Ni Nini Liwezalo Kufanywa?”
Dak. 20: Tumia Neno la Mungu kwa Matokeo Unapohubiri Juu ya Ufalme. Mazungumzo na wasikilizaji yashughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Sisi hujitahidi kushiriki na kila mtu tunayekutana naye katika huduma yetu habari ya Kimaandiko yenye kujenga kuhusu Ufalme. Hata hivyo, hatupaswi kusoma tu maandiko ya Biblia. Tunapaswa kuyafafanua, kutoa mfano, na kuonyesha jinsi yanavyotumika. Onyesha jinsi tunavyoweza kufanya hivyo, kwa kutumia baadhi ya maandiko yaliyo kwenye kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 282-283, chini ya kichwa kidogo “Watawala wa Kibinadamu Hawatoi Yale Ambayo Wanadamu Wanahitaji kwa Haraka.” Baada ya mazungumzo, panga mhubiri aliyejitayarisha vizuri aonyeshe jinsi ya kutumia andiko moja ifaavyo kwenye ziara ya kurudia, akitoa maelezo mafupi, mfano rahisi, na kumwonyesha kifupi mwenye nyumba jinsi utawala wa Ufalme utakavyomfaidi binafsi. Mhubiri aanza onyesho kwa kusoma andiko. Baada ya onyesho, zungumzia jinsi andiko lilivyofafanuliwa, mfano ulivyotolewa, na matumizi yalivyoonyeshwa. Watie wote moyo wasitawishe ustadi wa kutumia Neno la Mungu kwa matokeo.
Wimbo 171 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 7
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 17: “Mavazi Yenye Mpangilio Mzuri Humstahi Mungu.”f Ishughulikiwe na mzee. Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Mwombe ndugu ambaye ni msomaji mzuri asome kila fungu kwa sauti.
Dak. 23: “Kujulisha Jina la Mungu.”g Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Mnapozungumzia fungu la 4, tia ndani maelezo kutoka kwenye sanduku “Kujulisha Jina la Mungu,” kwenye ukurasa wa 124 katika kitabu Wapiga-Mbiu. Panga mhubiri stadi aonyeshe jinsi ya kufanya ziara ya kurudia. Ukitumia maandiko mawili au matatu kutoka kwenye kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 425-426, eleza kwa nini ni muhimu kujua na kutumia jina la Mungu.
Wimbo 197 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
d Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
e Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
f Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
g Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.