Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/03 uku. 1
  • Iga Wema wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Iga Wema wa Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • “Wema Wake, Jinsi Ulivyo Mwingi!”
    Mkaribie Yehova
  • Mweneo Mkubwa Ajabu wa Wema wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Wema—Unaweza Kuusitawishaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Wema Mwingi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 8/03 uku. 1

Iga Wema wa Yehova

1 Baada ya kufurahia machweo yenye kupendeza au mlo mtamu, je, hatuchochewi kumshukuru Yehova, aliye Chanzo cha wema wote? Wema wake hutuchochea tutake kumwiga. (Zab. 119:66, 68; Efe. 5:1) Tunawezaje kuonyesha sifa ya wema?

2 Kwa Wasioamini: Njia moja tunayoweza kuiga wema wa Yehova ni kwa kuwahangaikia kikweli wale ambao katika imani si jamaa zetu. (Gal. 6:10) Kuwaonyesha wema kwaweza kuwafanya wawe na maoni mazuri kuelekea Mashahidi wa Yehova na ujumbe wetu.

3 Kwa mfano, alipokuwa akisubiri katika hospitali, ndugu mmoja painia kijana aliketi karibu na mwanamke mmoja mzee aliyeonekana kuwa mgonjwa kuliko wengine waliokuwapo. Zamu ya ndugu huyo ya kumwona daktari ilipofika, alimruhusu mwanamke huyo aingie kwanza. Alikutana naye tena, sokoni, na mwanamke huyo akafurahi sana kumwona. Ingawa mwanzoni hakukubali habari njema, alisema sasa anajua kwamba Mashahidi wa Yehova wanawapenda kikweli jirani zao. Mwanamke huyo akaanza kujifunza Biblia kwa ukawaida.

4 Kwa Ndugu Zetu: Tunaiga pia wema wa Yehova tunapojitolea kuwasaidia waamini wenzetu. Nyakati za msiba, sisi huwa miongoni mwa watu wa kwanza kuja kuwasaidia ndugu zetu. Tunaonyesha roho hiyo hiyo tunapowasaidia wale wanaohitaji kusafirishwa kwenda mikutanoni, tunapowatembelea wagonjwa, na tunapoupanua upendo wetu kuelekea wale ambao hatuwajui vema kutanikoni.—2 Kor. 6:11-13; Ebr. 13:16.

5 Njia nyingine ambayo Yehova huonyesha wema ni kwa kuwa “tayari kusamehe.” (Zab. 86:5) Tunaweza kuonyesha kwamba tunapenda wema kwa kumwiga yeye katika kuwasamehe wengine. (Efe. 4:32) Hilo hufanya uhusiano wetu pamoja na waamini wenzetu uwe ‘mwema na wenye kupendeza.’—Zab. 133:1-3.

6 Wema mwingi wa Yehova na utufanye tumsifu na kushangilia. Na utuchochee tujitahidi kuiga wema wake katika mambo yote tunayofanya.—Zab. 145:7; Yer. 31:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki