Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/03 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 11
  • Juma Linaloanza Agosti 18
  • Juma Linaloanza Agosti 25
  • Juma Linaloanza Septemba 1
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 8/03 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Agosti 11

Wimbo 101

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 15 na Amkeni! la Julai 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika mojawapo la maonyesho hayo, onyesha jinsi ya kushughulikia kizuia mazungumzo, “Nina shughuli,” ambacho kinaweza kutokea.—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 19.

Dak. 15: “Iga Wema wa Yehova.”a Waombe wasikilizaji wasimulie mambo machache yaliyoonwa ambayo yanaonyesha jinsi ambavyo matendo ya fadhili yametokeza fursa za kutoa ushahidi. Pongeza kutaniko kwa jitihada za kuwasaidia waamini wenzao.

Dak. 20: “Baraka za Huduma ya Upainia.”b Tumia maswali yaliyopo. Omba painia mmoja au wawili waeleze baraka ambazo wamepokea kwa kufanya upainia. Taja kwamba mtu yeyote ambaye angependa kufanya upainia anaweza kupata fomu kutoka kwa mwandishi.

Wimbo 11 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 18

Wimbo 82

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya Hesabu. Zungumzia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee.” Tangaza tarehe ya kusanyiko la pekee linalofuata, na uwahimize wote wahudhurie. Ikiwa kusanyiko hilo litafanywa miezi michache ijayo, taja kwamba wale ambao wangependa kubatizwa wanapaswa kumjulisha mwangalizi msimamizi.

Dak. 15: “Kazi Ambayo Huburudisha.”c Panga mapema wahubiri wawili au watatu waeleze jinsi ambavyo huduma ya Kikristo huwaburudisha.

Dak. 18: “Tudumishe Mahali Petu pa Ibada Katika Hali Nzuri.”d (Fungu 1 hadi 5) Tumia maswali yaliyopo. Mnapozungumzia fungu la 3 na la 4, taja mipango ya kwenu ya usafi wa Jumba la Ufalme. Zungumzia mambo yoyote yanayohitaji kuzingatiwa. Pongeza kutaniko kwa jitihada zao za kudumisha mahali panapofaa pa ibada ya kweli.

Wimbo 114 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 25

Wimbo 175

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na Amkeni! la Agosti 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Kuwe na onyesho la mzazi na kijana mvulana au msichana wakijitayarisha kwa ajili ya kazi ya magazeti. Wanapitia kifupi kila dokezo kabla ya kufanya onyesho.

Dak. 15: “Kustaafu—Je, Ni Mlango Uongozao Kwenye Utendaji Zaidi?”e Ikiwezekana, mhoji kifupi mhubiri ambaye ametumia kustaafu kwake kutoka katika kazi ya kimwili kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova. Mwulize marekebisho ambayo amefanya na baraka ambazo amepata.

Dak. 20: Jipe Ujasiri wa Kuhubiri. (1 The. 2:2) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Eleza kwa nini wengi huogopa kuwahubiria wengine ujumbe wa Ufalme. Hata wale ambao wamekuwa watendaji kwa miaka mingi wanaweza kuogopa. Simulia baadhi ya mambo yaliyoonwa yanayopatikana katika Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 1999, ukurasa wa 25; Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 1999, ukurasa wa 25; na Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1996, ukurasa wa 31. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi walivyojipa ujasiri wa kuhubiri habari njema wakati ambapo walikuwa na woga. Malizia kwa kuwatia moyo wajipatie nguvu kutoka kwa Yehova, ukitumia Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 1999, ukurasa wa 23 hadi 24.

Wimbo 125 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 1

Wimbo 84

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Agosti. Taja toleo la vichapo la Septemba. Panga mapema mhubiri mmoja au wawili wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kujenga waliyopata katika mahubiri yasiyo rasmi wakati wa kusanyiko la wilaya, likizoni, au katika pindi nyingine miezi ya karibuni.

Dak. 15: Je, Wewe Hutimiza Ahadi Yako ya Kurudi? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 1999, ukurasa wa 10 hadi 11, chini ya kichwa “Njia Nyingine za Kutimiza Ahadi Zetu.” Tunapowakuta watu wanaopendezwa katika huduma yetu, kwa kawaida sisi hupanga kuendeleza mazungumzo hayo wakati mwingine. Je, sisi huwa waaminifu na kurudi kama tulivyoahidi? Changanua kanuni za Biblia zinazopaswa kutuchochea tutimize ahadi yetu. Waombe wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa yanayoonyesha jinsi walivyothawabishwa kwa kurudi upesi.

Dak. 20: “Tudumishe Mahali Petu pa Ibada Katika Hali Nzuri.”f (Fungu la 6 hadi 12) Tumia maswali yaliyopo. Kazia umuhimu wa kudumisha Jumba la Ufalme ifaavyo, ukikazia mambo yaliyo kwenye sanduku lililo katika ukurasa wa 4. Tia ndani ripoti fupi kuhusu hali ya Jumba lenu la Ufalme, na utaje mipango yoyote ya kufanya marekebisho au kuliboresha.

Wimbo 41 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

e Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

f Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki