Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai–Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” na Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Broshua zifuatazo zinaweza kutolewa mahali panapofaa: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ya Kiswahili yaweza pia kutolewa mwezi huo. Septemba: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, na Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Oktoba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, toa broshua Anataka na ujitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Toa kitabu Ujuzi au broshua Anataka. Ikiwa wenye nyumba tayari wana vichapo hivyo, watolee kitabu Mwabudu Mungu au kichapo cha zamani zaidi.
◼ Vichapo vinavyopatikana ambavyo vinaweza kuagizwa katika agizo linalofuata la kutaniko: Habari za Ufalme Na. 36, “Milenia Mpya—Unaweza Kutarajia Nini Wakati Ujao?”—Kiingereza; Habari za Ufalme Na. 34, “Kwa Nini Maisha Yamejaa Matatizo Sana?”—Kiingereza; 2000 Yearbook of Jehovah’s Witnesses, yenye historia ya Uingereza, Cheki, na Madagaska; Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo—Kiswahili.
◼ Kuanzia juma la Oktoba 20, 2003, tutajifunza kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli katika Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Mwangalizi-Msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Agosti 29 na 30, 2003, vichapo vyote vilivyoko Betheli vitahesabiwa. Kwa hiyo, hakuna maagizo yoyote ya vichapo ya kutaniko yatakayoshughulikiwa na kuchukuliwa siku hizo.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza Kalenda ya Mashahidi wa Yehova ya 2004, Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2004, na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2004 katika ombi lao la vichapo litakalofuata. Orodha ya lugha ambazo vichapo hivyo vinapatikana itakuwa katika “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” ambalo hutumwa kwa makutaniko yote kila mwezi.