Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/03 uku. 7
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Moyo Kamili Kumwelekea Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kuazimia Kumtumikia Yehova kwa Moyo Kamili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 8/03 uku. 7

Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee

Leo kuna habari nyingi kuhusu jinsi ya kuitunza afya ya moyo wetu halisi ili tuwe na maisha marefu yenye kufurahisha. Hali ya moyo wetu wa mfano ni muhimu hata zaidi. Basi, inafaa kama nini kwamba kichwa cha programu ya kusanyiko letu la pekee kuanzia Septemba 2003 ni: “Kumtumikia Yehova kwa Moyo Kamili.” (1 Nya. 28:9) Tunaweza kutazamia kujifunza nini?

Mwangalizi wa mzunguko atazungumzia kichwa “Kuwasaidia Wengine Wamtumikie Yehova kwa Nafsi Yenye Shangwe.” Mahojiano yatakazia shangwe inayotokana na kusitawisha upendezi na kuongoza mafunzo ya Biblia pamoja na watu wanaotaka kumtumikia Yehova. Bila shaka, wahudhuriaji wote watafarijiwa na kutiwa moyo na hotuba ya kwanza ya msemaji anayezuru, “Kulinda Mioyo Yetu Katika Ulimwengu Wenye Misukosuko.” Kipindi cha asubuhi kitamalizia kwa hotuba ya ubatizo.

Alasiri, sehemu “Kuwasaidia Wengine” itazungumzia jinsi tunavyoweza kuwasaidia wengine. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kuilinda mioyo ya watoto wao dhidi ya uvutano mbaya na kuwasaidia kumkaribia Yehova? Sehemu “Wasaidie Watoto Wako Waone Shangwe Katika Yehova” itatoa madokezo mazuri na itawaonyesha wazazi jinsi ya kufanya hivyo.

Je, tunatumia kwa faida yetu maandalizi yote ambayo Yehova anatoa ili kuidumisha mioyo yetu ya mfano ikiwa na afya na yenye nguvu? Hotuba ya mwisho ya msemaji anayezuru, “Dumisha Moyo Kamili Katika Kumtumikia Yehova,” itakazia mambo manne muhimu yanayoweza kutusaidia kuwa na afya nzuri ya kiroho. Tunatumia muda na jitihada kadiri gani katika kusali kwa bidii, kujifunza Neno la Mungu, kuhubiri kwa bidii, na kushirikiana na Wakristo wengine? Je, tunaweza kuboresha yoyote kati ya mambo hayo?

Yehova hutusihi hivi: “Elekeza moyo wako kwenye nidhamu na sikio lako kwenye maneno ya ujuzi.” (Mit. 23:12) Panga sasa kuhudhuria siku hiyo yenye kunufaisha ya maagizo ya Kimaandiko. Kufanya hivyo kutakuimarisha uendelee kumtumikia Yehova ukiwa na moyo kamili na nafsi yenye shangwe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki