Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada za pekee zitafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Ikiwa watu tayari wana kichapo hicho, kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kinaweza kutolewa. Aprili na Mei: Toa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho au matukio mengine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani na tengenezo, jitahidi kuwatolea kitabu Mwabudu Mungu. Jitahidi sana kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa na watu ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Watu fulani wakisema kwamba hawana watoto, watolee broshua Anataka. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ukitumia broshua hiyo.
◼ Kuanzia Machi 1, 2004, nchi ya Burundi itakuwa na ofisi ya tawi.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza kichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali shughulikieni ifaavyo bidhaa za ombi la pekee.
◼ Ni muhimu vikundi vya watu 20 au zaidi wanaopanga kutembelea ofisi ya tawi wawasiliane kwanza na ofisi kupitia barua. Tafadhali andikeni idadi ya watakaokuja, tarehe na saa ya kuwasili. Kabla ya kuja, tafadhali pitieni Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2002 kuhusu mavazi na mapambo yanayofaa mnapotembelea makao ya Betheli.
◼ Wahubiri wanaokabiliwa na masuala ya kawaida juu ya malezi ya watoto au haki ya kutembelea watoto, wanaweza kupata habari muhimu katika gazeti la Amkeni! la Desemba 8, 1997, ukurasa wa 3-12; katika Amkeni! la Oktoba 22, 1988, ukurasa wa 2-14 (toleo la Kiingereza); na kwenye chati inayopatikana katika Amkeni! la Oktoba 8, 1991, ukurasa wa 9.
◼ Mwandishi anapaswa kuhakikisha kwamba Dawati la Ujenzi wa Majumba ya Ufalme lina habari za karibuni za wahubiri wote waliobatizwa waliojaza fomu ya Kingdom Hall Volunteer Worker Questionnaire (S-82). Ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika hali ya mjitoleaji, kama vile kuhama au kuwekwa rasmi kuwa mtumishi wa huduma au mzee, fomu mpya inapaswa kujazwa na kutumwa mara moja. Ikiwa anwani au namba ya simu ya mjitoleaji imebadilika au ikiwa hana tena msimamo mzuri kutanikoni, wazee wanapaswa kuandikia Dawati la Ujenzi wa Majumba ya Ufalme mara moja. Anapozuru kutaniko, mwangalizi wa mzunguko anapaswa kupewa faili ya kutaniko yenye fomu za S-82 ili azipitie.