Habari Inayowasaidia Watu
Wakristo wa kweli hushiriki huduma ya watu wote ya kueneza habari njema. (Flp. 2:17) Ili kutimiza hilo, baadhi ya broshua, trakti, na makala za msingi katika lugha 20 zimewekwa kwenye Intaneti yenye anwani www.watchtower.org. Kituo hicho cha Intaneti hakikusudiwi kugawanya vichapo vya sasa kwa Mashahidi wa Yehova. Lengo lake ni kuwajulisha watu wote habari sahihi kuhusu yale ambayo Mashahidi wa Yehova hufundisha katika Biblia.
Hivi karibuni, habari zaidi zimeongezwa katika kituo chetu rasmi kwenye Intaneti. Broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? katika lugha zaidi ya 220 zimetiwa humo. Pia, anwani yetu ya Intaneti itaonyeshwa katika ukurasa wa mwisho wa magazeti yetu kuanzia Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari 8, 2004, katika lugha zote.
Unaweza kutumiaje kifaa hicho? Huenda ukakutana na mtu anayeonekana kuwa anapendezwa lakini anaelewa tu lugha tofauti. Ikiwa anaweza kutumia Intaneti, unaweza kumwonyesha anwani hiyo katika ukurasa wa mwisho kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi au Amkeni! Kwa kutumia anwani hiyo, anaweza kusoma broshua Anataka katika lugha yake mwenyewe hadi utakapomletea vichapo vya lugha yake. Au unaweza kumwelekeza kwenye kutaniko au kikundi cha watu wa lugha yake.