Vikumbusho vya Ukumbusho
Mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu utafanywa Jumapili, Aprili 4. Wazee wanapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:
◼ Mnapopanga saa za mkutano, hakikisheni kwamba mifano haipitishwi kabla ya jua kushuka.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, apaswa kujulishwa saa kamili na mahali hususa pa mwadhimisho.
◼ Matayarisho ya mkate na divai inayofaa yapaswa kufanywa mapema.—Ona Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 2003, ukurasa wa 14-15.
◼ Sahani, glasi, meza, na kitambaa kifaacho cha meza vyapasa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkutano huo papaswa kusafishwa kabisa mapema.
◼ Wakaribishaji na watakaopitisha mifano wapasa kuteuliwa na kuelezwa mapema kuhusu wajibu wao, utaratibu utakaofuatwa, na uhitaji wa kuvalia kwa njia ya heshima.
◼ Mipango yapasa kufanywa ili kuwapelekea mifano watiwa-mafuta wowote ambao ni wagonjwa na hawawezi kufika.
◼ Makutaniko kadhaa yanapotumia Jumba moja la Ufalme, kwapaswa kuwe na makubaliano mazuri miongoni mwa makutaniko hayo ili kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye jumba, milangoni, nje ya jumba, na kwenye maegesho ya magari.