Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho
Siku ya Ukumbusho mwaka huu ni Jumatatu, Aprili 2. Wazee wanapaswa kukumbuka mambo yafuatayo.
◼ Mnapopanga saa ya mkutano huo, hakikisheni kwamba mkate na divai havipitishwi kabla ya jua kushuka.
◼ Wote, kutia ndani msemaji, wajulishwe saa na mahali pa maadhimisho.
◼ Fanyeni mipango mapema ili kuwe na mkate na divai inayofaa.—Ona toleo la Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 2003, uku. 14-15.
◼ Sahani, glasi, meza inayofaa na kitambaa cha meza kinachofaa viletwe kwenye jumba na kupangwa mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine ambapo maadhimisho hayo yatafanywa pasafishwe kabisa mapema.
◼ Wakaribishaji na wale watakaopitisha mkate na divai wanapaswa kuteuliwa na kuelezwa mapema juu ya majukumu yao, utaratibu unaofaa kufuatwa, na umuhimu wa kuwa nadhifu na kuvalia mavazi yenye kuheshimika.
◼ Pangeni kuandaa mkate na divai kwa ajili ya watiwa-mafuta walio wagonjwa na wasioweza kuhudhuria.
◼ Ikiwa makutaniko zaidi ya moja yatatumia Jumba la Ufalme lilelile, makutaniko yafanye mipango inayofaa ili kusiwe na msongamano kwenye jumba, milangoni, nje ya jumba, au kwenye maegesho ya magari.