Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Mei 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ikiwa madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 yanafaa eneo la kutaniko lenu, yatumie kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15 na Amkeni! la Aprili 22. Madokezo mengine yanaweza kutumiwa. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Nina dini yangu mwenyewe.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 18-19.
Dak. 15: Je, Umemwomba Mwajiri Wako Ruhusa? Mzee ashughulikia sehemu hii kwa njia ya hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea makala, “Je, Utakuwapo?” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2000, ukurasa wa 1. Tia ndani maelezo kutoka kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 67.
Dak. 20: “Panukeni.”a Tia ndani maelezo kutoka kitabu Mwabudu Mungu, ukurasa wa 150 fungu la 14.
Wimbo 18 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Onyesha Shukrani Zako.”b Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyotajwa. Unapozungumzia fungu la 3, mwombe mhubiri mmoja au wawili waliofanya upainia msaidizi hivi karibuni waeleze baraka walizopata.
Dak. 20: Sisi Hutunzana. (1 Kor. 12:25, 26) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa 157-159, chini ya kichwa kidogo “Kuhangaikiana.” Ingawa watu wa Yehova huishi sehemu zote duniani, sote tumeungana kwa umoja. Imetupasa sote tusali kila siku kwa ajili ya ndugu zetu. Sisi pia hufanya haraka kutoa msaada wa vitu vya kimwili mahitaji ya dharura yanapotokea. Soma na kuzungumzia maandiko makuu, na utie ndani jambo moja au mawili yaliyoonwa kutoka katika vichapo vyetu.
Wimbo 100 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 24
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Onyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na Amkeni! la Mei 8. Rekebisha kila onyesho ili limvutie mtu katika eneo lenu.
Dak. 15: “Muziki Unaoburudisha.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani maelezo kutoka Kitabu cha Mwaka cha 2002, ikiwa kinapatikana, ukurasa wa 175, na gazeti Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1997, ukurasa wa 27, fungu la 1-2.
Dak. 18: Uwe Tayari Kuhubiri kwa Njia Isiyo Rasmi. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2003, ukurasa wa 3. Panga mapema wahubiri wachache waeleze mambo waliyoona walipokuwa wakihubiri kwa njia isiyo rasmi. Toa onyesho fupi la jinsi trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? na kijitabu Good News for All Nations, ikiwa kinapatikana, vinaweza kutumiwa tunapohubiri kwa njia isiyo rasmi.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 31
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Mei.
Dak. 17: Uhai—Zawadi ya Kuthaminiwa. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 395-397. Tia ndani maelezo kutoka Amkeni! Mei 22, 1993, ukurasa wa 10-11. Unaweza kuelezaje maoni ya Yehova kuhusu utoaji-mimba kwa mtu aliye na maoni kwamba mwanamke ana haki ya kuamua mambo yanayohusu mwili wake mwenyewe? Simulia jambo lililoonwa katika gazeti Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2000, ukurasa wa 4, fungu la 4-5.
Dak. 20: “Kutoa Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu.” Tutatoa kitabu hiki mwezi wa Juni. Taja mambo yaliyofafanuliwa kwenye ukurasa wa 7, fungu la 1-3 katika kitabu hiki. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu mambo yanayowapendeza katika sehemu hiyo. Pitia matangulizi yaliyodokezwa. Kazia jinsi picha zinavyoweza kutumiwa unapotoa kitabu hiki. Panga kijana atoe onyesho la kwanza, na mtu mzima atoe mojawapo ya yale mengine mawili. Ikiwa utangulizi tofauti utafaa zaidi eneo lenu, uzungumzieni na kuonyesha jinsi unavyoweza kutumiwa badala ya mmoja wa yale yaliyotajwa.
Wimbo 24 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Waombe wasikilizaji waeleze faida za kuwa na Jumba la Ufalme. Watie moyo akina ndugu waendelee kuunga mkono programu ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Tumia Vielezi Vyenye Matokeo Unapofundisha. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 2002, ukurasa wa 22-24. Ni mambo gani manne yanayofanya kielezi kiwe na matokeo? Kwa nini inafaa kutoa vielezi rahisi? Tunaweza kupata wapi vielezi vinavyofaa? Pitia baadhi ya vielezi vinavyotajwa kwenye sanduku katika ukurasa wa 23, na uzungumzie ni nini kinachofanya kila kielezi kiwe chenye matokeo.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.