-
Kujulisha Jina la Yehova Katika Dunia YoteHuduma ya Ufalme—2000 | Januari
-
-
Kujulisha Jina la Yehova Katika Dunia Yote
1 Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawe mashahidi “hadi sehemu ya mbali sana ya dunia,” alikuwa tayari amewawekea kielelezo cha kufuata. (Mdo. 1:8) Wakati wowote na mahali popote alipopata watu, alizungumza nao kuhusu kusudi la Mungu kwa wanadamu. Kwa kumwiga Yesu, jamii ya mtumwa mwaminifu inatumia njia mbalimbali kufanya jina la Yehova ‘lijulikane katika dunia yote.’—Isa. 12:4, 5.
2 Yaliyofanywa Siku za Zamani: Katika miaka iliyopita mahubiri yalichapishwa katika magazeti; ile “Photo-Drama of Creation” ilitolewa na kuonyeshwa kwa mamilioni; magari yenye vikuza-sauti yalitumiwa; kinanda cha gramafoni kilitumiwa sana na kwa muda fulani redio—yote hayo yalitumiwa ili kuhubiri habari njema. Bila shaka, mkazo umetiliwa katika kukutana na watu kibinafsi ili upendezi wowote unaoonyeshwa uweze kufuatiwa. Kwa sababu hiyo, huduma ya nyumba hadi nyumba imekuwa njia yenye matokeo sana katika kufanya jina la Yehova lijulikane kila mahali.—Mdo. 5:42.
3 Yanayofanywa Katika Siku Yetu: Kadiri nyakati zinavyoendelea kubadilika ulimwengu nao wasonga kwa kasi sana, na katika mahali pengi watu hawapatikani sana nyumbani. Wachache wana mwelekeo wa kutumia wakati wakisoma na kutafakari juu ya mambo ya kiroho. Kwa hiyo, ni lazima huduma yetu ibadilikane ili kufaa hali. Kwa kuongezea kuendelea kumaliza eneo kwa kuhubiri nyumba hadi nyumba, tumetiwa moyo kwenda mahali watu walipo na ‘kuwa tayari sikuzote’ kutetea tumaini tulilo nalo. (1 Pet. 3:15) Hilo lamaanisha kujitahidi kuwahubiria wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, watu barabarani, na katika bustani au katika maegesho ya magari, duka hadi duka na mahali pengine popote ambapo watu waweza kupatikana. Tukiwa na utegemezo wa Yehova kazi yetu itafanikiwa sana. Je, wewe unashiriki kuwafikia watu popote walipo?
4 Acheni sisi sote binafsi tutumie kila njia tuwezayo ili kufanya jina la Yehova lijulikane katika eneo letu. Tunaweza kupata uradhi katika kutimiza kikamili huduma yetu, tukitarajia Yehova awavute wenye mioyo minyoofu.—Yoh. 6:44.
-
-
Je, Utakuwapo?Huduma ya Ufalme—2000 | Januari
-
-
Je, Utakuwapo?
1 Shahidi mmoja wa muda mrefu alisema hivi: “Ukikosa siku ya kwanza ya kusanyiko, tayari unakuwa umekosa mengi sana!” Kwa nini alihisi hivyo? Kwa sababu siku ya kwanza ndiyo mwanzo wa karamu nono ya kiroho ambayo tunaandaliwa na tengenezo la Yehova. (Isa. 25:6) Tunapokuwapo kuanzia mwanzo, hiyo huonyesha kwamba twakubaliana na maneno ya mtunga-zaburi aliyesema: “Nilifurahi waliponiambia, na twende nyumbani kwa BWANA.”— Zab. 122:1.
2 Hata hivyo, mwaka jana katika baadhi ya mikusanyiko ya wilaya ya “Neno la Mungu la Kiunabii,” siku ya Ijumaa hudhurio lilikuwa chini kidogo kuliko Jumamosi na Jumapili. Hii yamaanisha kwamba asilimia kubwa ya ndugu na dada zetu walikosa kusikiliza sehemu za kusanyiko ambazo zilitoa habari muhimu kuhusu neno la kiunabii. Wao pia walipoteza ushirika wenye kupendeza pamoja na waamini wenzi.
3 Usiruhusu Kazi ya Kimwili Iingilie Kati: Hangaiko kuhusu kuhatarisha kazi ya kuajiriwa laweza kuwa ndiyo sababu iliyowafanya wengine wasihudhurie siku ya Ijumaa. Hata hivyo, Mashahidi wengi wamepata kwamba waajiri wao wako tayari kushirikiana nao katika jambo hili ikiwa tu wanaomba ruhusa mapema. Mwajiri mmoja alivutiwa sana na jinsi dada mmoja painia alivyoazimia kuhudhuria mikutano yote ya kutaniko na makusanyiko hivi kwamba mwajiri huyo alitumia siku nzima katika kusanyiko ambalo dada huyo alihudhuria!
4 Usidhanie kwamba mwajiri wako hatakupa ruhusa, au kukata kauli kwamba kukosa siku moja ya kusanyiko si kitu. Ukiwa na usadikisho wenye kuhisiwa moyoni jitayarishe kumwonyesha mwajiri wako kupitia Maandiko sababu kwa nini kuhudhuria kusanyiko ni sehemu muhimu ya ibada yako. (Ebr. 10:24, 25) Kisha weka tumaini lako katika ahadi za Yehova, ukitambua kwamba chochote utakachohitaji kimwili atakuandalia ukiweka mahitaji ya kiroho kwanza maishani.—Mt. 6:33; Ebr. 13:5, 6.
5 Jambo muhimu ni kuthamini “mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10, 11; Zab. 27:4) Hilo hutusukuma tufanye mipango ili tunufaike kikamili kutokana na uandalizi huu muhimu kutoka kwa Yehova. Anza kufanya mipango yako kamili sasa, na uazimie kwamba utakuwapo siku zote tatu!
-