Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Je, umewahi kujiuliza maoni ya Mungu kuhusu mambo ambayo wanadamu hufanya duniani? [Ngoja jibu.] Ona jinsi Mungu anavyoyaona matendo yetu. [Soma Methali 27:11.] Gazeti hili linazungumzia watu kadhaa ambao waliufurahisha moyo wa Mungu na linaeleza jinsi tunavyoweza kufanya vivyo hivyo.”
Amkeni! Mei 22
“Sayansi ya tiba imeleta maendeleo makubwa sana katika kutibu magonjwa, lakini je, unafikiri tutaona ulimwengu usio na magonjwa hata kidogo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linaeleza kwamba wakati utafika ambapo kila mtu duniani atafurahia afya kamilifu, kwa kuwa unabii huu utakuwa umetimia.” Soma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Watu fulani hawaoni ni lazima wawe washiriki wa dini fulani ili wamwabudu Mungu. Je, umewahi kufikiria jambo hilo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linachunguza jinsi Mungu alivyoshughulika na watu nyakati za zamani. Pia linazungumzia maana ya kumwabudu Mungu katika kweli.” Soma Yohana 4:24.
Amkeni! Juni 8
“Leo watu wengi wana upweke. Wao huhisi kwamba wametengwa na wengine. Je, huoni kuwa jambo hilo linahuzunisha? [Ngoja jibu. Kisha soma Zaburi 25:16.] Gazeti hili la Amkeni! linatoa madokezo ya kupambana na upweke.”