Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Oktoba 1-17: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa, mwachie broshua Anataka, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Oktoba 18–Novemba 14: Kampeni ya pekee ya kugawa broshua Endeleeni Kukesha! Novemba 15-30: Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mtu akisema kwamba hana watoto, toa broshua Anataka. Unapotumia broshua hiyo, jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Desemba: Toa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi au unaweza kutoa vichapo vingine kama vile, Biblia—Neno la Mungu au la Mwanadamu, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.
◼ Nyongeza iliyo katika toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme ni “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2005” na inapaswa kutunzwa kwa kuwa itatumiwa mwaka huo mzima.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza vichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali shughulikieni ifaavyo bidhaa za kuagizwa kipekee.