Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/04 kur. 3-6
  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2005

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2005
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Vichwa vidogo
  • Maagizo
  • RATIBA
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 10/04 kur. 3-6

Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2005

Maagizo

Katika mwaka wa 2005, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itafuata utaratibu unaoonyeshwa hapa.

VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [bi12], Mnara wa Mlinzi [w], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Toleo la 2004) [rs].

Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI kwa wimbo, sala, na maneno ya kuwakaribisha wasikilizaji. Kisha fuateni utaratibu huu unaofuata:

SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri-msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi katika kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, mtumishi wa huduma anayestahili anaweza kutumiwa.) Ikiwa maagizo mengine hayajatolewa, masanduku yaliyo kwenye kurasa ambazo mgawo huo unategemea yanapaswa kuzungumziwa. Mazoezi ya kila somo yasishughulikiwe. Mazoezi hayo yamekusudiwa kutumiwa na wanafunzi na pia ili kutoa ushauri faraghani.

HOTUBA NA. 1: Dakika 10. Hotuba hii itolewe na mzee au mtumishi wa huduma wanaostahili, na habari zitategemea Mnara wa Mlinzi, Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hotuba hii ya maagizo itolewe kwa dakika kumi bila maswali ya kurudia. Lengo la hotuba hii si kuzungumzia tu habari ambayo imeandaliwa bali ni kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa maishani, na kukazia mambo ambayo yatafaidi kutaniko. Kichwa kilichoonyeshwa ndicho kitatumiwa. Ndugu wanaopewa mgawo huu wanapaswa kumaliza kwa wakati. Ndugu anaweza kushauriwa faraghani inapohitajika.

MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee, au mtumishi wa huduma, anayestahili, atumie dakika sita za kwanza kuonyesha jinsi habari hiyo inavyohusu hali zenu. Anaweza kuzungumzia sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo. Mgawo huu si kutoa tu muhtasari wa usomaji wa Biblia. Lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji waelewe ni kwa nini habari hiyo ni yenye faida na jinsi inavyowafaidi. Msemaji awe mwangalifu asipitishe zile dakika zake sita za kwanza. Ahakikishe kwamba dakika nne zinabaki za wasikilizaji kupata nafasi ya kutoa maelezo. Awaombe wasikilizaji watoe maelezo mafupi (ya nusu dakika au hata fupi zaidi) kuhusu mambo yaliyowapendeza katika usomaji wa Biblia na faida yake. Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili au ya tatu kuondoka.

HOTUBA NA. 2: Dakika 4. Ndugu anapaswa kugawiwa usomaji huu. Kwa kawaida ni Biblia itakayosomwa. Mara moja kwa mwezi, sehemu fulani katika Mnara wa Mlinzi itasomwa. Mwanafunzi asome habari hiyo bila kutoa utangulizi wala umalizio. Sehemu zilizoratibiwa za kila juma zinatofautiana kidogo kwa urefu, lakini inawezekana kuzisoma kwa dakika nne au chini ya dakika nne. Mwangalizi wa shule achunguze habari hiyo kabla ya kumgawia yeyote mgawo huu, ili kuhakikisha kwamba habari zinafaa umri na uwezo wa mwanafunzi. Mwangalizi wa shule azingatie hasa kuwasaidia wanafunzi kusoma kwa njia yenye kueleweka, kwa ufasaha, kwa kukazia maana kwa njia inayofaa, kwa ubadilifu wa sauti, kutua kwa njia inayofaa, na kusoma kwa njia ya maongezi ya kawaida.

HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Dada atapewa mgawo huu. Wanafunzi wanaopewa mgawo huu ama watapewa kikao ama watachagua kikao katika orodha ya vikao iliyo kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani kwenye eneo la kutaniko lenu. Iwapo vichapo vya kutumiwa havijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Wanafunzi wapya wapewe migawo inayoonyesha vichapo vya kutumiwa. Mwangalizi wa shule atazingatia hasa jinsi mwanafunzi anavyoeleza habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na mambo makuu. Wanafunzi wanaogawiwa hotuba hiyo wanapaswa kujua kusoma. Mwangalizi wa shule atateua msaidizi mmoja.

HOTUBA NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi azungumzie kichwa kilichoonyeshwa. Ikiwa vichapo vya kutumiwa havijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hii katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Ndugu anapopewa mgawo huu, autoe kama hotuba inayofaa wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapopewa mgawo huu, autoe jinsi Hotuba Na. 3 inavyotolewa. Mwangalizi wa shule anaweza kumpa ndugu Mgawo Na. 4 anapoona inafaa kufanya hivyo. Tafadhali, vichwa vilivyotiwa alama ya nyota vipewe akina ndugu pekee ili wavitoe kama hotuba.

WAKATI: Wala hotuba wala maelezo ya mshauri yasipitishe wakati kamwe. Wanafunzi wanaotoa Hotuba Na. 2 hadi Na. 4 wakatizwe kwa busara muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa hotuba ya kwanza ya sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu ya usomaji wa Biblia, washauriwe faraghani wakipitisha wakati. Wote wanapaswa kufuata wakati. Programu nzima: Dakika 45, mbali na wimbo na sala.

SHAURI: Dakika 1. Baada ya kila mgawo wa mwanafunzi, mwangalizi wa shule atatumia muda usiozidi dakika moja kutoa maelezo yanayojenga kuhusu jambo linalostahili kusifiwa katika hotuba hiyo. Lengo lake si kupongeza tu, bali ni kuonyesha ni kwa nini jambo fulani katika hotuba lilikuwa zuri. Kulingana na uhitaji, mwanafunzi anaweza kupewa mashauri mengine faraghani baada ya mkutano au wakati mwingine yatakayomsaidia afanye maendeleo.

MSHAURI MSAIDIZI: Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo mbali na mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kumteua kuwa mshauri msaidizi. Ikiwa kuna wazee wengi katika kutaniko, basi mzee tofauti anayestahili anaweza kushughulikia mgawo huo mwaka mwingine. Daraka la mshauri msaidizi ni kuwashauri faraghani akina ndugu wanaoshughulikia Hotuba Na. 1 na mambo makuu ya usomaji wa Biblia, ikiwa kuna uhitaji. Si lazima awashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo. Utaratibu huo utafuatwa mwaka wa 2005 na huenda mabadiliko fulani yakafanywa baadaye.

FOMU YA MASHAURI: Imo katika kitabu cha shule.

PITIO LA MASWALI NA MAJIBU: Dakika 30. Kila baada ya miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio la maswali na majibu. Sehemu hiyo itafanywa baada ya sifa ya usemi na mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama inavyoonyeshwa hapa juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio. Ikiwa kutaniko lenu lina kusanyiko la mzunguko au mwangalizi wa mzunguko analitembelea juma la pitio, fuateni maagizo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 2003, ukurasa wa 6.

RATIBA

Jan. 3 Usomaji wa Biblia: Yoshua 16-20 Wimbo 6

Sifa ya Usemi: Usemi Unaoeleweka (be uku. 226 ¶1–uku. 227 ¶1)

Na. 1: Hofu Mungu wa Kweli (be uku. 272 ¶1–uku. 273 ¶1)

Na. 2: Yoshua 16:1–17:4

Na. 3: Kwa Nini Haitoshi Tu Kusoma Biblia? (rs uku. 64 ¶3-4)

Na. 4: Je, Utajiri au Umaskini Unaonyesha Kwamba Mtu Anamcha Mungu?

Jan. 10 Usomaji wa Biblia: Yoshua 21-24 Wimbo 100

Sifa ya Usemi: Kufafanua Maneno Yasiyoeleweka (be uku. 227 ¶2–uku. 228 ¶1)

Na. 1: Kutangaza Jina la Mungu (be uku. 273 ¶2–uku. 274 ¶1)

Na. 2: Yoshua 23:1-13

Na. 3: Dini ya Kweli Inategemea Biblia na Inatangaza Jina la Mungu (rs uku. 65 ¶1-2)

Na. 4: Je, Inafaa Kumwabudu Yesu?

Jan. 17 Usomaji wa Biblia: Waamuzi 1-4 Wimbo 97

Sifa ya Usemi: Kueleza Mambo Magumu (be uku. 228 ¶2-3)

Na. 1: Utu wa Yehova (be uku. 274 ¶2-5)

Na. 2: Waamuzi 2:1-10

Na. 3: Dini ya Kweli Inaonyesha Imani ya Kweli Katika Yesu Kristo (rs uku. 65 ¶3)

Na. 4: Unawezaje Kujilinda na Video za Muziki Wenye Kudhuru?

Jan. 24 Usomaji wa Biblia: Waamuzi 5-7 Wimbo 47

Sifa ya Usemi: Jinsi Moyo Unavyohusika (be uku. 228 ¶4–uku. 229 ¶1)

Na. 1: Jina la Mungu Ni “Ngome Imara” (be uku. 274 ¶6–uku. 275 kichwa kidogo)

Na. 2: Waamuzi 6:25-35

Na. 3: Biblia Inahusikaje na Uhuru Wetu wa Kufanya Maamuzi?

Na. 4: Dini ya Kweli Si ya Kidesturi, Bali Inaongoza Maisha Yetu (rs uku. 65 ¶4)

Jan. 31 Usomaji wa Biblia: Waamuzi 8-10 Wimbo 174

Sifa ya Usemi: Kuwaelimisha Wasikilizaji (be uku. 230 ¶1-6)

Na. 1: Kutoa Ushahidi Kumhusu Yesu (be uku. 275 kichwa kidogo–¶4)

Na. 2: w03 1/15 uku. 19-20 ¶16-18

Na. 3: Wafuasi wa Dini ya Kweli Wanapendana na Kujitenga na Ulimwengu (rs uku. 65 ¶5–uku. 66 ¶1)

Na. 4: Ufuatiaji wa Vitu vya Kimwili Haumaanishi Tu Ukusanyaji wa Mali

Feb. 7 Usomaji wa Biblia: Waamuzi 11-14 Wimbo 209

Sifa ya Usemi: Kuelimisha Watu kwa Kufanya Utafiti (be uku. 231 ¶1-3)

Na. 1: Kukazia Daraka la Yesu Akiwa Mkombozi (be uku. 276 ¶1-2)

Na. 2: Waamuzi 12:1-15

Na. 3: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wana Umoja?

Na. 4: Wafuasi wa Dini ya Kweli Wanatoa Ushuhuda Kuhusu Ufalme wa Mungu (rs uku. 66 ¶2)

Feb. 14 Usomaji wa Biblia: Waamuzi 15-18 Wimbo 105

Sifa ya Usemi: Kuyafafanua Maandiko (be uku. 231 ¶4-5)

Na. 1: Kukazia Daraka la Yesu Akiwa Kuhani Mkuu na Kichwa wa Kutaniko (be uku. 277 ¶1-2)

Na. 2: Waamuzi 15:9-20

Na. 3: aMtu Akisema, ‘Haidhuru Unashirikiana na Kanisa Gani, Maadamu Umwamini Yesu’ (rs uku. 68 ¶3)

Na. 4: Kwa Nini Wakristo Wanakataa Kupumbazwa Akili?

Feb. 21 Usomaji wa Biblia: Waamuzi 19-21 Wimbo 53

Sifa ya Usemi: Kufafanua Mambo (be uku. 232 ¶1)

Na. 1: Kukazia Daraka la Yesu Akiwa Mfalme Anayetawala (be uku. 277 ¶3-4)

Na. 2: w03 2/1 uku. 17-18 ¶18-21

Na. 3: bMtu Akisema, ‘Kwa Nini Unafikiri Kwamba Kuna Dini Moja Tu ya Kweli?’ (rs uku. 68 ¶4)

Na. 4: Baadhi ya “Mambo Mazito ya Mungu” Ni Yapi? (1 Kor. 2:10)

Feb. 28 Usomaji wa Biblia: Ruthu 1-4 Wimbo 120

Sifa ya Usemi: Kutoa Sababu ili Maandiko Yaeleweke (be uku. 232 ¶2-4)

Pitio la Maswali na Majibu

Mac. 7 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 1-4 Wimbo 221

Sifa ya Usemi: Kuchagua Habari Zitakazowafaidi Wasikilizaji (be uku. 232 ¶5–uku. 233 ¶1-4)

Na. 1: Kuweka Kristo Kuwa Msingi (be uku. 278 ¶1-4)

Na. 2: 1 Samweli 2:1-11

Na. 3: Yesu Hakupaa Mbinguni Katika Mwili wa Nyama (rs uku. 320 ¶2–uku. 321 ¶2)

Na. 4: Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawajihusishi na Utabiri wa Nyota?

Mac. 14 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 5-9 Wimbo 151

Sifa ya Usemi: Kutumia Habari Ambazo Umepewa (be uku. 234 ¶1–uku. 235 ¶3)

Na. 1: Habari Njema Hii ya Ufalme (be uku. 279 ¶1-4)

Na. 2: 1 Samweli 5:1-12

Na. 3: Kwa Nini Yesu Alijitokeza Katika Miili ya Nyama? (rs uku. 321 ¶3–uku. 322 ¶2)

Na. 4: Jinsi Tunavyoweza Kuimarisha Urafiki Wetu na Yehova

Mac. 21 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 10-13 Wimbo 166

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali Vizuri (be uku. 236 ¶1-5)

Na. 1: Kufafanua Maana ya Ufalme (be uku. 280 ¶1-5)

Na. 2: 1 Samweli 10:1-12

Na. 3: Wakristo Wanapaswa Kuwatendeaje Jamaa Zao Wasioamini?

Na. 4: Wale Watakaofufuliwa ili Kutawala na Kristo Watakuwa na Miili Kama Yake (rs uku. 322 ¶4–uku. 323 ¶1)

Mac. 28 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 14-15 Wimbo 172

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali ili Kutokeza Mambo Muhimu (be uku. 237 ¶1-2)

Na. 1: Kueleza Jinsi Ufalme Unavyotuhusu (be uku. 281 ¶1-4)

Na. 2: w03 3/15 uku. 19-20 ¶17-21

Na. 3: Kwa Nini Wakristo Hulipa Kodi?

Na. 4: Ufufuo Utamaanisha Nini kwa Watu Wengi (rs uku. 323 ¶2–uku. 324 ¶2)

Apr. 4 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 16-18 Wimbo 27

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali ili Kusababu Juu ya Habari (be uku. 237 ¶3–uku. 238 ¶2)

Na. 1: Kwa Nini Elimu Ni Muhimu kwa Wakristo? (w03 3/15 uku. 10 ¶1–uku. 11 ¶5)

Na. 2: 1 Samweli 17:41-51

Na. 3: Kwa Nini Watakaofufuliwa Hawataadhibiwa kwa Sababu ya Matendo Yao ya Zamani (rs uku. 324 ¶4)

Na. 4: Kutafakari Juu ya Matokeo ya Matendo Yetu Kunaweza Kutusaidia Kupenda Mema na Kuchukia Mabaya

Apr. 11 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 19-22 Wimbo 73

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali ili Kutambua Hisia za Moyoni (be uku. 238 ¶3-5)

Na. 1: Jinsi Vijana Wanavyoweza Kufanya Maendeleo ya Kiroho (w03 4/1 uku. 8-10)

Na. 2: 1 Samweli 20:24-34

Na. 3: Kwa Nini Unyenyekevu Ni Sifa Inayovutia?

Na. 4: Jinsi “Wale Wafu Wengine” Watakavyokuwa Hai Duniani (rs uku. 325 ¶1–uku. 326 ¶1)

Apr. 18 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 23-25 Wimbo 61

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali ili Kutia Mkazo (be uku. 238 ¶6–uku. 239 ¶1)

Na. 1: Mtumaini Yehova kwa Moyo Wako Wote (w03 11/1 uku. 4-7)

Na. 2: w03 5/1 uku. 17 ¶11-14

Na. 3: Wale Watakaotiwa Ndani ya Ufufuo wa Kuishi Duniani (rs uku. 326 ¶2–uku. 327 ¶3)

Na. 4: Kwa Nini Mungu Alifanya Agano na Abrahamu?

Apr. 25 Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 26-31 Wimbo 217

Sifa ya Usemi: Kutumia Maswali ili Kufichua Fikira Zisizofaa (be uku. 239 ¶2-4)

Pitio la Maswali na Majibu

Mei 2 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 1-3 Wimbo 91

Sifa ya Usemi: Mifano Aina ya Tashbihi na Sitiari Inayofundisha (be uku. 240 ¶1–uku. 241 ¶1)

Na. 1: Lengo la Elimu Si Kupata Kazi Tu (w03 3/15 uku. 11 ¶6–uku. 14 ¶6)

Na. 2: 2 Samweli 2:1-11

Na. 3: Matukio Yanayohusianishwa na Kuwapo kwa Kristo Hutukia Katika Kipindi cha Miaka Kadhaa (rs uku. 116 ¶1-2)

Na. 4: Faida Nyingi za Kuwa Mnyoofu

Mei 9 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 4-8 Wimbo 183

Sifa ya Usemi: Kutumia Mifano (be uku. 241 ¶2-4)

Na. 1: Yehova Anawajali Kikweli Vijana (w03 4/15 uku. 29 ¶3–uku. 31 ¶4)

Na. 2: 2 Samweli 5:1-12

Na. 3: Agano la Sheria Lilitimiza Nini?

Na. 4: Kurudi kwa Kristo Hakuonekani kwa Macho (rs uku. 116 ¶3–uku. 117 ¶2)

Mei 16 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 9-12 Wimbo 66

Sifa ya Usemi: Mifano Katika Maandiko (be uku. 242 ¶1-2)

Na. 1: Je, Yehova Huona Yale Unayofanya? (w03 5/1 uku. 28-31)

Na. 2: 2 Samweli 9:1-13

Na. 3: Kurudi kwa Yesu na Jinsi Kila Jicho Litakavyomwona (rs uku. 117 ¶4–uku. 118 ¶5)

Na. 4: Neno la Mungu Liko Hai kwa Njia Zipi? (Ebr. 4:12)

Mei 23 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 13-15 Wimbo 103

Sifa ya Usemi: Je, Mfano Huo Unaeleweka? (be uku. 242 ¶3–uku. 243 ¶1)

Na. 1: Je, Maandishi ya Noa Yana Maana Kwetu? (w03 5/15 uku. 4-7)

Na. 2: 2 Samweli 13:10-22

Na. 3: Yohana 11:25, 26 Linamaanisha Nini?

Na. 4: Matukio Yanayohusianishwa na Kuwapo kwa Kristo (rs uku. 119 ¶1-5)

Mei 30 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 16-18 Wimbo 132

Sifa ya Usemi: Mifano ya Hali za Kawaida (be uku. 244 ¶1-2)

Na. 1: Fikiri kwa Njia Inayofaa na Utende kwa Hekima (w03 7/15 uku. 21-23)

Na. 2: w03 5/15 uku. 16-17 ¶8-11

Na. 3: Wakristo Hawana Wajibu wa Kushika Sabato (rs uku. 250 ¶1–uku. 251 ¶3)

Na. 4: Kwa Nini Unyenyekevu Si Udhaifu?

Juni 6 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 19-21 Wimbo 224

Sifa ya Usemi: Mifano Inayowafaa Wasikilizaji (be uku. 244 ¶3–uku. 245 ¶4)

Na. 1: Kuelewa Kusudi la Nidhamu (w03 10/1 uku. 20 ¶1–uku. 21 ¶6)

Na. 2: 2 Samweli 19:1-10

Na. 3: Mkristo Anawezaje Kuingia Katika Pumziko la Mungu?

Na. 4: Biblia Haisemi Kama Adamu Alishika Sabato (rs uku. 251 ¶4–uku. 252 ¶2)

Juni 13 Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 22-24 Wimbo 74

Sifa ya Usemi: Kutumia Vizuri Vielelezo (be uku. 247 ¶1-2)

Na. 1: Uwe Mwenye Kufundishika na Uulinde Ulimi Wako (w03 9/15 uku. 21 ¶1–uku. 22 ¶4)

Na. 2: 2 Samweli 24:10-17

Na. 3: Yesu Hakugawanya Sheria ya Musa Katika Sehemu ya “Sherehe” na ya “Adili” (rs uku. 252 ¶3–uku. 253 ¶1)

Na. 4: Mkristo Anapaswa Kujitenga na Ulimwengu kwa Njia Zipi?

Juni 20 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 1-2 Wimbo 2

Sifa ya Usemi: Jinsi Yesu Alivyotumia Vielelezo (be uku. 247 ¶3)

Na. 1: Kujifunza Siri ya Kutosheka (w03 6/1 uku. 8-11)

Na. 2: w03 6/1 uku. 12-13 ¶1-4

Na. 3: Amri ya Kumi Ilikuwa ya Kipekee kwa Njia Gani?

Na. 4: Zile Amri Kumi Ziliondolewa Pamoja na Sheria ya Musa (rs uku. 253 ¶2-3)

Juni 27 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 3-6 Wimbo 167

Sifa ya Usemi: Njia za Kutumia Vielelezo (be uku. 248 ¶1-3)

Pitio la Maswali na Majibu

Julai 4 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 7-8 Wimbo 194

Sifa ya Usemi: Kutumia Ramani, Programu Zilizochapwa za Makusanyiko, na Video (be uku. 248 ¶4–uku. 249 ¶2)

Na. 1: Wathamini Waamini Wenzako Waliozeeka (w03 9/1 uku. 30-31)

Na. 2: 1 Wafalme 8:1-13

Na. 3: Yesu Alishindaje Ulimwengu?

Na. 4: Kuondolewa kwa Amri Kumi Hakumaanishi Kwamba Vizuizi vya Adili Viliondolewa (rs uku. 254 ¶1-2)

Julai 11 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 9-11 Wimbo 191

Sifa ya Usemi: Kutumia Vielelezo Mbele za Watu Wengi (be uku. 249 ¶3–uku. 250 ¶1)

Na. 1: Uthibitisho wa Kwamba Yesu Kristo Aliishi Duniani (w03 6/15 uku. 4-7)

Na. 2: 1 Wafalme 9:1-9

Na. 3: Maana ya Sabato kwa Wakristo (rs uku. 254 ¶3–uku. 256 ¶3)

Na. 4: Inawezekana Kushinda Mazoea ya Kutumia Dawa za Kulevya kwa Kufuata Kanuni za Biblia

Julai 18 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 12-14 Wimbo 162

Sifa ya Usemi: Kwa Nini Ni Muhimu Kusababu (be uku. 251 ¶1-3)

Na. 1: Mawazo Huongoza Kwenye Matendo, Kisha Matokeo (w03 1/15 uku. 30 ¶1-3)

Na. 2: 1 Wafalme 12:1-11

Na. 3: Jinsi Imani Inavyoweza Kutusaidia Kushinda Majaribu

Na. 4: Wale Ambao Biblia Inawaita Watakatifu (rs uku. 405 ¶1-3)

Julai 25 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 15-17 Wimbo 158

Sifa ya Usemi: Uanzie Wapi? (be uku. 251 ¶4–uku. 252 ¶3)

Na. 1: Jinsi ya ‘Kufahamu Mapenzi ya Yehova’ (w03 12/1 uku. 21 ¶3–uku. 23 ¶3)

Na. 2: w03 7/15 uku. 19 ¶15-17

Na. 3: Kwa Nini Hatupaswi Kusali kwa “Watakatifu”? (rs uku. 406 ¶1-3)

Na. 4: Roho Takatifu Inawafarijije Wakristo?

Ago. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 18-20 Wimbo 207

Sifa ya Usemi: Wakati wa Kukubali Maoni ya Wengine (be uku. 252 ¶4–uku. 253 ¶2)

Na. 1: Vijana, Tembeeni kwa Kumstahili Yehova (w03 10/15 uku. 23 ¶1–uku. 24 ¶1)

Na. 2: 1 Wafalme 18:1-15

Na. 3: Wakristo Wote Wanaweza Kuzaa Matunda Mengi

Na. 4: Ukweli Kuhusu Kuabudu Masalio na Mifano ya “Watakatifu” (rs uku. 407 ¶1–uku. 408 ¶1)

Ago. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 21-22 Wimbo 92

Sifa ya Usemi: Kuuliza Maswali na Kutoa Sababu (be uku. 253 ¶3–uku. 254 ¶2)

Na. 1: Suluhisho Lenye Kudumu la Umaskini (w03 8/1 uku. 4-7)

Na. 2: 1 Wafalme 21:15-26

Na. 3: Watakatifu wa Kweli Wakristo Hawajaondolewa Dhambi (rs uku. 408 ¶2)

Na. 4: Kwa Nini Ni Lazima Tuwe Wajasiri, na Tunawezaje Kukuza Sifa Hiyo?

Ago. 15 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 1-4 Wimbo 16

Sifa ya Usemi: Kutoa Sababu Zenye Kusadikisha Zinazotegemea Kabisa Neno la Mungu (be uku. 255 ¶1–uku. 256 ¶2)

Na. 1: Mlipokea Bure, Toeni Bure (w03 8/1 uku. 20-22)

Na. 2: 2 Wafalme 3:1-12

Na. 3: Kwa Nini Watu wa Kabla ya Gharika Waliishi kwa Miaka Mingi Sana?

Na. 4: Maandiko Hayafundishi Kwamba Wanadamu Wote Wataokoka (rs uku. 415 ¶1)

Ago. 22 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 5-8 Wimbo 193

Sifa ya Usemi: Sadikisha kwa Kutoa Uthibitisho (be uku. 256 ¶3-5)

Na. 1: Kujifunza Ustadi wa Kuwa na Busara (w03 8/1 uku. 29-31)

Na. 2: w03 8/1 uku. 19 ¶18-22

Na. 3: Je, Wanadamu Wote Wataokolewa Hatimaye? (rs uku. 415 ¶2)

Na. 4: Tunapaswa Kuziiga Sifa Gani Nzuri za Yona?

Ago. 29 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 9-11 Wimbo 129

Sifa ya Usemi: Kutoa Uthibitisho wa Kutosha (be uku. 256 ¶6–uku. 257 ¶3)

Pitio la Maswali na Majibu

Sept. 5 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 12-15 Wimbo 175

Sifa ya Usemi: Kujitahidi Kugusa Moyo (be uku. 258 ¶1-5)

Na. 1: Je, Unamtafuta Yehova kwa Bidii? (w03 8/15 uku. 25-28)

Na. 2: 2 Wafalme 12:1-12

Na. 3: Kwa Nini Tujitahidi Kuwa Wapole?

Na. 4: “Watu wa Namna Zote” Wataokoka (rs uku. 416 ¶1)

Sept. 12 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 16-18 Wimbo 203

Sifa ya Usemi: Kuwafanya Watu Waeleze Yaliyo Moyoni Mwao (be uku. 259 ¶1-3)

Na. 1: Watu Walikumbuka Nini Kuhusu Yesu? (w03 8/15 uku. 6 ¶5–uku. 8 ¶6)

Na. 2: 2 Wafalme 16:10-20

Na. 3: Biblia Inasema Kwamba Wengine Hawataokolewa Kamwe (rs uku. 416 ¶2-4)

Na. 4: Tunawezaje Kuhakikisha Lile Linalokubalika kwa Bwana?

Sept. 19 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 19-22 Wimbo 89

Sifa ya Usemi: Kuchochea Hisia Zinazofaa (be uku. 259 ¶4–uku. 260 ¶1)

Na. 1: “Endelea Kushika Kiolezo cha Maneno Yenye Afya” (w03 1/1 uku. 29 ¶3–uku. 30 ¶4)

Na. 2: 2 Wafalme 19:20-28

Na. 3: Mtu Akiokolewa, Je, Ameokolewa Sikuzote (rs uku. 417 ¶1-4)

Na. 4: Tunaweza Kujifunza Nini kwa Ndugu Zetu Wakristo Katika Smirna ya Kale?

Sept. 26 Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 23-25 Wimbo 84

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Kukuza Hofu ya Mungu (be uku. 260 ¶2-3)

Na. 1: Biblia na Vitabu Vyake Vinavyokubalika—Sehemu ya 1 (si uku. 299 ¶1-6)

Na. 2: w03 8/15 uku. 20 ¶6-10

Na. 3: Tunatarajia Mazuri Wakati Ujao

Na. 4: Kwa Nini Ni Lazima Matendo Yaambatane na Imani? (rs uku. 417 ¶5–uku. 418 ¶2)

Okt. 3 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 1-4 Wimbo 51

Sifa ya Usemi: Mungu Anajali Mwenendo Wetu Ukoje? (be uku. 260 ¶4-5)

Na. 1: Biblia na Vitabu Vyake Vinavyokubalika—Sehemu ya 2 (si uku. 300-302 ¶7-16)

Na. 2: 1 Mambo ya Nyakati 4:24-43

Na. 3: Tunajuaje Kwamba kwa Kweli Kuna Ibilisi (rs uku. 269 ¶3–uku. 270 ¶3)

Na. 4: Yehova Anatupenda Kila Mmoja

Okt. 10 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 5-7 Wimbo 195

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Kujichunguza (be uku. 261 ¶1-3)

Na. 1: Biblia na Vitabu Vyake Vinavyokubalika—Sehemu ya 3 (si uku. 302-305 ¶17-26)

Na. 2: 1 Mambo ya Nyakati 5:18-26

Na. 3: Yale Tunayojua Kuhusu “Siku ya Yehova”

Na. 4: Shetani Si Uovu Ulio Ndani ya Watu (rs uku. 270 ¶4–uku. 271 ¶2)

Okt. 17 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 8-11 Wimbo 201

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wasikilizaji Kutii kwa Moyo Wote (be uku. 261 ¶4–uku. 262 ¶3)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kiebrania ya Maandiko Matakatifu —Sehemu ya 1 (si uku. 305-306 ¶1-5)

Na. 2: 1 Mambo ya Nyakati 10:1-14

Na. 3: Mungu Hakumwumba Ibilisi (rs uku. 271 ¶3)

Na. 4: Tunapaswa Kuwatendea Nani kwa Busara?

Okt. 24 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 12-15 Wimbo 80

Sifa ya Usemi: Kushirikiana na Yehova Kufikia Mioyo ya Watu (be uku. 262 ¶4)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kiebrania ya Maandiko Matakatifu —Sehemu ya 2 (si uku. 306-307 ¶6-9)

Na. 2: w03 11/1 uku. 10-11 ¶10-13

Na. 3: Inamaanisha Nini Kweli Kutembea Katika Jina la Yehova?

Na. 4: Kwa Nini Mungu Hakumharibu Shetani Mara Alipoasi? (rs uku. 272 ¶1-2)

Okt. 31 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 16-20 Wimbo 129

Sifa ya Usemi: Kufaulu Kupima Wakati Vizuri (be uku. 263 ¶1–uku. 264 ¶4)

Pitio la Maswali na Majibu

Nov. 7 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 21-25 Wimbo 215

Sifa ya Usemi: Kutoa Himizo Linalofaa (be uku. 265 ¶1–uku. 266 ¶1)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kiebrania ya Maandiko Matakatifu —Sehemu ya 3 (si uku. 307-310 ¶10-16)

Na. 2: 1 Mambo ya Nyakati 22:1-10

Na. 3: Usipuuze Nguvu za Ibilisi (rs uku. 273 ¶1-3)

Na. 4: cJinsi Ndoa Inavyoweza Kuimarishwa

Nov. 14 Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 26-29 Wimbo 35

Sifa ya Usemi: Kuhimiza kwa Upendo (be uku. 266 ¶2-5)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kiebrania ya Maandiko Matakatifu —Sehemu ya 4 (si uku. 310-312 ¶17-25)

Na. 2: 1 Mambo ya Nyakati 29:1-9

Na. 3: Kwa Nini Watumishi wa Yehova Wanateswa?

Na. 4: Uvutano Mwovu wa Shetani Utakoma Karibuni (rs uku. 274 ¶2–uku. 275 ¶2)

Nov. 21 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 1-5 Wimbo 46

Sifa ya Usemi: Kuhimiza kwa Kutumia Maandiko (be uku. 267 ¶1-2)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kiebrania ya Maandiko Matakatifu —Sehemu ya 5 (si uku. 312-313 ¶26-31)

Na. 2: 2 Mambo ya Nyakati 2:1-10

Na. 3: Tambua Kusudi la Nidhamu

Na. 4: dJe, Mahusiano Yote ya Kingono Ni Mabaya (rs uku. 234 ¶1–uku. 235 ¶1)

Nov. 28 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 6-9 Wimbo 106

Sifa ya Usemi: Kuwa na ‘Uhuru wa Kusema’ (be uku. 267 ¶3-4)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kigiriki ya Kikristo ya Maandiko Matakatifu—Sehemu ya 1 (si uku. 315-316 ¶1-7)

Na. 2: w03 12/1 uku. 15-16 ¶3-6

Na. 3: Jinsi Tunavyoonyesha Kwamba Tuna Furaha Tele Katika Yehova

Na. 4: eMaoni ya Biblia Kuhusu Ngono Kati ya Watu wa Jinsia Moja (rs uku. 235 ¶3–uku. 236 ¶1)

Des. 5 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 10-14 Wimbo 116

Sifa ya Usemi: Kwa Nini Ni Muhimu Kuwa Mwenye Kutia Moyo? (be uku. 268 ¶1-3)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kigiriki ya Kikristo ya Maandiko Matakatifu—Sehemu ya 2 (si uku. 316-317 ¶8-16)

Na. 2: 2 Mambo ya Nyakati 12:1-12

Na. 3: Kwa Nini Tunahitaji Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu?

Na. 4: Mabadiliko Yaliyo ya Lazima ili Kumpendeza Mungu (rs uku. 236 ¶2–uku. 237 ¶1)

Des. 12 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 15-19 Wimbo 182

Sifa ya Usemi: Kuwakumbusha Wasikilizaji Matendo ya Yehova (be uku. 268 ¶4–uku. 269 ¶2)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kigiriki ya Kikristo ya Maandiko Matakatifu—Sehemu ya 3 (si uku. 317-319 ¶17-25)

Na. 2: 2 Mambo ya Nyakati 19:1-11

Na. 3: Mtu Mkamilifu Aliwezaje Kufanya Dhambi? (rs uku. 54 ¶3–uku. 55 ¶3)

Na. 4: Yale Tunayojifunza Kutokana na Familia ya Akina Yesu

Des. 19 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 20-24 Wimbo 186

Sifa ya Usemi: Kuonyesha Jinsi Ambavyo Yehova Amewasaidia Watu Wake (be uku. 269 ¶3-5)

Na. 1: Maandishi-Awali ya Kigiriki ya Kikristo ya Maandiko Matakatifu—Sehemu ya 4 (si uku. 319-320 ¶26-32)

Na. 2: w03 12/15 uku. 17 ¶13-15

Na. 3: Faida za Kujifunza Jinsi ya Kutosheka na Machache

Na. 4: Kwa Nini Tunapaswa Kutambua Uzito wa Dhambi? (rs uku. 56 ¶1–uku. 57 ¶1)

Des. 26 Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 25-28 Wimbo 137

Sifa ya Usemi: Kufurahia Matendo ya Mungu ya Sasa (be uku. 270 ¶1–uku. 271 ¶2)

Pitio la Maswali na Majibu

[Maelezo ya Chini]

a Wakati ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kuwajibu kwa njia inayofaa watu katika eneo lenu ambao wameshikilia maoni fulani-fulani na wanaopinga, na kadhalika.

b Wakati ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kuwajibu kwa njia inayofaa watu katika eneo lenu ambao wameshikilia maoni fulani-fulani na wanaopinga, na kadhalika.

c Mgawo wa ndugu pekee.

d Mgawo wa ndugu pekee.

e Mgawo wa ndugu pekee.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki