Jaribu Kutumia Utangulizi Unaoweza Kubadilishwa Ufaane na Hali
Tukipendezwa kikweli na watu tutajitahidi kutambua mahitaji yao na kuwaonyesha jinsi Ufalme utakavyotatua kabisa matatizo wanayokabili. (Flp. 2:4) Utangulizi ambao wahubiri wengi wameona kuwa wenye matokeo mazuri ni kumwuliza mwenye nyumba maoni yake kuhusu picha za Paradiso katika vichapo vyetu, kama zile ambazo zimeorodheshwa upande wa kulia wa ukurasa huu. Unaweza kutumia mojawapo ya tangulizi zifuatazo:
◼ “Je, unafikiri kwamba siku moja wanadamu wataweza kufurahia hali tunazoona katika picha hii?”
◼ “Sisi sote tungependa kuwaona watoto wetu wakiishi katika mazingira kama haya. Unafikiri hali hiyo inaweza kuletwa na nini?”
◼ “Picha hii inaonyesha jinsi dunia itakavyokuwa wakati ambapo mapenzi ya Mungu yatatendeka duniani kama vile mbinguni. Unaona mambo gani yaliyo tofauti na maisha ya leo?”
◼ “Je, ungependa kuishi katika mazingira yanayoonyeshwa katika picha hii? [Ngojea jibu.] Je, unafikiri kwamba tutaona mabadiliko hayo katika wakati wetu?”
Sikiliza kwa makini mtu anapojibu, na umwulize kwa fadhili swali moja au mawili ya ziada ili aeleze maoni yake. Watu fulani wakisema hawangetaka kuishi katika mazingira yanayoonyeshwa katika picha, au kwamba mambo hayo hayawezekani, usikate kauli haraka kwamba hawapendezwi. Waulize kwa busara sababu za maoni yao. Huenda ukagundua kwamba wanahangaishwa sana na matatizo yanayowakabili wanadamu, ambayo hayaonekani kuwa na suluhisho.—Eze. 9:4.
Unapotambua mahangaiko ya mwenye nyumba, yabadili mazungumzo yako kupatana na mahangaiko yake. Kazia jambo fulani katika ujumbe wa Ufalme linalolenga mahangaiko yake moja kwa moja. Mwonyeshe andiko moja au mawili yanayohusu jambo linalomtia wasiwasi, ili ajionee yale ambayo Neno la Mungu linasema. (Ona mapendekezo katika upande wa kulia wa ukurasa.) Akipendezwa, mwachie kichapo na upange kurudi. Unaporudi endeleza mazungumzo kwa kutaja kifupi yale mliyozungumzia katika ziara ya kwanza.
[Sanduku katika ukurasa wa 6]
Picha Mbalimbali za Paradiso
Kitabu Creation: ukurasa wa 237, 243, 251
Kitabu Mwalimu: ukurasa wa 251-254
Kitabu Ujuzi: ukurasa wa 4-5, 188-189
Broshua Anataka: ukurasa wa 11, 13
Kitabu Usalama wa Kweli: ukurasa wa 98
Kitabu Mwabudu Mungu: ukurasa wa 92-93
[Sanduku katika ukurasa wa 6]
Mambo Yanayowahangaisha Watu
Kifo, maombolezo
Kuharibiwa kwa dunia
Kushuka moyo
Kuwatenda wanyama kikatili
Magonjwa, ulemavu
Makao, matatizo ya uchumi
Serikali zilizoshindwa kusuluhisha matatizo
Ubaguzi, tofauti ya maisha kati ya matajiri na maskini
Ufisadi, ukosefu wa haki
Uhalifu, ujeuri
Ukosefu wa maadili
Umaskini, ukandamizaji
Upungufu wa chakula, utapiamlo
Vita, ugaidi