Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/05 kur. 3-5
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mkaribie Yehova
  • Je, Kuna Muumba Anayekujali?
  • Endeleeni Kukesha!
  • Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?
  • Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
  • Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Biblia —Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
  • Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Jinsi ya Kutoa Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma ya Ufalme—2006
  • (1) Swali, (2) Andiko, na (3) Sura
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Madokezo ya Utoaji wa Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kutoa Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 1/05 kur. 3-5

Tunza

Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani

Yatumie mapendekezo yafuatayo unapotayarisha mambo ya kusema utakapotoa kichapo cha kila mwezi.

Mkaribie Yehova

“Watu wengi wanaomwamini Mungu wangependa kuwa na uhusiano wa karibu zaidi naye. Je, unajua kwamba Mungu anatusihi tumkaribie? [Soma Yakobo 4:8.] Kitabu hiki kimekusudiwa kuwasaidia watu watumie Biblia zao kumkaribia Mungu.” Soma fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 16.

“Ukosefu wa haki umezidi leo. Ni kama andiko hili linavyosema. [Soma Mhubiri 8:9b.] Wengi hutilia shaka kama kweli Mungu anajali. [Soma sentensi mbili za kwanza katika fungu la 4 kwenye ukurasa wa 119.] Sura hii inaeleza kwa nini Mungu ameruhusu ukosefu wa haki kwa muda fulani.”

Je, Kuna Muumba Anayekujali?

“Tunaweza kupata wapi ushauri bora wa kutatua matatizo yetu makubwa? [Ngojea jibu, kisha usome Mathayo 7:28, 29.] Maneno haya yanaonyesha jinsi watu walivyoitikia Yesu alipotoa Mahubiri yake ya Mlimani. Ona kile ambacho wengine wamesema. [Mwonyeshe maelezo kwenye ukurasa wa 152.] Sura hii inazungumzia maisha na mafundisho ya Yesu.”

“Je, umewahi kujiuliza: ‘Ikiwa kuna Mungu, je, ataondoa kuteseka na ukosefu wa haki tunaouona kila mahali?’ [Ngojea jibu, kisha usome Ufunuo 21:3, 4.] Kitabu hiki kinaeleza kile ambacho Mungu atafanya ili kuondoa mateso yote na chanzo chake.” Mwonyeshe sura ya 10.

Endeleeni Kukesha!

“Watu wengi huhangaishwa na matatizo na matukio yenye kushtua yaliyo ya kawaida leo. [Taja jambo linalojulikana katika eneo lenu.] Je, unajua kwamba mambo kama hayo ni ishara inayoonyesha kwamba serikali ya Mungu itaanza kutawala dunia karibuni? [Ngojea jibu, kisha usome andiko moja linalofaa kama vile Mathayo 24:3, 7, 8; Luka 21:7, 10, 11; au 2 Timotheo 3:1-5.] Broshua hii inazungumzia sababu inayofanya iwe muhimu kutambua maana ya matukio ya siku zetu na tumaini la wanadamu.”

“Watu wengi leo hufadhaishwa na matukio yenye kushtua au kwa sababu ya kupatwa na msiba mbaya. Baadhi yao hujiuliza kwa nini Mungu hazuii mambo hayo yasitupate. Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu ataondoa taabu zote za wanadamu hivi karibuni. [Soma Ufunuo 14:6, 7.] Ebu ona faida ambazo hukumu ya Mungu itawaletea wanadamu. [Soma 2 Petro 3:10, 13.] Broshua hii ina habari nyingi zaidi kuhusu jambo hili muhimu.”

Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele

“Kama wewe ungealikwa kuishi katika mazingira mazuri kama haya, je, ungekubali? [Onyesha picha kwenye ukurasa 4-5, na ungojee jibu.] Ona kile ambacho Neno la Mungu linasema tunahitaji kufanya ili tupate kuishi maisha kama haya milele. [Soma Yohana 17:3.] Kitabu hiki kitakusaidia upate ujuzi unaoongoza kwenye uzima wa milele.” Panga kuzungumzia mafungu matano ya kwanza katika sura ya kwanza utakaporudi.

Fungua kitabu kwenye ukurasa wa 188-189, kisha yatumie maelezo ya picha na umwulize mwenye nyumba swali hili: “Je, watumaini kuishi katika Paradiso, wakati ujuzi juu ya Mungu unapoijaa dunia? [Ngojea jibu, kisha usome Isaya 11:9.] Kitabu hiki kinaweza kukusaidia ujifunze kile ambacho Biblia inasema kuhusu Paradiso na jinsi ambavyo tutapata kuishi humo.” Panga kuzungumzia fungu la 11-16 katika sura ya kwanza utakaporudi.

Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu

“Je, unafikiri kwamba ulimwengu ungekuwa mahali bora kama watu wangefuata maneno haya maishani mwao? [Soma Mathayo 7:12a, kisha ungojee jibu.] Kitabu hiki kinazungumzia mafundisho mengi ya yule mwalimu mkuu aliyepata kuishi.” Kazia picha na maelezo ya picha katika sura ya 17.

“Wazazi wengi leo wanajitahidi kuwafundisha watoto wao maadili bora. Je, unafikiri jambo hilo ni muhimu? [Ngojea jibu, kisha usome Methali 22:6.] Ona kwamba wazazi wanatiwa moyo kuanza kuwazoeza watoto wao tangu utotoni. Kitabu hiki kinaweza kuwasaidia wafanye hivyo.” Kazia picha na maelezo ya picha katika sura ya 15 au ya 18.

“Mara nyingi wazazi hushangazwa na maswali ambayo watoto wao huuliza. Inaweza kuwa vigumu kujibu baadhi ya maswali hayo, sivyo? [Ngojea jibu, kisha usome Waefeso 6:4.] Kitabu hiki kinaweza kuwasaidia wazazi wajibu maswali ya watoto wao.” Kazia picha chache na maelezo ya picha hizo katika sura ya 11 na 12 au 34 hadi 36.

Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?

“Sisi sote tuna wasiwasi kwa sababu ya uhalifu na ujeuri katika eneo letu. Je, unafikiri kwamba kuna mtu yeyote anayeweza kutatua matatizo haya? [Ngojea jibu.] Mungu ana suluhisho.” Fungua ukurasa wa 196; soma na ueleze Methali 2:21, 22 katika fungu la 19. Mwonyeshe kichwa cha sura ya 16, na umtolee kitabu.

Fungua ukurasa wa 6, na useme hivi: “Watu wengi huamini kwamba dunia yetu maridadi na viumbe wote walio hai walitokea wenyewe tu. Maoni yako ni nini kuhusu chanzo cha dunia na viumbe wote walio hai? [Ngojea jibu.] Kuna mambo mengi sana yanayothibitisha masimulizi ya Biblia kumhusu Muumba mwenye nguvu nyingi na anayetupenda sana. Yeye ndiye Mungu wa kweli, na jina lake ni Yehova.” Soma Zaburi 83:18, na ueleze kifupi jinsi atakavyofanya dunia nzima iwe paradiso.

Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu

“Kuna dini nyingi sana leo, sivyo? Je, umewahi kujiuliza jinsi tunavyoweza kujua ni ipi inayompendeza Mungu?” Baada ya kupata jibu, fungua ukurasa wa 377. Kazia jambo la 7, na umwulize mwenye nyumba kama anakubali kwamba dini ya kweli inapaswa kuleta umoja kati ya jamii zote za wanadamu. Fungua mojawapo ya maandiko yaliyotajwa, na ukiwa na nafasi, uyazungumzie mambo machache mengine katika orodha hiyo. Ikiwa mwenye nyumba anapendezwa kikweli, mtolee kitabu. Kabla ya kuondoka unaweza kumwuliza swali hili: “Dini ya kweli inapaswa kumsaidia mtu kuwa na mwenendo wa aina gani?” Panga ziara ya kurudia ili ujibu swali hilo.

Ikiwa mtu anataja kwamba yeye ni mfuasi wa dini fulani kubwa, unaweza kusema hivi: “Inapendeza kukutana na watu wa dini tofauti-tofauti. Watu wamemtafuta Mungu kwa njia mbalimbali. [Ikifaa, soma Matendo 17:26, 27.] Mara nyingi watu hufuata dini ya wazazi wao. [Soma fungu la 12 kwenye ukurasa wa 8.] Inaelimisha kujifunza kuhusu dini nyingine. Kitabu hiki kinaeleza chanzo, desturi, na mafundisho ya zile dini kubwa ulimwenguni.” Mwonyeshe mwenye nyumba kifupi kile ambacho kitabu kinasema kuhusu dini yake, kwenye mojawapo za kurasa zifuatazo: Dini ya Sikh (100-101); Uhindu (116-117); Dini ya Buddha (141); Dini ya Tao (164-166); Dini ya Confucius (177); Dini ya Shinto (190-195); Dini ya Kiyahudi (220-221); na Uislamu (289).

Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

“Huenda umesikia juu ya [taja jambo ambalo limetangazwa katika vyombo vya habari.] Watu wanapokufa bila kutarajiwa, wengi hujiuliza ikiwa kuna faraja yoyote ile kwa waliofiwa. Unaonaje?” Mruhusu mwenye nyumba kujibu, kisha ufungue ukurasa wa 299, na umwonyeshe picha ya ufufuo. Endelea kwa kusema: “Wengi wanashangaa kujua kwamba wenye haki na wasio haki pia watafufuliwa katika Paradiso duniani. [Soma andiko la Matendo 24:15 ambalo limenukuliwa katika fungu la 9 kwenye ukurasa wa 297, kisha umwonyeshe maelezo ya andiko hilo katika fungu la 10.] Kitabu hiki kinazungumzia mambo mengine mengi yenye kuvutia kuhusu kusudi la Mungu la wakati ujao.”

Biblia —Neno la Mungu au la Binadamu?

“Karibu kila mtu anakabili matatizo magumu siku hizi. Wengi huwaendea washauri mbalimbali ili wapate mwongozo. Wengine huwaendea wachawi. Unafikiri tunaweza kupata wapi ushauri mzuri ambao unaweza kutusaidia kwelikweli? [Ngojea jibu.] Biblia inataja jambo muhimu ambalo sisi sote tunahitaji kuelewa. [Soma 2 Timotheo 3:16, kisha ufungue ukurasa wa 187, na usome fungu la 9.] Kitabu hiki kitakusaidia kuelewa kwamba ushauri wa Biblia hutuletea manufaa sikuzote tukiufuata.”

Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi

“Watu wengi humkumbuka Yesu katika kipindi hiki cha Krismasi. Hata hivyo, kwa sababu mambo mengi yenye kuhuzunisha hutukia kotekote duniani, huenda wengine wakatilia shaka kama Yesu anatujali. Unaonaje?” Ngojea jibu. Fungua sura ya 24, na uzungumzie kifupi kwa nini Yesu alikuja duniani, kisha usome andiko la Yohana 15:13, na ukazie kwamba Yesu aliwapenda wengine kutoka moyoni.

“Yesu Kristo anapotajwa, wengi humfikiria kuwa mtoto mchanga au mtu anayeteseka ambaye anakaribia kufa. Hawajui mengi kumhusu Yesu ila kuzaliwa na kufa kwake. Mambo mazuri ajabu aliyosema na kutenda alipoishi duniani hupuuzwa mara nyingi. Kila mtu ambaye amepata kuishi duniani huguswa na yale aliyotenda na kufundisha. Kwa hiyo ni muhimu tujifunze mengi tuwezavyo kuhusu mambo mazuri aliyotufanyia.” Soma Yohana 17:3. Fungua ukurasa wa kwanza wa utangulizi na usome fungu la nne.

Mungu Anataka Tufanye Nini?

“Je, unafikiri Mungu alikusudia tuishi kwa taabu kama tunavyoishi leo? [Ngojea jibu, kisha usome Mathayo 6:10.] Je, umewahi kujiuliza Ufalme wa Mungu ni nini?” Fungua somo la 6, na usome maswali ya somo hili. Anza kuzungumzia somo hilo au upange kulizungumzia utakaporudi.

“Ijapokuwa wanadamu wamefanya maendeleo mengi siku hizi, bado magonjwa na kifo husababisha maumivu mengi na huzuni nyingi. Je, unajua kile ambacho Yesu atawafanyia wagonjwa, wazee, na hata wafu?” Ngojea jibu. Ikiwa mtu huyo anataka kujua jibu, fungua somo la 5, na umsomee maswali ya fungu la 5-6. Zungumzia mafungu hayo, au upange kuyazungumzia utakaporudi.

Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?

“Umewahi kujiuliza: Je, kifo ni mwisho kabisa wa mtu? Au kuna maisha mengine baada ya kifo?” [Ngojea jibu.] “Biblia inajibu maswali yote ambayo tunaweza kuwa nayo kuhusu kifo.” (Soma Mhubiri 9:5, 10.) Kisha fungua ukurasa wa 13 katika broshua Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai na uzungumzie kichwa kidogo, “Hali ya Wafu.”

“Umewahi kujiuliza babu zetu waliokufa zamani wako wapi? Je, wanaweza kutusaidia au kutudhuru?” [Ngojea jibu.] “Ona kile ambacho Biblia inasema kuwahusu wafu katika Zaburi 49.” (Soma Zaburi 49:10, 17-19.) Kisha zungumzia somo la 4 katika broshua.

Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli

“Unafikiri tunaweza kupata wapi msaada wa kushughulikia matatizo tunayokabili maishani? [Ngojea jibu, kisha usome Waroma 15:4.] Ona kwamba Maandiko matakatifu yanatupa mafundisho, tumaini, na faraja zinazoweza kutuimarisha kuvumilia magumu. Kitabu hiki kina mapendekezo mazuri ya jinsi ya kusoma Biblia ili tupate faida nyingi kutokana na usomaji wetu.” Kazia mambo manne yanayotajwa kwenye ukurasa wa 30.

“Tangu Yesu alipoishi duniani, watu wengi wamekuwa wakiomba Ufalme wa Mungu uje.” Umewahi kujiuliza wanadamu watafaidikaje Ufalme huo utakapokuja? [Ngojea jibu, kisha usome Danieli 2:44.] Kitabu hiki kinaeleza Ufalme wa Mungu ni nini na yale utakayotimiza. Kinaeleza pia jinsi tunavyoweza kunufaishwa na utawala huo wa uadilifu.” Onyesha picha kwenye ukurasa wa 92-93.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki