Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 uku. 1
  • Mshukuru Yehova kwa Fadhili Zake Zenye Upendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mshukuru Yehova kwa Fadhili Zake Zenye Upendo
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Hubariki Jitihada Zetu za Kuadhimisha Ukumbusho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • ‘Enyi Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Wasaidie Wengine Wafaidike na Fidia
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Kwa Nini Tunahudhuria Ukumbusho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 2/05 uku. 1

Mshukuru Yehova kwa Fadhili Zake Zenye Upendo

Kifo cha Kristo Kitakumbukwa Machi 24

1 Mtunga-zaburi alisema hivi kwa shauku: “Watu na wamtolee Yehova shukrani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.” (Zab. 107:8) Fadhili zenye upendo za Mungu hazimaanishi kwamba anawahurumia watu tu. Jambo hilo linaonyeshwa wazi katika maneno haya ya kumsifu Mungu yaliyoongozwa na roho takatifu: “Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, ziliendelea kunitegemeza.” (Zab. 94:18) Yehova alionyesha fadhili nyingi zenye upendo alipomtoa Mwana wake mzaliwa-pekee kwa ajili yetu.—1 Yoh. 4:9, 10.

2 Ukumbusho wa kifo cha Kristo unapokaribia tunawezaje kumshukuru “Mungu wa fadhili zenye upendo”? (Zab. 59:17) Sisi sote tunapaswa kutenga wakati wa kutafakari juu ya siku za mwisho za Yesu duniani. (Zab. 143:5) Tutafaidika pia kwa kusoma sehemu za Biblia ambazo tumepangiwa kusoma kabla ya Ukumbusho, kama inavyoonyeshwa katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2005 na, ikiwezekana, kusoma na kufanya utafiti katika sura ya 112-116 za kitabu Mtu Mkuu na vitabu vingine vinavyozungumzia Biblia. Tafakari sana juu ya sehemu ambazo unasoma, uzifikirie kwa makini. (1 Tim. 4:15) Tunaposali wakati wa kujifunza Neno la Mungu, moyo wetu unaimarishwa, na pia tunaonyesha kwamba tunampenda Yehova.—Mt. 22:37.

3 Wachochee Wengine Wamshukuru Mungu: Watu 16,760,607 walihudhuria Ukumbusho mwaka uliopita. Na miaka michache iliyopita, ndugu katika kijiji kimoja huko Liberia walimwandikia chifu wa mji fulani na kumweleza kwamba walitaka kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana katika mji wake. Chifu huyo aliwapa ndugu ruhusa ya kutumia uwanja wa mpira kwa ajili ya mwadhimisho huo, naye akautangaza katika sehemu hiyo yote na kuwakaribisha watu. Ijapokuwa kulikuwa na wahubiri watano tu katika kijiji hicho, watu 636 walihudhuria Ukumbusho!

4 Sisi vilevile tunataka kuwasaidia watu wengi iwezekanavyo kujiunga nasi tunapoadhimisha Ukumbusho. Kwa nini usiandike orodha ya majina ya wote unaotaka kuwaalika? Katika ukurasa wa nyuma wa toleo la Amkeni! la Machi 8 na Mnara wa Mlinzi la Machi 15 kuna mwaliko wa kuhudhuria Ukumbusho. Vikaratasi vya mwaliko wa Ukumbusho vinaweza kutumiwa pia. Chapa au uandike vizuri wakati na mahali pa Ukumbusho kwenye kikaratasi hicho, na umpe kila mtu ambaye unamwalika. Siku ya Machi 24 inapokaribia, mtembelee tena kila mtu uliyemwalika ili kumkumbusha, na kukamilisha mipango ya kuhudhuria Ukumbusho.

5 Tunawezaje kuwasaidia wanafunzi wa Biblia ambao hawajaanza kuhudhuria mikutano bado, ili wanufaike kikamili na mwadhimisho huo? Tumia dakika chache wakati wa kila funzo ili uwasaidie kuelewa umuhimu wa Ukumbusho. Unaweza kupata habari nzuri sana katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 2004, ukurasa wa 3-7, na kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 336-340.

6 Wakaribishe Wageni: Kwenye Ukumbusho, ongea na wageni na uwakaribishe. (Rom. 12:13) Panga uketi pamoja na wale ambao umewaalika, na uhakikishe kwamba wana Biblia na kitabu cha nyimbo. Tunataka hasa kuwakaribisha kwa moyo ndugu na dada wasiotenda ambao wamehudhuria. Tukionyesha kwamba tunawapenda na kuwajali, huenda jambo hilo likawasaidia kuanza kuhudhuria mikutano tena na kuhubiri kwa ukawaida. (Luka 15:3-7) Kwenye pindi hiyo takatifu, tufanye yote tuwezavyo kuwatia wengine moyo wajiunge nasi kumshukuru Yehova kwa ‘fadhili zake zenye upendo za ajabu.’—Zab. 31:21.

[Maswali ya Funzo]

1. Yehova ametuonyeshaje fadhili zenye upendo?

2. Tunawezaje kuonyesha shukrani zetu kwa Yehova?

3, 4. (a) Tunawezaje kuwaiga ndugu zetu huko Liberia? (b) Wewe umepanga kumwalika nani kwenye Ukumbusho?

5. Tunawezaje kuwatia moyo wanafunzi wa Biblia wahudhurie?

6. Kwa nini ni muhimu kuwakaribisha wageni kwenye Ukumbusho?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki