Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 14
  • Juma Linaloanza Februari 21
  • Juma Linaloanza Februari 28
  • Juma Linaloanza Machi 7
Huduma ya Ufalme—2005
km 2/05 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Februari 14

Wimbo 174

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu) ili kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 15 na Amkeni! la Januari 22. Onyesha kifupi jinsi mapendekezo hayo yanavyoweza kubadilishwa ili yafae eneo lenu.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, uku. 8.

Dak. 35: “Majira ya Ukumbusho Ni Wakati wa Kuongeza Utumishi.”a Mwangalizi wa utumishi atazungumzia habari hiyo. Unapozungumzia fungu la 6, toa maelezo mafupi kuhusu gazeti la Amkeni! la Septemba 8, 2004, ukurasa wa 12-13. Tangaza majina ya wale waliojiandikisha kuwa mapainia wasaidizi. Taja mikutano ya ziada ya utumishi iliyopangwa. Watie wote moyo wafanye zaidi katika huduma yao ya kiroho, kwa njia moja au nyingine, wakati wa majira haya ya Ukumbusho.

Wimbo 14 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 21

Wimbo 31

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu katika sanduku kwenye ukurasa wa 6, “Wasaidie Wapate Ushahidi Zaidi.” Watie moyo wote wajaze fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43-SW) wakati inapofaa, bila kuchelewa.

Dak. 20: “Mshukuru Yehova kwa Fadhili Zake Zenye Upendo.”b Tangaza wakati na mahali pa Ukumbusho pamoja na jina la msemaji na mambo mengine yanayohusika. Unapozungumzia fungu la 4, panga onyesho la mhubiri anayemwalika kwenye Ukumbusho mtu ambaye anampelekea magazeti kwa ukawaida. Ndugu wanapaswa kupewa vikaratasi vya mwaliko wa Ukumbusho kwenye mkutano huu, ikiwa hawajavipata bado.

Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 6.”c Panga onyesho la dakika nne kumhusu mwanafunzi wa Biblia anayeuliza kwa nini ni watu wachache sana kati ya wale wanaohudhuria Ukumbusho wanakula mkate na kunywa divai. Yule anayeongoza funzo anampongeza kwa swali lake, analiandika, na kupendekeza walizungumzie baada ya kujifunza somo la juma hilo. Baada ya funzo, yule anayeongoza anamwonyesha mwanafunzi habari zilizo chini ya swali “Ni Nani Wanaopaswa Kula Mkate na Kunywa Divai?” kwenye ukurasa wa 338 katika kitabu Kutoa Sababu. Wanasoma sehemu hiyo pamoja na mwanafunzi anashukuru kwa kupata jibu linaloeleweka vizuri kwa swali lake.

Wimbo 21 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 28

Wimbo 42

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Februari. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu), ili kuonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari 8. Mnaweza kutumia njia nyingine zinazofaa. Mwishoni mwa onyesho, mhubiri anamwalika mwenye nyumba kwenye Ukumbusho kwa kutumia ukurasa wa mwisho wa gazeti la Amkeni! la Machi 8 au vikaratasi vya mwaliko vilivyochapwa.

Dak. 20: Onyesha Kwamba Unawajali Walio Dhaifu. (Mdo. 20:35) Baada ya utangulizi usiozidi dakika moja, zungumzia kwa maswali na majibu gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 2004, ukurasa wa 17-18, fungu la 12-16, kama inavyofanywa kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi. Ndugu aliye msomaji mzuri asome mafungu. Kazia hasa jinsi habari hizo zinavyoweza kutumiwa kuhusiana na Ukumbusho na hotuba ya pekee inayokaribia.

Dak. 10: Toa Endeleeni Kukesha! Zungumzia na upange maonyesho ya jinsi ya kutoa broshua hiyo mwezi wa Machi. Unaweza kutumia mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005 au njia nyingine zinazofaa kwenye eneo lenu.

Wimbo 72 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 7

Wimbo 12

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu katika sanduku la “Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho.”

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Toa Magazeti Katika Huduma.”d Unapozungumzia fungu la 3 na 4, onyesha jinsi ya kutumia habari hizo katika eneo lenu. Hoji kwa ufupi mhubiri mmoja au wawili walio na matokeo mazuri katika kazi ya magazeti kwenye eneo la biashara, barabarani, sehemu za umma, au kila wanapopata fursa. Waombe waeleze jinsi wanavyotoa magazeti katika sehemu hizo. Panga onyesho fupi, au mhubiri aonyeshe jinsi alivyotoa magazeti kwa mafanikio.

Wimbo 192 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki