Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/06 uku. 5
  • Msaada Unaopatikana kwa Utayari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaada Unaopatikana kwa Utayari
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Uangalizi Wenye Upendo Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kutaniko la Kikristo—Chanzo cha Msaada Wenye Kutia Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Fanya Zaidi ya Kusema Tu: ‘Ukaote Moto na Kushiba’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 2/06 uku. 5

Msaada Unaopatikana kwa Utayari

1 Anna, ni dada ambaye hufanya kazi inayochukua muda wake mwingi, na mume wake si mwamini. Ilikuwa vigumu kwake kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida, kushiriki katika huduma, na kujifunza Neno la Mungu. Ingawa bado alimpenda Yehova, aliacha kuhubiri. Jambo la kufurahisha ni kwamba alipokea msaada wa kiroho kutoka kwa wazee wenye kujali.

2 Kukubali msaada wa kiroho unaotolewa na kutaniko la Kikristo huonyesha kwamba tunamtegemea Yehova mwenyewe. Kwa kuiga utunzaji wenye upendo wa Yesu Kristo, wazee wa kutaniko hutafuta nafasi za kuwatia moyo na kuwapa msaada unaofaa wale wanaokabili matatizo ya kiroho. (1 The. 5:14) Huenda mara nyingi mtu akahitaji kusikia maneno yanayotia moyo kutoka kwa Maandiko yenye kujenga. Kuchukua hatua ya kuwategemeza wale ambao wamekuwa dhaifu kwa muda mfupi ni jambo linalopaswa kufanywa na kila Mkristo, si wazee peke yao. Bila shaka kila mmoja wetu ameona matokeo ya “neno linalosemwa wakati unaofaa.”—Met. 25:11; Isa. 35:3, 4.

3 Chukua Hatua ya Kwanza: Ili tuwaonyeshe upendezi wale wanaohitaji msaada, lazima tuchukue hatua ya kwanza, tuonyeshe hisia-mwenzi, na tuwe na bidii. Yonathani alipotambua hali ya Daudi yenye kufadhaisha, ‘alisimama, akaenda kwa Daudi kule Horeshi, ili autie nguvu mkono wake.’ (1 Sam. 23:15, 16) Wasaidie wengine kwa upole. Maneno yanayoonyesha upendezi wa kweli ndiyo yenye matokeo zaidi. Isitoshe, Yesu alionyesha kuwa ili kumpata ndugu au dada wa kiroho unahitaji kujitahidi kwa bidii ukiwa na lengo fulani akilini. (Luka 15:4) Tukiwa na tamaa kubwa ya kumsaidia mtu mwingine tutachochewa kuendelea kutoa msaada hata ikiwa hafanyi maendeleo haraka.

4 Inatia moyo kama nini tunapochukua hatua ya kwanza kuwakaribisha wengine, kama vile wale walio katika funzo letu la kitabu, waandamane nasi katika huduma! Tunapomsaidia mtumishi mwenzetu wa Yehova ashiriki katika huduma, tunaweza kutumia fursa hiyo kumtia moyo afanye mengi zaidi katika utumishi wa Mungu. Pindi kama hizo zenye furaha tunazotumia katika utumishi wa Yehova ni zenye kutia moyo hasa kwa wale ambao wanajaribu kuwa na usawaziko wa kiroho tena.

5 Uandalizi wa Upendo: Huenda wale ambao hawajahubiri au kuhudhuria mikutano kwa muda fulani wakahitaji msaada wa ziada ili kuimarisha imani yao. Huenda wakahitaji kujifunza Biblia kwa kutumia kitabu kama vile Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, Mkaribie Yehova, au Biblia Inafundisha Nini Hasa? Kwa kuwa mtu huyo amebatizwa, kwa kawaida si lazima funzo hilo liongozwe kwa muda mrefu sana. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kuwa chonjo kuangalia ni nani wanaoweza kunufaika kutokana na uandalizi huo.—Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1998 na Novemba 2000.

6 Anna, aliyetajwa awali, alikubali kwa shukrani wazee walipomwomba dada aliyekomaa kiroho ajifunze Biblia pamoja naye. Alimkaribia Yehova tena baada tu ya kujifunza mara nne. Alianza tena kuhudhuria mikutano ya kutaniko naye akawa tena na tamaa ya kumsifu Yehova Mungu hadharani. Dada huyo aliyekomaa alimsaidia pia katika huduma kwa kumpeleka kwa mafunzo mengine ya Biblia hadi alipopata nguvu za kutosha kuhubiri nyumba kwa nyumba. Alihitaji tu msaada wenye fadhili ili arudie hali yake ya kiroho!

7 Kila mtu hupata baraka kwa kuwaimarisha wale wanaohitaji msaada. Yule anayesaidiwa hupata furaha ya kumkaribia Yehova na kushiriki katika utendaji wa tengenezo Lake. Wazee hushangilia kuona maendeleo kama hayo ya kiroho. (Luka 15:5, 6) Washiriki wa kutaniko huwa na uhusiano mzuri na hilo hutokeza umoja kwani kila mmoja humjali mwenzake kwa upendo. (Kol. 3:12-14) Tuna sababu nzuri ajabu za kumwiga Yehova ambaye ni msaada unaopatikana kwa utayari!—Efe. 5:1.

[Maswali ya Funzo]

1. Mtu anawezaje kuwa dhaifu kiroho?

2. Wakristo wote wanaweza kuwa msaada unaopatikana kwa utayari katika njia gani?

3, 4. Kuwasaidia wengine kunatia ndani nini, nasi tunaweza kufanyaje hivyo?

5. Katika hali fulani, ni msaada gani ambao wazee wanaweza kutoa?

6. Dada mmoja alipataje tena nguvu za kiroho?

7. Tunapata manufaa gani kwa kuwaimarisha wengine kiroho?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki