Matangazo
◼ Machi: Tutatoa kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu waliopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutawatolea hasa kile kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tunapaswa kuwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia tukitumia kitabu hicho. Juni: Tutatoa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu lakini mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Aprili una miisho-juma mitano, huo ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Ukumbusho utaadhimishwa Jumatano, Aprili 12, 2006. Ikiwa kutaniko lenu linafanya mikutano Jumatano, mikutano hiyo inapaswa kufanywa siku tofauti. Jambo hilo lisipowezekana kwa sababu makutaniko mengine yanatumia Jumba la Ufalme siku zile nyingine, sehemu za Mkutano wa Utumishi zilizo muhimu sana kwa kutaniko lenu zinaweza kushughulikiwa katika Mkutano mwingine wa Utumishi.
◼ Wahubiri wanapaswa kupewa matoleo mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yafikapo. Hilo litawawezesha kufahamu habari iliyomo kabla ya kuyatoa magazeti hayo katika utumishi wa shambani. Pia, wahubiri wanapaswa kupewa Huduma Yetu ya Ufalme mara tu inapofika. Wanaweza kupewa nakala zao kupitia mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Video Noah—He Walked With God itazungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi mwezi wa Mei mahali ambapo inapatikana. Ikihitajika, video hiyo inaweza kuagizwa kupitia kutaniko haraka iwezekanavyo.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza kichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali shughulikieni ifaavyo bidhaa za ombi la pekee.