Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho
Siku ya Ukumbusho mwaka huu ni Jumatano, Aprili 12. Wazee wanapaswa kukumbuka mambo yafuatayo.
◼ Mnapopanga saa ya mkutano huo, hakikisheni kwamba mkate na divai havitapitishwa kabla ya jua kushuka.
◼ Wote, kutia ndani msemaji, wanapaswa kujulishwa saa na mahali pa maadhimisho.
◼ Fanyeni mipango mapema ili kuwe na mkate na divai inayofaa.—Ona toleo la Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 2003, uku. 14-15.
◼ Sahani, glasi, meza na kitambaa cha meza vinavyofaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine ambapo maadhimisho hayo yatafanywa panapaswa kusafishwa mapema.
◼ Wakaribishaji na wale watakaopitisha mkate na divai wanapaswa kuteuliwa na kuelezwa mapema juu ya wajibu wao, utaratibu unaofaa kufuatwa, na umuhimu wa kuwa nadhifu na kuvalia mavazi yenye kuheshimika.
◼ Pangeni kuandaa mkate na divai kwa ajili ya watiwa-mafuta walio wagonjwa na wasioweza kuhudhuria.
◼ Ikiwa makutaniko zaidi ya moja yatatumia Jumba la Ufalme lilelile, mipango mizuri inahitajika ili kusiwe na msongamano usio wa lazima kwenye Jumba, milangoni, nje ya Jumba, au kwenye maegesho ya magari.