Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/06 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 11
  • Juma Linaloanza Desemba 18
  • Juma Linaloanza Desemba 25
  • Juma Linaloanza Januari 1
Huduma ya Ufalme—2006
km 12/06 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 11

Wimbo 174

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Novemba 15 na Amkeni! la Novemba. Katika mojawapo ya maonyesho, onyesha jinsi tunavyoweza kushughulikia kizuia mazungumzo “Mimi sipendezwi.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 16.

Dak. 15: Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2007. Hotuba pamoja na mahojiano yashughulikiwe na mwangalizi wa shule. Zungumzia mambo yanayohitaji kukaziwa katika kutaniko lenu kutoka nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2006. Eleza kwamba mwangalizi wa shule hataji mapema sifa ya usemi ambayo mwanafunzi anafanyia kazi. Kwa kuwa tutamaliza kusoma Maandiko ya Kiebrania kutoka Isaya 24 hadi Malaki mwaka wa 2007, mwaka huo utakuwa wakati unaofaa kwa ndugu ambao wamegawiwa mambo makuu ya usomaji wa Biblia na wengine wanaotoa maelezo wafanye utafiti katika vichapo vinavyozungumzia vitabu hivyo vya kinabii. Wahoji wahubiri wawili au watatu kutoka vikundi vifuatavyo: mwanafunzi mpya, mwanafunzi kijana ambaye anafanya maendeleo, na mwanafunzi mwenye uzoefu. Waombe waeleze jinsi ambavyo shule hii imewafaidi katika huduma na hali yao ya kiroho. Watie wote moyo wajitahidi kutimiza migawo yao, washiriki kutoa maelezo kuhusu usomaji wa Biblia, na kutumia mapendekezo wanayopata kila juma kutoka kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.

Dak. 20: “Msiache Upendo Mliokuwa Nao Mwanzoni.”a Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo yametajwa bila kunukuliwa.

Wimbo 193 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 18

Wimbo 150

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Pitia Sanduku la Swali. Taja mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya Desemba 25 na Januari 1.

Dak. 15: “Warudie Wote Wanaopendezwa kwa Kadiri Fulani.”b Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamefaulu kupata anwani za watu wenye kupendezwa waliokutana nao walipokuwa wakihubiri barabarani au isivyo rasmi. Waombe wasimulie mambo yenye kupendeza waliyoona walipowarudia watu hao. Unaweza kupanga mapema mhubiri mmoja au wawili watoe maelezo.

Dak. 20: “Roho ya Kujitolea Huleta Baraka.”c Hoji mhubiri mmoja au wawili ambao wanajulikana kwa roho yao ya kujitolea. Wameonyeshaje roho ya kujitolea? Imewabidi kufanya marekebisho gani, na ni nini kimewasaidia kuyafanya? Wamepata baraka gani?

Wimbo 108 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 25

Wimbo 210

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na Amkeni! la Desemba. Baada ya kila onyesho, mhubiri aulize swali lenye kuchochea fikira linaloweza kujibiwa katika ziara itakayofuata akitumia kitabu Biblia Inafundisha.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu na Kikumbusho.

Dak. 20: “Je, Una Eneo la Kibinafsi?”d Tia ndani maelezo mafupi kutoka kwa mwangalizi wa utumishi kuhusu mipaka ya eneo la kutaniko lenu, mara ambazo eneo hilo limehubiriwa, na uwezekano wa kuwa na maeneo ya kibinafsi.

Wimbo 219 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 1

Wimbo 158

Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za mwezi wa Desemba. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Kutoa Ripoti ya Maendeleo ya Huduma. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, kuanzia kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 83 hadi mwisho wa sura hiyo.

Dak. 23: “Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la 2007 la ‘Mfuateni Kristo!’”e Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Watie moyo wote wafanye mipango mapema iwezekanavyo ili wahudhurie kusanyiko.

Wimbo 65 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki