Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/07 uku. 7
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 2/07 uku. 7

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Februari 26, 2007. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Januari 1 hadi Februari 26, 2007. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Ni wakati gani tunapaswa kuwaeleza wasikilizaji jinsi wanavyoweza kutumia habari tunayotoa, na tutafanyaje hivyo? [be uku. 158 fu. 1-3]

2. Kwa nini ni muhimu tuwaonyeshe wengine faida ya habari tunayozungumzia, na tunaweza kufanyaje hivyo? [be uku. 159 fu. 3-4]

3. Kwa nini ni muhimu kutumia maneno yanayofaa? [be uku. 160]

4. Ni nini kitakachotusaidia tutumie semi tofauti-tofauti kwa usahihi? [be uku. 161 fu. 5-6; uku. 162 fu. 1, 4]

5. Taja baadhi ya faida za kuzungumza ukitegemea muhtasari ambao umeandikwa au muhtasari ambao umeshika akilini. [be uku. 166 fu. 1-3]

HOTUBA NA. 1

6. Kujitayarisha kusoma mbele ya watu kunahusisha nini? [be uku. 43 fu. 2, 4]

7. Ni nini kinachohitajiwa ili tumwige Yehova katika kupenda yaliyo sawa na kuchukia yaliyo makosa? (Ebr. 5:14) [w05 1/1 uku. 9 fu. 11]

8. Tunapaswa kukumbuka nini tunaposoma habari fulani katika Biblia ambayo inatufanya tutilie shaka kama Mungu alitenda kwa njia iliyo sawa au ya haki? [w05 2/1 uku. 24 fu. 7]

9. Tufanyeje iwapo matakwa ya wanadamu yanapingana na sheria ya Mungu? [w05 4/15 uku. 12 fu. 9]

10. Kitabu cha Isaya chakaziaje uangalifu kwenye Ufalme mikononi mwa Mesiya, na kwa yule mtangulizi, Yohana Mbatizaji? [si uku. 123 fu. 35]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. “Kifuniko” na “mfumo uliofumwa” unaotajwa kwenye Isaya 25:7 ni nini?

12. Watu wanawezaje ‘kumwona’ na ‘kumsikia’ Yehova? (Isa. 30:20, 21)

13. Kweli au Si kweli: Hezekia alitoa sala iliyo katika Isaya 38:3 kwa sababu tu alitamani kuishi muda mrefu?

14. Waisraeli wangewezaje kutumikia wakiwa mashahidi wa Yehova, nasi tunaweza kuwaigaje? (Isa. 43:10)

15. Kupatana na kielelezo cha kinabii kinachotajwa kwenye Isaya 52:11, 12, ni nini kinachohitajika kwa wale ‘wanaovichukua vyombo vya Yehova?’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki