Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova na kitabu Ujuzi. Machi: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha na tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu waliopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee ya kitheokrasi lakini hawashiriki sana na kutaniko, tutajitahidi kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, tukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaoshindwa kutimiza takwa la saa, wazee wanapaswa kupanga kuwasaidia. Madokezo yanapatikana katika barua za kila za S-201.
◼ Kichwa cha hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ni, “Unaweza Kuhisi Salama Katika Ulimwengu Huu Wenye Taabu!” Ona tangazo linalohusiana na hili kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2006.