Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Februari 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi tunavyoweza kutoa Mnara wa Mlinzi la Januari 15 na Amkeni! la Januari. Katika mojawapo ya maonyesho hayo, onyesha jinsi tunavyoweza kushughulikia kizuia-mazungumzo “Sipendezwi na dini.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 16-17.
Dak. 35: “Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova.”a Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Mahali panapofaa katika mazungumzo hayo, tangaza wakati na mahali pa Ukumbusho, mipango kwa ajili ya mikutano ya ziada ya utumishi wa shambani, na mradi wa kutaniko wa mapainia wasaidizi mwezi wa Aprili.
Wimbo 147 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 19
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: “Mwige Mwalimu Mkuu Unapotumia Kitabu Biblia Inafundisha.”b Mnapozungumzia fungu la 6, toa onyesho fupi la mhubiri akitumia sanduku mwishoni mwa sura ya 6 katika kitabu Biblia Inafundisha ili kupitia sura hiyo na mwanafunzi.
Dak. 20: Je, Unaweza Kuanzisha Funzo la Biblia Mwezi wa Machi? Mazungumzo na wasikilizaji. Sehemu ya kwanza ya mwezi wa Machi, tutatoa kitabu Biblia Inafundisha tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitieni mapendekezo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2006, ukurasa wa 3-6. Ukitumia moja kati ya mapendekezo kwenye ukurasa wa 6 au utoaji mwingine unaofaa eneo lenu, toa onyesho la jinsi tunavyoweza kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Waombe wasikilizaji watoe maelezo ya mambo waliyoona walipotoa kitabu hicho, hasa kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Wimbo 220 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 26
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au utoaji mwingine unaofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi tunavyoweza kutoa Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na Amkeni! la Februari. Katika mojawapo ya maonyesho hayo, mhubiri awe akihubiri katika eneo la biashara.
Dak. 15: “Usiwasahau Wasiotenda.”c Tia ndani maelezo katika Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 2004, ukurasa wa 21-22, mafungu 13-16.
Dak. 20: “Mwige Kristo Katika Huduma Yako.”d Kadiri wakati unavyoruhusu, wakaribishe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyoonyeshwa.
Wimbo 18 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 5
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Habari za Kitheokrasi. Mpe kila mtu aliyehudhuria nakala ya mwaliko wa pekee wa Ukumbusho, na utaje mipango ya kutaniko lenu ya kugawa mialiko hiyo katika eneo lenu. Watie moyo wahubiri wote washiriki kikamili. Panga kuwe na onyesho la jinsi ya kutumia mwaliko huo.
Dak. 15: Kuhubiri Habari Njema kwa Utaratibu. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, kuanzia kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 102 hadi mwisho wa sura hiyo.
Dak. 15: “Tumekabidhiwa Hazina.”e Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa.
Wimbo 104 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.